Ushauri kwa wahitimu wa kidato cha 4 (O-Level)

Ushauri kwa wahitimu wa kidato cha 4 (O-Level)

Forgotten

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2018
Posts
3,518
Reaction score
10,839
Huu ni ushauri kwa mliomaliza kidato cha 4 (O-Level) mwaka huu na mnafikiria kujiunga na chuo japokuwa mna ufaulu mzuri wa kujiunga A-Level. Kama ni mzazi una mtoto aliyemaliza masomo hayo na ana wazo hili unaweza kumpatia ushauri huu. Natoa ushauri huu from experience na niliyoyaona baada ya mimi kupita njia hiyohiyo.

Kumekuwa na wimbi kubwa la wahitimu wengi wa kidato cha 4 kukwepa masomo ya A-Level wakiona kama ni kupoteza muda kwasababu tu ukipita chuo unapata ujuzi kwa fani unayoitaka, unaokoa muda (which isn't true), kupata ajira za diploma, kukimbia masomo ya A-Level yanayoaminika kuwa ni magumu.

Ila ni lazima wanafunzi wajue umuhimu wa masomo ya A-Level. Kwenye ngazi za kielimu A-Level inakupa hadhi ya "High School Graduate" ambayo kuipata kwenye nchi nyingi ni 12 years in school, sasa ukiishia form 4 unahesabika kama mtu ambaye hajahitimu High School. Pia, A-Level hutoa ujuzi muhimu na maarifa ambayo huunda msingi wa elimu zaidi na stadi za maisha. Wanafunzi hupata msingi mzuri kwa masomo kama: hesabu, sayansi na sanaa ya lugha.

Kimataifa elimu zinazotolewa Tanzania na kutambulika ni High School (A-Level), Bachelor's Degree, Master's Degree. Kutokana na Utandawazi na mapinduzi ya Teknolojia ni vyema kuendana na kasi ya Dunia kwa kuwa na International Credentials, hii itakupa wigo mpana kwenye soko la ajira na hata elimu pia.

Sasa tukirudi kwenye my experience, mwaka jana nilitaka kwenda kujiendeleza kielimu nje ya nchi, Central Europe. Shida ikaja kwenye vyeti nilivyonavyo kwakuwa sikuhitimu High School (12 years) nikawa sikidhi vigezo vya kujiunga na masomo hayo, japokuwa tayari nilikuwa nimefanya post-secondary studies. Ikatakiwa nifanye Foundation Program, ambayo inaongeza gharama za kifedha na muda wa mwaka mmoja.

So ushauri wangu ni vyema upite A-Level then, Bachelor's Degree. Ukihitimu unakuwa na ngazi mbili za kielimu zinazotambulika kimataifa. Hapahapa nchini kuna waajiri wanataka watu waliohitimu High School.

Ushauri wangu kwa serikali, katika maboresho ya sera za elimu 2027 baada ya kufuta darasa la 7 na kufanya uhitimu wa elimu yetu kuwa miaka 12 badala ya 13. Waangalie namna ya kufanya O-Level na A-Level kuwa mandatory na kidato cha 4 kuwe na mtihani wa taifa kama ilivyo sasa ila kusiwe na cheti na baada ya kuhitimu A-Level ndiyo mwanafunzi apate High School Certificate.
 
Huu ni ushauri kwa mliomaliza kidato cha 4 (O-Level) mwaka huu na mnafikiria kujiunga na chuo japokuwa mna ufaulu mzuri wa kujiunga A-Level. Kama ni mzazi una mtoto aliyemaliza masomo hayo na ana wazo hili unaweza kumpatia ushauri huu. Natoa ushauri huu from experience na niliyoyaona baada ya mimi kupita njia hiyohiyo.

Kumekuwa na wimbi kubwa la wahitimu wengi wa kidato cha 4 kukwepa masomo ya A-Level wakiona kama ni kupoteza muda kwasababu tu ukipita chuo unapata ujuzi kwa fani unayoitaka, unaokoa muda (which isn't true), kupata ajira za diploma, kukimbia masomo ya A-Level yanayoaminika kuwa ni magumu.

Ila ni lazima wanafunzi wajue umuhimu wa masomo ya A-Level. Kwenye ngazi za kielimu A-Level inakupa hadhi ya "High School Graduate" ambayo kuipata kwenye nchi nyingi ni 12 years in school, sasa ukiishia form 4 unahesabika kama mtu ambaye hajahitimu High School. Pia, A-Level hutoa ujuzi muhimu na maarifa ambayo huunda msingi wa elimu zaidi na stadi za maisha. Wanafunzi hupata msingi mzuri kwa masomo kama: hesabu, sayansi na sanaa ya lugha.

