Ushauri kwa wahitimu wa kidato cha 4 (O-Level)

Ushauri kwa wahitimu wa kidato cha 4 (O-Level)

Toa maelezo kuhusu hii
Foundation Program ni mwaka wa maandalizi kwa masomo ya Bachelor's Degree kwa International Students ambao hawakidhi vigezo. Vyuo vyao vinataka uwe umehitimu High School ambayo ni miaka 12, ukiwa na cheti cha O-Level ni miaka 11 hivyo unakuwa hujakidhi vigezo.
 
Huu ni ushauri kwa mliomaliza kidato cha 4 (O-Level) mwaka huu na mnafikiria kujiunga na chuo japokuwa mna ufaulu mzuri wa kujiunga A-Level. Kama ni mzazi una mtoto aliyemaliza masomo hayo na ana wazo hili unaweza kumpatia ushauri huu. Natoa ushauri huu from experience na niliyoyaona baada ya mimi kupita njia hiyohiyo.

Kumekuwa na wimbi kubwa la wahitimu wengi wa kidato cha 4 kukwepa masomo ya A-Level wakiona kama ni kupoteza muda kwasababu tu ukipita chuo unapata ujuzi kwa fani unayoitaka, unaokoa muda (which isn't true), kupata ajira za diploma, kukimbia masomo ya A-Level yanayoaminika kuwa ni magumu.

Ila ni lazima wanafunzi wajue umuhimu wa masomo ya A-Level. Kwenye ngazi za kielimu A-Level inakupa hadhi ya "High School Graduate" ambayo kuipata kwenye nchi nyingi ni 12 years in school, sasa ukiishia form 4 unahesabika kama mtu ambaye hajahitimu High School. Pia, A-Level hutoa ujuzi muhimu na maarifa ambayo huunda msingi wa elimu zaidi na stadi za maisha. Wanafunzi hupata msingi mzuri kwa masomo kama: hesabu, sayansi na sanaa ya lugha.

Kimataifa elimu zinazotolewa Tanzania na kutambulika ni High School (A-Level), Bachelor's Degree, Master's Degree. Kutokana na Utandawazi na mapinduzi ya Teknolojia ni vyema kuendana na kasi ya Dunia kwa kuwa na International Credentials, hii itakupa wigo mpana kwenye soko la ajira na hata elimu pia.

Sasa tukirudi kwenye my experience, mwaka jana nilitaka kwenda kujiendeleza kielimu nje ya nchi, Central Europe. Shida ikaja kwenye vyeti nilivyonavyo kwakuwa sikuhitimu High School (12 years) nikawa sikidhi vigezo vya kujiunga na masomo hayo, japokuwa tayari nilikuwa nimefanya post-secondary studies. Ikatakiwa nifanye Foundation Program, ambayo inaongeza gharama za kifedha na muda wa mwaka mmoja.

So ushauri wangu ni vyema upite A-Level then, Bachelor's Degree. Ukihitimu unakuwa na ngazi mbili za kielimu zinazotambulika kimataifa. Hapahapa nchini kuna waajiri wanataka watu waliohitimu High School.

Ushauri wangu kwa serikali, katika maboresho ya sera za elimu 2027 baada ya kufuta darasa la 7 na kufanya uhitimu wa elimu yetu kuwa miaka 12 badala ya 13. Waangalie namna ya kufanya O-Level na A-Level kuwa mandatory na kidato cha 4 kuwe na mtihani wa taifa kama ilivyo sasa ila kusiwe na cheti na baada ya kuhitimu A-Level ndiyo mwanafunzi apate High School Certificate.
Mfumo wa nchi nyingi za Ulaya hazina A-level bali mwanafunzi akihitimu form four anaenda university moja kwa moja.

Anzia na mfumo wa elimu wa Netherlands nakadhalika uone kama wana ujinga wa A-level halafu linganisha na mfumo wetu wa elimu wa kukaririshwa madesa kuanzia Primary, O'level hadi A'level.

Yaani hakuna mwanafunzi anachojua nje ya alichokaririshwa darasani.

Mwanangu akimaliza form four hata awe na division one ya pointi 7 ataenda chuo na sio kupoteza muda A'level kama wengi tulivyopoteza.

Tunakutana na mabumunda yaliyohitimu A'level mtaani unamuuliza swali la mtego kidogo tu ya kile ambacho walifundishwa shuleni haelewi chochote.

Nimesoma chuo na watu waliopitia certificate kisha diploma halafu wale wa fresh from school (A'level) wanakimbizwa vibaya sana kazi za group za wanasaidiwa na watu wa diploma.

