Yesu Anakuja
JF-Expert Member
- Apr 10, 2019
- 12,675
- 25,924
Ninajiita mtenda dhambi ila niliyesamehewa, kwasababu hakika ninafichwa na kafara la Damu ya Yesu Kristo tu mbele za Mungu, na hii ni baada ya kukabidhi maisha yangu kwake kwa maana ya kuokoka. Amekuwa Mungu wangu, mwokozi wangu, akiniangalia hanioni mimi, anaona kafara la Damu ya Yesu kwasababu nimekabidhi maisha kwake kwa njia ya Kumkiri Yesu, na hiyo Damu ndio Damu ya Agano Jipya iletayo ondoleo la dhambi.
Simaanishi kwamba kwasababu Neema ipo hivyo niwe natenda dhambi kwasababu nimeshakabidhi maisha kwake, Noo, najiona kila siku mimi ni mdhaifu nahitaji msaada wa Mungu, najitakasa kila siku na kuukimbia uovu kwa msaada wake, ili niishi maisha matakatifu. Biblia inasema
Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa.. (UFUNUO 22:11)
Maishani mwangu nilishawahi kuwa mtenda dhambi sana, nilimuudhi sana Mungu, tena nikiwa naijua kweli, nilikuwa kwenye kifungo cha uzinzi, ujeuri, kiburi na kila kitu, ilifika mahali nikawa naamini pengine kilichobaki kwangu ni adhabu tu, dhambi zangu ni nyingi mno, labda Mungu asingenisamehe. Lakini baada ya kusoma Neno lake, nilikuja kugundua kuwa, pamoja na kwamba huwa anaadhibu pia, Mungu ni mwenye huruma mno kwetu, siku zote anasubiri tugeuke, tutubu ili atusamehe, ni mwenye hasira lakini hashiki hasira zake milele, huwa anaghairi kutufanyia mabaya, naye hurufahia rehema. Yaani pale anapoturehemu huwa anafurahia.
La kufahamu ni kwamba, ukitenda dhambi usiitubie, lazima itakutafuna tu, it is just a matter of time, na hata isipokutafuta katika ulimwengu huu, itakusababisha uende moto wa milele. Ila ukijijua una dhambi, ukatubu kwa kumaanisha kuziacha, Mungu huzifuta na kuzitupa kwenye kilindi cha bahari, hatazikumbuka tena, hata kama wewe utazikumbuka yeye Mungu ameamua kuzisahau kwasababu anazifuta kabisa kabisa na unabaki bila dhambi.. mimi dhambi zangu mtu akinikumbusha huwa nawaambia, MUNGU ALISHANISAMEHE, ALISHAZIFUTA, MIMI SINA DHAMBI, KAMA UNAZIKUMBUKA KAJADILIANE NA MUNGU HUKO, USIJADILIANE NA MIMI. Na huu ndio ukweli.
ISAYA 43:25 Mimi, naam, mimi, ndimi niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka dhambi zako.
Yoe.2:12-13 "Lakini sasa, asema BWANA, nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote, na kwa kufunga, na kwa kulia, na kwa kuomboleza, RARUENI MIOYO YENU, WALA SI MAVAZI YENU; Kwa maana yeye ndiye mwenye neema, amejaa huruma; si mwepesi wa hasira ni mwingi wa rehema; naye hughairi mabaya"
MIKA 7: 18 – 19. Ni nani aliye Mungu kama wewe, mwenye kusamehe uovu, na kuliachilia kosa la watu wa urithi wake waliosalia? Hashiki hasira yake milele, kwa maana yeye hufurahia rehema. Atarejea na kutuhurumia; atayakanyaga maovu yetu, nawe utazitupa dhambi zao zote katika vilindi vya bahari.
Zaburi 103:11-13"Maana mbingu zilivyoinuka juu ya nchi, Kadiri ile ile rehema zake ni kuu kwa wamchao. Kama mashariki ilivyo mbali na magharibi, Ndivyo alivyoweka dhambi zetu mbali nasi.
Kama vile baba awahurumiavyo watoto wake, Ndivyo Bwana anavyowahurumia wamchao."