Kimataifa elimu zinazotolewa Tanzania na kutambulika ni High School (A-Level), Bachelor's Degree, Master's Degree. Kutokana na Utandawazi na mapinduzi ya Teknolojia ni vyema kuendana na kasi ya Dunia kwa kuwa na International Credentials, hii itakupa wigo mpana kwenye soko la ajira na hata elimu pia.

Sasa tukirudi kwenye my experience, mwaka jana nilitaka kwenda kujiendeleza kielimu nje ya nchi, Central Europe. Shida ikaja kwenye vyeti nilivyonavyo kwakuwa sikuhitimu High School (12 years) nikawa sikidhi vigezo vya kujiunga na masomo hayo, japokuwa tayari nilikuwa nimefanya post-secondary studies. Ikatakiwa nifanye Foundation Program, ambayo inaongeza gharama za kifedha na muda wa mwaka mmoja.

So ushauri wangu ni vyema upite A-Level then, Bachelor's Degree. Ukihitimu unakuwa na ngazi mbili za kielimu zinazotambulika kimataifa. Hapahapa nchini kuna waajiri wanataka watu waliohitimu High School.

Ushauri wangu kwa serikali, katika maboresho ya sera za elimu 2027 baada ya kufuta darasa la 7 na kufanya uhitimu wa elimu yetu kuwa miaka 12 badala ya 13. Waangalie namna ya kufanya O-Level na A-Level kuwa mandatory na kidato cha 4 kuwe na mtihani wa taifa kama ilivyo sasa ila kusiwe na cheti na baada ya kuhitimu A-Level ndiyo mwanafunzi apate High School Certificate.
Asante Kwa kushare.

Kuna baadhi ya taasisi uhitaji elimu ya high school ili kupata ajira nauliza swali hill ili kupata ufahamu mzuri.
 
Hiki kitu huwa kinanishangaza sana unakuta mtoto ana sifa zote za kuingia kidato cha Tano ila mzazi sijui anatoa wapi ushauri anaacha kumpeleka mtoto.

Halafu badae anaanza kulia.
Advance Level ni nzuri sana.
 
Asante Kwa kushare.

Kuna baadhi ya taasisi uhitaji elimu ya high school ili kupata ajira nauliza swali hill ili kupata ufahamu mzuri.
Ajira nyingi vigezo ni Diploma au degree labda kwenye majeshi ndo huwa wanaweka vigezo vya O & A level mbali na hapo binafsi sijawahi kuona kigezo cha ajira kikawa hizo level za elimu
 
Mimi nipo degree 3 year ila Naona Bora ningepitaga certificate na Diploma.

Naona serikali inatoa priority sana kwa watu waliosoma diploma na sio degree

Nasoma Bachelor degree in Gender and Development.

Naona Bora ningesoma dimploma kuliko advance level
 
Kwamba akipita Diploma hawezi kufikia hiyo Masters ambayo ndo kiwango cha elimu kinachotambuliwa mujibu wa maelezo yako?
Anaweza, ila mtaala wetu wa elimu unakuwa umemfelisha mhitimu huyu maana kimataifa atahesabika hakuhitimu masomo ya upili. Ndiyo maana ni vyema serikali ikapitia sera za elimu upya, mfano Kenya wana mtaala mzuri unaozalisha wahitimu wengi kwa ngazi ya High School.
 
Hiki kitu huwa kinanishangaza sana unakuta mtoto ana sifa zote za kuingia kidato cha Tano ila mzazi sijui anatoa wapi ushauri anaacha kumpeleka mtoto.

Halafu badae anaanza kulia.
Advance Level ni nzuri sana.
Yupi ulimuona ambae mtoto wake hakupita Advance na baadae akaanza kulia? Na sababu ya kulia ilikua ni nini ? Fafanua
 
Ni kweli Katika Kazi za mabeberu huwa wanatambua Elimu ya A level Kama high school hata pia ukiomba vyuo .

Mtoa mada yupo sahihi
Je kwa mtu ambae hajapita High school akasoma Diploma akaenda hadi akamaliza degree akitaka kusoma Masters kwenye nchi ya mabeberu atanyimwa fursa kwasababu hakupita high-school?
 
Kwahiyo unataka kutueleza kuwa level ya Diploma haitambuliki kimataifa?
Kuna nchi kadhaa za Africa najua zinatambua ngazi hii ya elimu ila kwa mabara ya Ulaya na Marekani ya Kaskazini naamini ni 99% ngazi hii haitambuliki. Kuna nchi wanatambua ni post-secondary education ila inakuwa tofauti na kwenye mitaala yao.
 
