ESPRESSO COFFEE
JF-Expert Member
- Sep 6, 2014
- 6,170
- 7,665
Habarini,
Kwasasa Timu Ya Taifa Ya Tanzania kwa upande wa Wanaume kwenye mpira wa miguu, Kwa Miaka Mingi Imekuwa haifanyi vizuri katika Mashindano Ya Timu za Taifa. Hii inatokana na kukosa Wachezaji wenywe uwezo wa Kupambana na Kuleta Matokeo Chanya.
Ni wakati sasa Wa Shirikisho La Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuanzisha Ligi ya Wanachuo Tanzania ikihusisha Vyuo Mbalimbali Vilivyopo Nchini ili kuweza kuibua Vipaji vitakavyo Isaidia Timu Ya Taifa. Kunaweza Kusiwe na matokeo Ya Haraka Katika Kupata Vipaji lakini naamini Mbeleni Kunaweza Kuleta Matokeo Chanya.
Ni Ushauri Wangu Kuwa Kuwe Kuna Ligi ambayo itahusisha Vyuo mbalimbali, Kuanzia Vyuo Vikuu, Vyuo vya Kati na Vyuo Vingine ili wanafunzi Waweze Kuonesha uwezo wao na baadae kuisaidia Timu ya Taifa. Hii pia Itawasaidia Wanafunzi Kujipatia Vipato vyao kupitia Mishahara na Kujikimu kwa namna Mbalimbali.
Chuo ambacho kitawezesha Timu yake kushinda hii ligi, Basi TFF waweke utaratibu kwa Kushirikiana na Bodi ya Ligi kuhakikisha Kuwa Timu inatakayo ongoza Ligi iwezi kuingia Moja Kwa Moja Kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara. Kama Ilivyo Kwa Ligi Daraja La Pili na Ligi Daraja la kwanza Basi Kuwe na Ligi ya Vyuo Tanzaia, Na Wanavyuo Waweze Kuonesha Uwezo wao kupitia Hii Ligi.
Kwa Muda Mrefu sasa, Michezo Vyuoni Imekuwa Ikisahaulika na Wanafunzi wamekuwa Wakifanya Kwa kujifurahisha Tuuu bila kuwa na malengo maalumu au mipango madhubuti ya Michezo Vyuoni. Hii inachangakiwa sana Na Kukosa ‘Support’ kutoka Kwa Mamlaka Zinazo simamia Michezo Nchini.
Ni ukweli usio pingika kuwa Vyuo vinabeba Vijana wengi wenye vipaji vikubwa katika Michezo, Hasa Mpira wa Miguu. Kama TFF itaweza kutumia Kundi Kubwa hili la Vijana Katika Kupata Na Kuibua Vipaji basi ni wakati sasa wa Kuanza Huu mchakato kwa kushirikiana na Wizara Ya Elimu Nchini.
TFF isaidie kusimimamia Hii Ligi, Kutafura Wadhamini na wawekezaji Katika Hizi Timu ili ziweze kujiendesha. Tujiulize swali, Je Kijana Kama Kelvin John Angekuwa Mwanachuo Hapa Nchini inamaana kuwa kipaji chake kingepotea bila kuonekana. Je Ni Vipaji vya Vijana Wangapi Vinapotea Hapa Nchini kwa Kua wapo Chuoni?
Ni wakati sasa wa TFF kuangalia hili kundi muhimu nchini na Kuwasadia Hawa Vijana ili waweze kuonesha uwezo wao wanapo kuwa vyuoni na mara baada ya Kumaliza Chuo waweze kujiunga na Timu Mbalimbali Nje na Ndani ya Nchi.
Ni matumaini Yangu kuwa TFF, Bodi ya Ligi, Wizara ya Elimu na Vyuo Hapa Nchini vikiamua Kuanzisha Huu Mchakato Unawezekana Bila Shida Yoyote.
Miaka 3, 4,5 au 2 Ambayo kijana Anatumia Kuwa Chuoni atumie kuonesha Uwezo wake katika Mpira wa miguu na Kumuandaa na Maisha Ya Baadae na kusaidia Taifa lake.