Hata matokeo ya mwisho watu wa diploma wanaongoza kwa mbali kwasababu wana uzoefu na msingi wa profession tangu certificate.
 
Foundation Program ni mwaka wa maandalizi kwa masomo ya Bachelor's Degree kwa International Students ambao hawakidhi vigezo. Vyuo vyao vinataka uwe umehitimu High School ambayo ni miaka 12, ukiwa na cheti cha O-Level ni miaka 11 hivyo unakuwa hujakidhi vigezo.
OUT itamuhusu au sio?
 
Wazazi wanataka shortcut kwenye maisha. Na wengi hawana exposure kabisa. Mimi naona ni ukatili kwa mtoto kumwekea limits kwenye maisha yake. Mtoto mwenye elimu ya A - Level ana nafasi kubwa ya kupata fursa nyingi kimataifa.
 
Aah sawa je mitaala inayotumika Advance hapa kwetu ni sawa na mitaala inayotumika kwao?
Mfumo wetu wa elimu utakaoanza kutumika 2027 unaweza kufanana na England. Unapozungumzia mtaala (curriculum) kwa shule zetu za Serikali ni tofauti kabisa na International Schools zilizopo hapahapa nchini. Kinachofaya A-Level itambulike kimataifa ni miaka inayohitajika mwanafunzi kuhitimu, hapa kwetu mwanafunzi anakaa shule miaka 13 kuhitimu High School ambayo ni zaidi ya ile inayotambulika kimataifa (12).
 
Mfumo wa nchi nyingi za Ulaya hazina A-level bali mwanafunzi akihitimu form four anaenda university moja kwa moja.

Anzia na mfumo wa elimu wa Netherlands nakadhalika uone kama wana ujinga wa A-level halafu linganisha na mfumo wetu wa elimu wa kukaririshwa madesa kuanzia Primary, O'level hadi A'level.

Yaani hakuna mwanafunzi anachojua nje ya alichokaririshwa darasani.

Mwanangu akimaliza form four hata awe na division one ya pointi 7 ataenda chuo na sio kupoteza muda A'level kama wengi tulivyopoteza.

Tunakutana na mabumunda yaliyohitimu A'level mtaani unamuuliza swali la mtego kidogo tu ya kile ambacho walifundishwa shuleni haelewi chochote.

Nimesoma chuo na watu waliopitia certificate kisha diploma halafu wale wa fresh from school (A'level) wanakimbizwa vibaya sana kazi za group za wanasaidiwa na watu wa diploma.

Hata matokeo ya mwisho watu wa diploma wanaongoza kwa mbali kwasababu wana uzoefu na msingi wa profession tangu certificate.
Una akili za kimaskini sana.
 
Mfumo wetu wa elimu utakaoanza kutumika 2027 unaweza kufanana na England. Unapozungumzia mtaala (curriculum) kwa shule zetu za Serikali ni tofauti kabisa na International Schools zilizopo hapahapa nchini. Kinachofaya A-Level itambulike kimataifa ni miaka inayohitajika mwanafunzi kuhitimu, hapa kwetu mwanafunzi anakaa shule miaka 13 kuhitimu High School ambayo ni zaidi ya ile inayotambulika kimataifa (12).
Wamepunguza sasa kuna la 6 ndio mwisho ila bado inasoma 13 mwanzo ilikua 14
 
Mfumo wa nchi nyingi za Ulaya hazina A-level bali mwanafunzi akihitimu form four anaenda university moja kwa moja.

Anzia na mfumo wa elimu wa Netherlands nakadhalika uone kama wana ujinga wa A-level halafu linganisha na mfumo wetu wa elimu wa kukaririshwa madesa kuanzia Primary, O'level hadi A'level.

Yaani hakuna mwanafunzi anachojua nje ya alichokaririshwa darasani.

Mwanangu akimaliza form four hata awe na division one ya pointi 7 ataenda chuo na sio kupoteza muda A'level kama wengi tulivyopoteza.

Tunakutana na mabumunda yaliyohitimu A'level mtaani unamuuliza swali la mtego kidogo tu ya kile ambacho walifundishwa shuleni haelewi chochote.

Nimesoma chuo na watu waliopitia certificate kisha diploma halafu wale wa fresh from school (A'level) wanakimbizwa vibaya sana kazi za group za wanasaidiwa na watu wa diploma.

