majibu tafadhari ya findings zako bro...Hiki kitu nimekifuatilia sana, na kipindi chote nilichokuwa kimya humu nilikuwa nafuatilia hili suala kwenye mifumo yake ikiwemo kuangalia waliotutangulia jinsi wanavyojiendesha,
tuna anza sasa au tuna anza lini au tuna anza anzaje... kwa style gani mkuu... tutume number PM utuunge mkuu au utaratibu ni upi hapo mkuu...Nami naunga mkono hoja. Kama watu watakuwa wapo free basi mchakato wa kumteua mtu ili atoe muongozo wa nini cha kufanya ikiwemo mapendezo basi ufanyike
Ndugu wana JF
Kwa muda mrefu kumekuwa na masuala mbalimbali yahusuyo kujilipua (kwenda nje ya nchi) ambayo watu wanauliza mmoja mmoja kwa lemgo la kutaka msaada na ushauri namna ya kufika na jinsi ya kuanza maisha huko nje.
Kutokana na kutoa msaada kwa wengi (binafsi) kwa kutumia njia binafsi nimeona nifungue uzi huu ili kuweka mambo yote wazi kwa kadiri itakavyowezekana na kualika wengine pia waweze kutoka maoni yao.
Ndugu zangu nchi yetu ya Tanzania ki uwezo bado ni changa, fursa za kutoka ni chache na hata changamoto ni nyingi. Huko kwa wenzetu fursa ni nyingi ndio maana imekuwa chanzo cha kuvuta wahamiaji wengi sana toka mataifa masikini.
Nchi masikini wenzetu huko mbele raia wao wamejaa haswa kutokana na moyo wa kusaidiana na kuvutana.
Nimeamua nilete hoja hii kama ambavyo wenzetu hufanya huko Nairaland ya Nigeria ili kila mtu mwenye ujuzi au ufahamu juu ya namna ya kutoka (kujilipua) atoe msaada kwa wengine kwenda huko... si lazima wewe binafsi usaidie mtu binafsi NO, hata mbinu tu za jinsi ya kufika huko.
Kabla sijaingia kwenye kiini cha mada naomba nitoe faida na changamoto za kujilipua.
FAIDA
1. Fursa nzuri za kiuchumi na kujiinua hasa ukiwa na malengo.. Wakuu binafsi nimeishi Marekani kwa miaka nane. moja ya faida nilizopata huko ni kujiinua kiuchumi.... binafsi wakati naenda kusoma huko nilijiwekea malengo ya kujenga ghorofa nyumbani, kufungua mashine za kusaga na kukoboa nafaka pamoja na kumiliki fuso za mizigo...
kipato cha mfanyakazi wa kule ni kikubwa mno kushinda hata cha baadhi ya maboss wetu hapa... hivyo nilijitahidi nilipokuwa kule malengo yangu yaimie... ni kweli baada ya muda huo nilifanikiwa kutimiza yote.
2. Huduma nzuri za afya, Elimu, Sheria, miundombinu.
CHANGAMOTO
1. changamoto kubwa kwa kuwa kule ni upweke (ku feel home mara kwa mara japo wakati mwingine ukizoea hutoweka)
2. Xenophobia hii ni kwa baadhi ya nchi tu sio zote.
USHAURI WA WAPI UENDE NA NAMNA GANI UENDE
Kwa wale wahitaji wa masuala ya maisha kujijenga na kuchuma nashauri nchi hizi, USA, UK, NORDIC COUNTRIES, NA WESTERN EUROPE COUNTRIES. kwa Afrika nashauri SA.
Jinsi gani utaenda namna ni nyingi.... naorodhesha baadhi hapo chini...
1. kwenda kimasomo ambapo unaweza tafuta sponsors then ukapata scolarship itayokuwezesha kupata visa na kujilipua huko baada ya masomo...
2. Kutafuta mwenzi wa nje ambaye atakualika huko kisha mtaoana na kukuwezesha kupata resident permit na baadae uraia.
3. Kuhamisha mataji na biashara njia hii unakubaliwa popote alimradi uwe na biashara halali,
4. kwenda kwa shughuli za utamaduni
Wenzetu wakenya na wanigeria wameunda mfumo wa kualikana wao kwa wao, kwamba mtu anakutumia barua ya mwaliko, then unakwenda ukifika huko anakutafutia mtu mnaoana kisheria tu ili upate karatasi kisha kila mtu anasika hamsini zake....
Wapendwa mambo ni mengi siwezi andika yote ndio maana nimeanziasha uzi huu tutaendelea kujuzana kwa kairi michango ya watu itakavyokuwa na maswali yatayojitokeza.
Nawakaribisha nyote. Na wote wenye maujuazi au mauzoefu ya huko mbele... karibuni tusaidiane tujenge taifa letu... Tuwasaidie vijana wakasake fursa.
Kabisa mkuu, kwa asilimia kubwa mwangaza umetolewa humu mtu akiutumia atafanikiwa... mfano kuna wengi wanatamni kwenda south na mkuu segito wa kalenga ametoa mwaliko na anaishi huko watu wajiongeze.... mfano south ukiwa na passport ni kukata ticket tuuu mengine unaongea na mwenyeji basi... tusiwe waoga wote waliokwenda huko wengine hawakuwa na ndugu achilia mbali rafiki.Mkuu Zogoo dk naunga mkono hoja.Lusungo katoa shamba,Izzo katoa utaalamu Na sisi wakulima tufanyie kazi hili shamba (kujilipua nje) watu wengi wamechangia Na bado wanachangia.Ukianza toka mwanzo wa huu uzi
1) tovuti za nchi zinazotoa mafunzo ya Kusoma nje bure www.topuniversities.com
2) Kwa wale wanaotaka kwenda SA dadayetu
Katoa mualiko
3) Wataalamu wa migodi kuajiriwa nje habari zake ziko humu.
