Ushauri Kwa Viongozi Wakuu Wa Serikali – Awamu Ya Nne, Hususani Mhe Meghji, Karamagi,

Ushauri Kwa Viongozi Wakuu Wa Serikali – Awamu Ya Nne, Hususani Mhe Meghji, Karamagi,

Mzee S.H.Kasori,

Asante sana kwa ujumbe wako mzito.
Sisi kama vijana wa Taifa hili tunapenda sana kuendelea kupata mawazo ya busara kama haya kutoka kwa wazee wetu.
Naomba niungane na wewe hasa kwenye masuala ya maadili kwa viongozi wetu,kukemea ufisadi na elimu nchini mwetu.
Ni kweli kabisa kuwa hali ya shule,vyuo vyetu vikuu,na sekondari zetu ni mbaya mno.Busara inahitajika ili kuweza kubadilisha hali hii na kuwakomboa watanzania ambao wengi wanategemea sana vyuo hivyo na shule hizo ili kuweza kupata ujuzi na maarifa ya kupambana na kukabiliana na maisha yao ya kila siku.
Serikali yetu imetutupa sana kwa hili,tunasikia tu nyimbo za ujenzi wa shule kwa nguvu za wananchi wakati serikali yenyewe inatenga fungu dogo kwenye sekta ya elimu kwa kweli huu ni usaliti.
Tunachoona ni mashangingi ya kila aina yakinunuliwa na wakuu wetu wa kiserikali huku hali yetu ya kimaisha hailingani kabisa na gharama hizo. Kuna wakati huwa najiuliza kuwa hawa viongozi wana vichwa vyenye akili au vina maji ndani yake? Mbona busara zao ni ndogo namna hiyo?
Basi mzee wetu tunatumaini kuwa viongozi wetu watayaona haya machache uliyoyasema na pengine huruma itawaingia mioyoni mwao ili waweze kuwasaidia watanzania .

-Wembe
 
Mzee Mkombozi22
Ama nimefiarijika sana ila kwa kustushwa kusoma ushauri wako kuntu ktk thread uliyoianzisha. Ninamini kuwa unafuatilia vyema masaibu yanayotukuta sisi vijana wa Taifa hili.
Najua wengi watasoma au kupelekewa na wapambe wao huu ujumbe wako ila amin amin nakuambia kuwa bado watafanya shingo ngumu.

Mie nakushukuru kwa kunielimisha na nimejikomboa kifikra kwa post yako hii, Nawaasa wana JF msiwe kama RA, EL, NK na EM kwa kusoma juu juu, tafakurini hoja anazojenga mzee wetu ambaye naweza kumwita SHUJAA.
 
Saluti Mzee Kasori; Kwa Miaka Uliyosema Kuwa Ulianza Kuajiriwa Na Serikali,ina Maana Ni Moja Kwa Moja Ulikuwa Unafanya Kazi Na Akina Mramba Ktk Ile Serikali Ya Nyerere,mzee Samahani Nakuuliza Tu Swali Moja, Je? Huyu Mramba Tamaa Aliitoa Wapi,na Ni Nini Kinamsababishia Tamaa Maana Kwa Hesabu Za Haraka Tu Ni Kwamba Tangu Alipoanza Kuajiriwa Na Mpaka Mwishoni Mwa Serikali Ya Mkapa Pesa Tu Ya Mshahara Ingemtosha Kabisa Kamalizia Kipindi Chake Cha Kuishi Hapa Duniani Ukizingatia Umri Alionao Sasa Tena Kwa Raha Sasa Hizi Pesa Za Kukwapua Anataka Kupeleka Wapi Na Umri Huu?
 
Samahani Mzee Kasori, Nina Swali Lingine.nakumbuka Huyu Mkapa Alivyopendwa Na Nyerere Mpaka Nyerere Akadiriki Kumwita Mr Clean, Na Pia Nakumbuka Jinsi Nyerere Picha Zilivyokuwa Haziendi Na Hawa Kaburu, Sasa Baada Ya Nyerere Kufariki Huu Ushkaji Wa Mkapa Na Hao Makaburu Ulitokana Na Nini Mpaka Akakubali Kuwafukia Wale Raia Wakiwa Hai Ktk Yale Machimbo Kule Shinyanga Na Kuwatwanga Kwa Risasi Ndugu Zetu Kule Arusha Mererani?
 
Mimi Nawaombea Kwa Mungu Nyie Mnaojifanya Eti Hiyo Keki Taifa Ni Mali Yenu Nyie Mafisadi Na Kuwaacha Wananchi Wakitaabika Na Mwenyezi Mungu Awapige Kwa Ukimwi
 
I have come across many writers and publishers, but this guy is amazing. He is articulate, intelligent and smart. I am young, and i use to under estimate CCM members.This guy prove me wrong.

Hii ni chachu kwa wanachama wengine wa CCM walio amua kuburuzwa kama mzigo wa chumvi. Mtu mwenye upeo ni yule asiyekubali kuburuzwa.

I wish ndg ungekuja mara kwa mara kuchambua uozo wa serikali ya Jakaya Mrisho Kikwete. Uozo unaonuka sio Tanzania tuu, bali hata ng'ambo.
 
Naomba iunganishwe na huyo ndugu yake mwingine.. hii ni mojawapo ya makala safi kabisa ambazo hazina udaku..
 
Back
Top Bottom