Ushauri kwa vijana waliyohitimu vyuoni

Ushauri kwa vijana waliyohitimu vyuoni

Mparee2

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2012
Posts
3,092
Reaction score
5,386
Mkipata kazi kwanza mjue mlichojifunza Chuoni ni kama 60% hivyo mnahitaji kujifunza kwa haraka majukumu mtakayo pangiwa bila dharau kwa mtakao wakuta. Degree inakusaidia kupata kazi ila haikusaidii kuendelea kubakia kazini.

Kitakachokufanya usalie kazini na kuendelea kula mema ya nchi ni kama utafanya yafuatayo;

1. Kufanya kazi kwa bidii na kukamilisha majukumu yako kwa USAHIHI na kwa wakati.

2. Kuwasiliana/Communication kama kuna kitu umeshindwa/huelewi uliza ili uelekezwe ili usiharibu au kushindwa kumaliza kwa wakati (hii ni muhimu sana).

3. Epuka kupiga Soga wakati wa kazi na utani sijui wa Yanga na simba, mitindo ya nguo/nywele nk hii hupelekea uzembe wa kuchelewesha huduma.

Kumbuka mteja/huduma unayotoa ndio imekuweka kazini. Simu/Meseji/ndugu/marafiki wanaweza kusubiri.

4. Wewe ni msomi hivyo angalia taratibu gani zipo vizuri kwenye Idara uliyopangiwa uzifuate na zile mbaya epuka; mbaya ni kama kuchelewa kazini, wizi, kutoroka, kupiga soga wakati wa kazi, majungu nk.

5. Epuka visingizio vya mara kwa mara (watu wengi wanachangamoto zao ila hawazileti makazini); hii inaweza kukupa reputation mbaya kwa muda mfupi na kupelekea kuachishwa pale kunapokuwa na haja...

Narudia tena, Degree itakusaidia kupata kazi ila haikusaidii kusalia kazini na kumbuka wapo wasomi wengi pengine kuliko wewe wapo nje wanasubiria hiyo nafasi!

Mkifeli na kufukuzwa msije anza kulia lia kuwa mmeonewa huku nimeshawapa marking scheme ya mtihani; Kazi kwenu!
 
Mkipata kazi kwanza mjue mlichojifunza Chuoni ni kama 60% hivyo mnahitaji kujifunza kwa haraka majukumu mtakayo pangiwa bila dharau kwa mtakao wakuta. Degree inakusaidia kupata kazi ila haikusaidii kuendelea kubakia kazini.

Kitakachokufanya usalie kazini na kuendelea kula mema ya nchi ni kama utafanya yafuatayo;

1. Kufanya kazi kwa bidii na kukamilisha majukumu yako kwa USAHIHI na kwa wakati.

2. Kuwasiliana/Communication kama kuna kitu umeshindwa/huelewi ili uelekezwe ili usiharibu au kushindwa kumaliza kwa wakati (hii ni muhimu sana).

3. Epuka kupiga Soga wakati wa kazi na utani sijui wa Yanga na simba, mitindo ya nguo/nywele nk hii hupelekea uzembe wa kuchelewesha huduma.

Kumbuka mteja/huduma unayotoa ndio imekuweka kazini. Simu/Meseji/ndugu/marafiki wanaweza kusubiri.

4. Wewe ni msomi hivyo angalia taratibu gani zipo vizuri kwenye Idara uliyopangiwa uzifuate na zile mbaya epuka; mbaya ni kama kuchelewa kazini, wizi, kutoroka, kupiga soga wakati wa kazi, majungu nk.

5. Epuka visingizio vya mara kwa mara (watu wengi wanachangamoto zao ila hawazileti makazini); hii inaweza kukupa reputation mbaya kwa muda mfupi na kupelekea kuachishwa pale kunapokuwa na haja...

Narudia tena, Degree itakusaidia kupata kazi ila haikusaidii kusalia kazini na kumbuka wapo wasomi wengi pengine kuliko wewe wapo nje wanasubiria hiyo nafasi!

Mkifeli na kufukuzwa msije anza kulialia huku nimeshawapa marking scheme ya mtihani kwa watakao ajiriwa, Kazi kwenu!
Uishi Maisha marefu mkuu 💪
 
Kwahiyo huyo jamaa alieajiriwa ofisini kwenu mwenye degree anakunyima usingizi Sana?
nawasadia tu madogo kwani wanapigwa chini (huku private) kwa poor performance bila kujua wanakosea wapi.
Wengi hufikiri wapo kule kuuza sura kumbe kule ni kupiga kazi (result oriented) na sio blaa blaa siku ipite....
Mimi ni mshauri tu na nimerescure kadhaa karibu watimuliwe nikaona niweke huku na wengine waone
Huko kwingine ukiwa na ka degree upo salama hata kama unapiga blaa blaa lakini sio private...huku ni result oriented; kama hakuna matokeo mlango upo wazi....
 
Mnawaza kufanya kazi za watu tu kwaakili hizi kutoboa sahau😀😀😀😀😀😀. Tunategemea uandike jumbe za jinsi ya kupata mtaji, unakuja kuwafundisha vijana jinsi ya kumheshimu boss ili wasifukuzwe kazi 😀😀😀😀
 
Mkuu umeuza mechi...ubarikiwe sana. Wenye kusikia wasikie
 
Mnawaza kufanya kazi za watu tu kwaakili hizi kutoboa sahau😀😀😀😀😀😀. Tunategemea uandike jumbe za jinsi ya kupata mtaji, unakuja kuwafunfisha vijana jinsi ya kumheshimu boss ili wasifukuzwe kazi 😀😀😀😀
post moja haiwezi ku cover kila kitu lakini pia ni ukweli usiofichika kuwa; kwa Nchi hasa masikini; ajira kwenye Mashirika/viwanda huwapatia vijana wengi mitaji ya uhakika. Kwa Nchi zetu hizi usipokuwa makini utaunda group la wasomi wachuuzi na sio wafanya biashara/ wazalishaji ambao wanaweza kulipa Kodi.
Subiri post zingine.
"By the way sijafundisha kupigia Boss magoti ; NILICHOFUNDISHA NI KUTHAMINI KAZI INAYOKUPA KIPATO;
kitu ambacho hakipo kwa sasa ndio sababu maeneo mengi huduma ni mbovu!!!
 
Back
Top Bottom