Hata matokeo ya mwisho watu wa diploma wanaongoza kwa mbali kwasababu wana uzoefu na msingi wa profession tangu certificate.
Ni lazima mfumo wa elimu ubadilishwe. Tuwaige hata majirani zetu Kenya, baada ya kufutwa darasa la 6 tutakuwa tunaenda sawa na sera za elimu za kimataifa ila tunapaswa kuwa na ngazi moja tu ya elimu ya upili inayotambulika ili kuachana na hizi O-Level & A-Level.
 
Wazazi wanataka shortcut kwenye maisha. Na wengi hawana exposure kabisa. Mimi naona ni ukatili kwa mtoto kumwekea limits kwenye maisha yake. Mtoto mwenye elimu ya A - Level ana nafasi kubwa ya kupata fursa nyingi kimataifa.
Kweli kabisa, serikali inapaswa kuangalia namna nzuri ya kufanya elimu ya upili iwe ile inayotambulika kimataifa ikiwa na maana elimu ya juu kabisa kwa secondary iwe inakamilisha miaka 12. Kenya mfumo wao ni 8-4-4 maana yake ukitoka shule ya msingi, unaenda shule ya upili na ukihitimu moja kwa moja umekamilisha miaka 12 ya High School ambayo inatambulika Kimataifa na unaweza kujinga vyuo vya kati au chuo kikuu.

Huu mfumo wa 7-4-2 unampa mwanafunzi option ya kuishia njani na kuruka ngazi muhimu ya A-Level kwenda chuo.
 
Narudia tena na tena hapa kuandika, vijana nendeni A-level ikiwa mna ndoto za kusoma zaidi, kutokupoteza muda na kuwa na wigo mpana wa kusomea mambo tofauti tofauti au kuwa na uwanja wa kimataifa.

Diploma wakasomee watu wenye hizi sifa tu;
1. Wanaosaka ujuzi wa kwenda kuajiriwa moja kwa moja baada ya kuhitimu hiyo diploma.
2. Waliokosa sifa stahiki za kuendelea mbele zaidi kimasomo kwa njia ya moja kwa moja.
 
Hiki kitu huwa kinanishangaza sana unakuta mtoto ana sifa zote za kuingia kidato cha Tano ila mzazi sijui anatoa wapi ushauri anaacha kumpeleka mtoto.

Halafu badae anaanza kulia.
Advance Level ni nzuri sana.
Na mimi najiuliza. Mtoto kachaguliwa form five, kwa nini asiende kusoma hiyo miaka miwili ili akimaliza asone Diploma mana wengine wanaona Diploma ni rahisi kuajiriwa kuliko Degree
 
Mimi nipo degree 3 year ila Naona Bora ningepitaga certificate na Diploma.

Naona serikali inatoa priority sana kwa watu waliosoma diploma na sio degree

Nasoma Bachelor degree in Gender and Development.

Naona Bora ningesoma dimploma kuliko advance level
Huo ndio ukweli. Mwanangu alitakiwa kujiunga na A level mm nikagoma nikampeleka diploma ya CO Iringa sasa hivi anaajira ya serikali na anajisomea mengine taratibu wakati anauhakika yupo kazini
 
Mfumo wa nchi nyingi za Ulaya hazina A-level bali mwanafunzi akihitimu form four anaenda university moja kwa moja.

Anzia na mfumo wa elimu wa Netherlands nakadhalika uone kama wana ujinga wa A-level halafu linganisha na mfumo wetu wa elimu wa kukaririshwa madesa kuanzia Primary, O'level hadi A'level.

Yaani hakuna mwanafunzi anachojua nje ya alichokaririshwa darasani.

Mwanangu akimaliza form four hata awe na division one ya pointi 7 ataenda chuo na sio kupoteza muda A'level kama wengi tulivyopoteza.

Tunakutana na mabumunda yaliyohitimu A'level mtaani unamuuliza swali la mtego kidogo tu ya kile ambacho walifundishwa shuleni haelewi chochote.

Nimesoma chuo na watu waliopitia certificate kisha diploma halafu wale wa fresh from school (A'level) wanakimbizwa vibaya sana kazi za group za wanasaidiwa na watu wa diploma.

Hata matokeo ya mwisho watu wa diploma wanaongoza kwa mbali kwasababu wana uzoefu na msingi wa profession tangu certificate.
Huo ndio ukweli
 
Kama hajasoma physics basi aende tu high school.
Vyuo vya Kati ni vizuri kwa upande wa afya na engineering tu zile kozi zingne ni Bora akatokea advance tu ili aje kupata mkopo.
Kitu kingine kinachopelekea watu kukimbia advance ni competition ya kupata vyuo Bora vyaa gvt kwa ajiri ya kozi nzri Kama medical doctor, n.k.
Nimeshuhudia watu wamesoma pcb na wakafaulu vzr kwa dv 1 of 8 pnt lkn walikosa hata nafasi ya nursing kwa vyuo vya gvt kwa sababu kule wanataka angalau pnt 6 kwenye masomo husika,
wamejikuta wanasoma food science, natural science na course zingne za afya ambazo hata mtu Alie soma CBG anaweza kuzisoma.
 