4) Watu wanao taka kuhost tovuti(website) ziko
5) wanao taka kwenda Japan habari ziko
6) tovuti za nchi ambazo pasipoti ya Tanzania unaingia bila ya visa Au unapata visa ukifika hiyo nchi
7) tovuti ya kupata (green card lottery)
www.us-departmentofstate.gov.dvlottery
Na habari nyingi zingine sizikumbuki
Tuzifanyie kazi.
Tafadhali msife moyo Watu wengi watatoka
Kweli kabisa mkuu, nina ndugu yangu kazamia ujerumani huu Kama mwaka wa 20 na kapata urai kabisa, huku nyumbani kasimamisha mijengo kadhaa.Haha kweli mkuu... Si unaona hapa mtu anamkarisha tamaa mwenzie ooh Huku hivi na vile hapohapo yeye bado yupo huko....
Ni kweli usemayo si rahisi mbongo akukaribishe kwake huko Ulaya hapo atakukwepa sana....
Haha ndo wabongo tulivyo... huwezi mshauri mtu eti ulimwengu wa tatu kuzuri kuliko ulimwengu w kwanza!! ni wivu na roho mbaya tu zimetujaa.Kweli kabisa mkuu, nina ndugu yangu kazamia ujerumani huu Kama mwaka wa 20 na kapata urai kabisa, huku nyumbani kasimamisha mijengo kadhaa.
Kila Mara tunachati sana na kujuliana hali, kuna siku nikamchomekea vipi nataka na Mimi nizamie huko, hii kazi yangu nayofanya Pesa haitoshi yote inaishia mdomoni tu na maisha yanaendelea kubana. Akasema naomba nikushauri bora ubaki Tanzania usije ukajaribu kuwaza kuja huku, manyanyaso, ubaguzi, kazi hakuna...... Dah!! Nikajiuliza huyu kukaa zaidi ya miaka 20 kama yangekuwepo matatizo hayo siangekuwa karudi? Watanzania watu wa ajabu sana
Hahaaaaaaa umenichekesha sanaKweli kabisa mkuu, nina ndugu yangu kazamia ujerumani huu Kama mwaka wa 20 na kapata urai kabisa, huku nyumbani kasimamisha mijengo kadhaa.
Kila Mara tunachati sana na kujuliana hali, kuna siku nikamchomekea vipi nataka na Mimi nizamie huko, hii kazi yangu nayofanya Pesa haitoshi yote inaishia mdomoni tu na maisha yanaendelea kubana. Akasema naomba nikushauri bora ubaki Tanzania usije ukajaribu kuwaza kuja huku, manyanyaso, ubaguzi, kazi hakuna...... Dah!! Nikajiuliza huyu kukaa zaidi ya miaka 20 kama yangekuwepo matatizo hayo siangekuwa karudi? Watanzania watu wa ajabu sana
Naunga mkono hoja. Ila msinione mchoyo tuanze ambao tumekuwa active kwenye uzi toka mwanzoni
Nami naunga mkono hoja. Kama watu watakuwa wapo free basi mchakato wa kumteua mtu ili atoe muongozo wa nini cha kufanya ikiwemo mapendezo basi ufanyike
Mkuu lomayani asante kwa ushauri.Kwa kweli hakuna kama nyumbani!Nimeishi na nimetembelea nchi zote ambazo umezitaja hapo juu.Lakini inasikitisha dharau,ubaguzi na kodi unazotozwa ukiwa ndani ya nchi hizo.Unapoondoka au kuoa mwanamke wa kwao hapo dnipo dharau na ubaguzi unapooneshwa live.Mwanamk mweupe hawzi ishi nawewe maisha yake yote,ataangalia zaidi nini unacho.Wengi wanataka wapate mtoto au watoto "breeding bull",halafu hapo biashara yako imetoka.Hupti kazi ya kipato kikubwa,na usalama wako dhidi ya chemicals na polisi uko mashakani.Huwezi ongea chochote mbele yao,labda tu pale unapokandia serikali yako,au watu weusi wenzio.Kuna baadhi ya sehemu ambazo hili halionekani sana,kama vile Washington DC.
wazo zuri mkuu, thumb upNaimani daby, lusungo,stunter, kaveli, shyshii, dr. Adam, segito wa kalenga, mgogoone n. k tulianza mwanzo vizuri tukielekezana mbinu na changamoto za kujilipua. Wenye husda walikuja na kusababisha movement kuwa na mwendo mdogo. Tuna kila sababu ya kumshukuru izzo na lusungo kwa walivyokuwa wameamua kujitoa. Hili la kuwa na whatsapp group ni lizuri sasa tungekubaliana nani alianzishe na vipi viwe vigezo vya mtu kuungwa. Kwa kuanza napendekeza waanzilishi wa kundi wawe daby, lusungo, stunter
Mkuu Daby mimi nadhani wala usiumize kichwa chako kusubiri jibu hapo, cha msingi nikufanya maamuzi tuu. kwani mpka sasa njia tumeonyeshwa hapa ni sisi kushikamana kwa namna yoyote ile ili tuwaonyeshe ndugu zetu walioonyesha nia ya kutusaidia sisi wenye nia ya kwenda n'gambo kuwa tumeamua kwa nia moja hata kuchangiana ili kuwatoa wenye mapungufu ya nauli na mambo mengine ili kuonyesha nia na dhamira yetu kuwa ni njema na si vinginevyo binafsi niko tayari hata kuchangia michango ya kuwatoa waliotayari kuondoka ili wakasome ramani huko mbele.
Sent from my SM-J110H using JamiiForums mobile app