Huu ndio wakati sasa.
Kwasasa Timu Ya Taifa Ya Tanzania kwa upande wa Wanaume kwenye mpira wa miguu, Kwa Miaka Mingi Imekuwa haifanyi vizuri katika Mashindano Ya Timu za Taifa. Hii inatokana na kukosa Wachezaji wenywe uwezo wa Kupambana na Kuleta Matokeo Chanya.
Ni wakati sasa Wa Shirikisho La Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuanzisha Ligi ya Wanachuo Tanzania ikihusisha Vyuo Mbalimbali Vilivyopo Nchini ili kuweza kuibua Vipaji vitakavyo Isaidia Timu Ya Taifa. Kunaweza Kusiwe na matokeo Ya Haraka Katika Kupata Vipaji lakini naamini Mbeleni Kunaweza Kuleta Matokeo Chanya.
Ni Ushauri Wangu Kuwa Kuwe Kuna Ligi ambayo itahusisha Vyuo mbalimbali, Kuanzia Vyuo Vikuu, Vyuo vya Kati na Vyuo Vingine ili wanafunzi Waweze Kuonesha uwezo wao na baadae kuisaidia Timu ya Taifa. Hii pia Itawasaidia Wanafunzi Kujipatia Vipato vyao kupitia Mishahara na Kujikimu kwa namna Mbalimbali.
Chuo ambacho kitawezesha Timu yake kushinda hii ligi, Basi TFF waweke utaratibu kwa Kushirikiana na Bodi ya Ligi kuhakikisha Kuwa Timu inatakayo ongoza Ligi iwezi kuingia Moja Kwa Moja Kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara. Kama Ilivyo Kwa Ligi Daraja La Pili na Ligi Daraja la kwanza Basi Kuwe na Ligi ya Vyuo Tanzaia, Na Wanavyuo Waweze Kuonesha Uwezo wao kupitia Hii Ligi.
Kwa Muda Mrefu sasa, Michezo Vyuoni Imekuwa Ikisahaulika na Wanafunzi wamekuwa Wakifanya Kwa kujifurahisha Tuuu bila kuwa na malengo maalumu au mipango madhubuti ya Michezo Vyuoni. Hii inachangakiwa sana Na Kukosa ‘Support’ kutoka Kwa Mamlaka Zinazo simamia Michezo Nchini.
Ni ukweli usio pingika kuwa Vyuo vinabeba Vijana wengi wenye vipaji vikubwa katika Michezo, Hasa Mpira wa Miguu. Kama TFF itaweza kutumia Kundi Kubwa hili la Vijana Katika Kupata Na Kuibua Vipaji basi ni wakati sasa wa Kuanza Huu mchakato kwa kushirikiana na Wizara Ya Elimu Nchini.
TFF isaidie kusimimamia Hii Ligi, Kutafura Wadhamini na wawekezaji Katika Hizi Timu ili ziweze kujiendesha. Tujiulize swali, Je Kijana Kama Kelvin John Angekuwa Mwanachuo Hapa Nchini inamaana kuwa kipaji chake kingepotea bila kuonekana. Je Ni Vipaji vya Vijana Wangapi Vinapotea Hapa Nchini kwa Kua wapo Chuoni?
Ni wakati sasa wa TFF kuangalia hili kundi muhimu nchini na Kuwasadia Hawa Vijana ili waweze kuonesha uwezo wao wanapo kuwa vyuoni na mara baada ya Kumaliza Chuo waweze kujiunga na Timu Mbalimbali Nje na Ndani ya Nchi.
Ni matumaini Yangu kuwa TFF, Bodi ya Ligi, Wizara ya Elimu na Vyuo Hapa Nchini vikiamua Kuanzisha Huu Mchakato Unawezekana Bila Shida Yoyote.
Miaka 3, 4,5 au 2 Ambayo kijana Anatumia Kuwa Chuoni atumie kuonesha Uwezo wake katika Mpira wa miguu na Kumuandaa na Maisha Ya Baadae na kusaidia Taifa lake.
Huu ndio wakati sasa.