Kuna nchi kadhaa za Africa najua zinatambua ngazi hii ya elimu ila kwa mabara ya Ulaya na Marekani ya Kaskazini naamini ni 99% ngazi hii haitambuliki. Kuna nchi wanatambua ni post-secondary education ila inakuwa tofauti na kwenye mitaala yao.
Aah sawa je mitaala inayotumika Advance hapa kwetu ni sawa na mitaala inayotumika kwao?
 
Huu ni ushauri kwa mliomaliza kidato cha 4 (O-Level) mwaka huu na mnafikiria kujiunga na chuo japokuwa mna ufaulu mzuri wa kujiunga A-Level. Kama ni mzazi una mtoto aliyemaliza masomo hayo na ana wazo hili unaweza kumpatia ushauri huu. Natoa ushauri huu from experience na niliyoyaona baada ya mimi kupita njia hiyohiyo.

Kumekuwa na wimbi kubwa la wahitimu wengi wa kidato cha 4 kukwepa masomo ya A-Level wakiona kama ni kupoteza muda kwasababu tu ukipita chuo unapata ujuzi kwa fani unayoitaka, unaokoa muda (which isn't true), kupata ajira za diploma, kukimbia masomo ya A-Level yanayoaminika kuwa ni magumu.

Ila ni lazima wanafunzi wajue umuhimu wa masomo ya A-Level. Kwenye ngazi za kielimu A-Level inakupa hadhi ya "High School Graduate" ambayo kuipata kwenye nchi nyingi ni 12 years in school, sasa ukiishia form 4 unahesabika kama mtu ambaye hajahitimu High School. Pia, A-Level hutoa ujuzi muhimu na maarifa ambayo huunda msingi wa elimu zaidi na stadi za maisha. Wanafunzi hupata msingi mzuri kwa masomo kama: hesabu, sayansi na sanaa ya lugha.

Kimataifa elimu zinazotolewa Tanzania na kutambulika ni High School (A-Level), Bachelor's Degree, Master's Degree. Kutokana na Utandawazi na mapinduzi ya Teknolojia ni vyema kuendana na kasi ya Dunia kwa kuwa na International Credentials, hii itakupa wigo mpana kwenye soko la ajira na hata elimu pia.

Sasa tukirudi kwenye my experience, mwaka jana nilitaka kwenda kujiendeleza kielimu nje ya nchi, Central Europe. Shida ikaja kwenye vyeti nilivyonavyo kwakuwa sikuhitimu High School (12 years) nikawa sikidhi vigezo vya kujiunga na masomo hayo, japokuwa tayari nilikuwa nimefanya post-secondary studies. Ikatakiwa nifanye Foundation Program, ambayo inaongeza gharama za kifedha na muda wa mwaka mmoja.

So ushauri wangu ni vyema upite A-Level then, Bachelor's Degree. Ukihitimu unakuwa na ngazi mbili za kielimu zinazotambulika kimataifa. Hapahapa nchini kuna waajiri wanataka watu waliohitimu High School.

Ushauri wangu kwa serikali, katika maboresho ya sera za elimu 2027 baada ya kufuta darasa la 7 na kufanya uhitimu wa elimu yetu kuwa miaka 12 badala ya 13. Waangalie namna ya kufanya O-Level na A-Level kuwa mandatory na kidato cha 4 kuwe na mtihani wa taifa kama ilivyo sasa ila kusiwe na cheti na baada ya kuhitimu A-Level ndiyo mwanafunzi apate High School Certificate.
Ukimaliza A-level unakuwa umehitimu fani ipi?

Maana aliyehitimu diploma/certificate tayari ana fani aliyosomea. Kiufupi amesomea kazi tofauti na A-level unaenda kusoma ulichosoma O-level kikawa advanced kidogo.

Somea fani acha kusomea madesa ambayo hakuna mtu aliyehitimu A-level akawa na fani fulani ya kazi aliyosomea.

Hata ajira, mhitimu wa form four na form six wanaajiriwa kama watu wasio na profession yoyote ila certificate/diploma ni mtu aliyesomea kazi fulani na anaajiriwa kama professional wa eneo husika.
 
Hiki kitu huwa kinanishangaza sana unakuta mtoto ana sifa zote za kuingia kidato cha Tano ila mzazi sijui anatoa wapi ushauri anaacha kumpeleka mtoto.

Halafu badae anaanza kulia.
Advance Level ni nzuri sana.
wanaambiana diploma anaajirika fasta! Mzazi anakuwa katua Mzigo
 
Back
Top Bottom