USHAURI WANGU KWENU: siku zote mshahara wa dhambi ni mauti, ila ukitubu Mungu anakupa uzima wa milele. Hivyo asiwepo mtu wa kuwavunja moyo, kwamba labda mmekuwa watenda dhambi sana hamtasamehewa, No. Mungu atawasamehe. Haijalishi umetenda dhambi gani, labda ukiondoa ile ya kumkufuru Roho Mtakatifu. Tubu,rudi kwa Mungu, atakusamehe, atasahau dhambi zako, utakuwa kiumbe kipya. Kwa lugha nyingine, Mungu hana kisirani, hakasiriki milele, huwa anasamehe ukijirudi.
Simaanishi kwamba kwasababu Neema ipo hivyo niwe natenda dhambi kwasababu nimeshakabidhi maisha kwake, Noo, najiona kila siku mimi ni mdhaifu nahitaji msaada wa Mungu, najitakasa kila siku na kuukimbia uovu kwa msaada wake, ili niishi maisha matakatifu. Biblia inasema
Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa.. (UFUNUO 22:11)
Maishani mwangu nilishawahi kuwa mtenda dhambi sana, nilimuudhi sana Mungu, tena nikiwa naijua kweli, nilikuwa kwenye kifungo cha uzinzi, ujeuri, kiburi na kila kitu, ilifika mahali nikawa naamini pengine kilichobaki kwangu ni adhabu tu, dhambi zangu ni nyingi mno, labda Mungu asingenisamehe. Lakini baada ya kusoma Neno lake, nilikuja kugundua kuwa, pamoja na kwamba huwa anaadhibu pia, Mungu ni mwenye huruma mno kwetu, siku zote anasubiri tugeuke, tutubu ili atusamehe, ni mwenye hasira lakini hashiki hasira zake milele, huwa anaghairi kutufanyia mabaya, naye hurufahia rehema. Yaani pale anapoturehemu huwa anafurahia.
La kufahamu ni kwamba, ukitenda dhambi usiitubie, lazima itakutafuna tu, it is just a matter of time, na hata isipokutafuta katika ulimwengu huu, itakusababisha uende moto wa milele. Ila ukijijua una dhambi, ukatubu kwa kumaanisha kuziacha, Mungu huzifuta na kuzitupa kwenye kilindi cha bahari, hatazikumbuka tena, hata kama wewe utazikumbuka yeye Mungu ameamua kuzisahau kwasababu anazifuta kabisa kabisa na unabaki bila dhambi.. mimi dhambi zangu mtu akinikumbusha huwa nawaambia, MUNGU ALISHANISAMEHE, ALISHAZIFUTA, MIMI SINA DHAMBI, KAMA UNAZIKUMBUKA KAJADILIANE NA MUNGU HUKO, USIJADILIANE NA MIMI. Na huu ndio ukweli.
ISAYA 43:25 Mimi, naam, mimi, ndimi niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka dhambi zako.
Yoe.2:12-13 "Lakini sasa, asema BWANA, nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote, na kwa kufunga, na kwa kulia, na kwa kuomboleza, RARUENI MIOYO YENU, WALA SI MAVAZI YENU; Kwa maana yeye ndiye mwenye neema, amejaa huruma; si mwepesi wa hasira ni mwingi wa rehema; naye hughairi mabaya"
MIKA 7: 18 – 19. Ni nani aliye Mungu kama wewe, mwenye kusamehe uovu, na kuliachilia kosa la watu wa urithi wake waliosalia? Hashiki hasira yake milele, kwa maana yeye hufurahia rehema. Atarejea na kutuhurumia; atayakanyaga maovu yetu, nawe utazitupa dhambi zao zote katika vilindi vya bahari.
Zaburi 103:11-13"Maana mbingu zilivyoinuka juu ya nchi, Kadiri ile ile rehema zake ni kuu kwa wamchao. Kama mashariki ilivyo mbali na magharibi, Ndivyo alivyoweka dhambi zetu mbali nasi.
Kama vile baba awahurumiavyo watoto wake, Ndivyo Bwana anavyowahurumia wamchao."
USHAURI WANGU KWENU: siku zote mshahara wa dhambi ni mauti, ila ukitubu Mungu anakupa uzima wa milele. Hivyo asiwepo mtu wa kuwavunja moyo, kwamba labda mmekuwa watenda dhambi sana hamtasamehewa, No. Mungu atawasamehe. Haijalishi umetenda dhambi gani, labda ukiondoa ile ya kumkufuru Roho Mtakatifu. Tubu,rudi kwa Mungu, atakusamehe, atasahau dhambi zako, utakuwa kiumbe kipya. Kwa lugha nyingine, Mungu hana kisirani, hakasiriki milele, huwa anasamehe ukijirudi.