Shida yako unatoa maoni kwa kaungalia njia wewe,ambayo sio njia ya kila mtu wengine hawana haja ya kwenda nje na wengine kamwe hawataajiriwa
 
Mkuu kama sina haja ya kwenda huko ughaibuni kuna haja gani ya kwenda A-Level?Maana umejieleza sana lakini mwisho ukasema wewe umekwama kwenda eirope kwa sababu hukusoma A-level. Ushauri wako ni mzuri sana
 
Mkuu kama sina haja ya kwenda huko ughaibuni kuna haja gani ya kwenda A-Level?Maana umejieleza sana lakini mwisho ukasema wewe umekwama kwenda eirope kwa sababu hukusoma A-level. Ushauri wako ni mzuri sana
Ni ushauri tu, hata mimi nilipomaliza O-Level sikuona umuhimu wa A-Level nikaachana nayo.

Huu ni ushauri kwa wale waliomaliza kidato cha 4 na wapo njia panda kufanya maamuzi wachukue ngazi ipi kielimu.
 
Huu ni ushauri kwa mliomaliza kidato cha 4 (O-Level) mwaka huu na mnafikiria kujiunga na chuo japokuwa mna ufaulu mzuri wa kujiunga A-Level. Kama ni mzazi una mtoto aliyemaliza masomo hayo na ana wazo hili unaweza kumpatia ushauri huu. Natoa ushauri huu from experience na niliyoyaona baada ya mimi kupita njia hiyohiyo.

Kumekuwa na wimbi kubwa la wahitimu wengi wa kidato cha 4 kukwepa masomo ya A-Level wakiona kama ni kupoteza muda kwasababu tu ukipita chuo unapata ujuzi kwa fani unayoitaka, unaokoa muda (which isn't true), kupata ajira za diploma, kukimbia masomo ya A-Level yanayoaminika kuwa ni magumu.

Ila ni lazima wanafunzi wajue umuhimu wa masomo ya A-Level. Kwenye ngazi za kielimu A-Level inakupa hadhi ya "High School Graduate" ambayo kuipata kwenye nchi nyingi ni 12 years in school, sasa ukiishia form 4 unahesabika kama mtu ambaye hajahitimu High School. Pia, A-Level hutoa ujuzi muhimu na maarifa ambayo huunda msingi wa elimu zaidi na stadi za maisha. Wanafunzi hupata msingi mzuri kwa masomo kama: hesabu, sayansi na sanaa ya lugha.

Kimataifa elimu zinazotolewa Tanzania na kutambulika ni High School (A-Level), Bachelor's Degree, Master's Degree. Kutokana na Utandawazi na mapinduzi ya Teknolojia ni vyema kuendana na kasi ya Dunia kwa kuwa na International Credentials, hii itakupa wigo mpana kwenye soko la ajira na hata elimu pia.

Sasa tukirudi kwenye my experience, mwaka jana nilitaka kwenda kujiendeleza kielimu nje ya nchi, Central Europe. Shida ikaja kwenye vyeti nilivyonavyo kwakuwa sikuhitimu High School (12 years) nikawa sikidhi vigezo vya kujiunga na masomo hayo, japokuwa tayari nilikuwa nimefanya post-secondary studies. Ikatakiwa nifanye Foundation Program, ambayo inaongeza gharama za kifedha na muda wa mwaka mmoja.

So ushauri wangu ni vyema upite A-Level then, Bachelor's Degree. Ukihitimu unakuwa na ngazi mbili za kielimu zinazotambulika kimataifa. Hapahapa nchini kuna waajiri wanataka watu waliohitimu High School.

Ushauri wangu kwa serikali, katika maboresho ya sera za elimu 2027 baada ya kufuta darasa la 7 na kufanya uhitimu wa elimu yetu kuwa miaka 12 badala ya 13. Waangalie namna ya kufanya O-Level na A-Level kuwa mandatory na kidato cha 4 kuwe na mtihani wa taifa kama ilivyo sasa ila kusiwe na cheti na baada ya kuhitimu A-Level ndiyo mwanafunzi apate High School Certificate.
Unakitu utafika mbali mkuu
 
Back
Top Bottom