Ni muhimu kutumia bati zenye ubora katika uezekaji wa nyumba.
Mara nyingi bati za geji kubwa ni nzuri kutumika katika paa zenye slope ndogo ili panapotokea ukarabati juu ya paa zisibondeke pondeke.
Bati za geji kubwa (G28) hudumu kwa muda mrefu kwa maana ya kuimili hali zote za mvua na jua na si rahisi kupata kutu kwa muda mfupi.
Bati za geji ndogo (G30,G32) ni nzuri kwa majengo ya kawaida ya muda au uzio kwenye majenzi makubwa, na hutumika sana kwenye nyumba zenye slope kali zisizohitaji kupanda juu ya paa.
Na ni muhimu kuyapaka rangi ya kuzuia kutu /kununua yenye kuwa na rangi ya kuzuia kutu.
Ili bati lidumu ni lazima kench/trusses na purlins(mbao zenye kushika Bati) zake ziwe imara haijalishi ni geji ipi unatumia.
Kench na purlins ni vitu muhimu sana vya kuzingatia katika uezekaji wa paa.
Unapotumia bati za geji ndogo ni lazima kenchi na purlins ziwe nyingi ili kuimalisha paa na kuweka muonekano mzuri wa kutokubonyea bonyea.
Kuhusu gharama ni kuwa :-
Gharama za kutumia G28 ni sawa sawa na G30 kwa kuwa malighafi za kuezeka G30 ni nyingi kuliko G28 zenye malighafi ndogo lakini bati zake ni ghali.
Kuhusu kampuni ipi ni nzuri, hapa sina jibu sahihi kwa kuwa specifications za mabati zinajulikana kitaifa na kimataifa,tofauti ni namna ya kufanya marketing na customer care kwa wateja.
Muhimu :
Ili paa liwe na muonekano mzuri ni lazima kuwatumia wataalamu wa majenzi ikiwezekana kila urefu wa bati husika ujulikane na kiwanda kikate urefu husika kuliko kuunga uunga vipande vya either (2.5-3.0m).
Lakini pia ni vizuri uezekaji wa paa uzingatie volume ya maji ili kudesign slope nzuri isiyowezesha maji kutuama na kusababisha kutu.
Hata hivyo ni vema kuanza kufikiria uezekaji wa zege kwa baadhi ya majengo, ambapo finishing yake juu ya paa ifanywe kwa kutumia malighafi zisizo pitisha maji (epox coating n. k......)
Asante kwa ufafauzi. Naomba nitoe mchango wangu kutokana na nilichojifunza kwa muda mfupi kwenye hii industry ya roofing.
Kwanza nisema watu wengi kila siku wanajenga au kufanya biashara hizi lakini kuna mahali wanafeli ku grasp taarifa sahihi za kitaalam.
Nitazungumzia viwanda nilivyotembelea Alaf, Sunshare, Bati Bomba na kingine pale Tabata..
Gauge za mabati hutofautiana kulingana na unene au thickness ya bati, G30 inakadiriwa kuwa na thickness ya 0.25mm na G28 ni 0.35mm. This is techinical diferences. Na pia kuna chemical diferences lakini karibu zote zinafanana maana zimeundwa na Aluminium na Zinc ktk ratio tofauti tofauti. Zinc na Aluminium ndio properties zinazozui bati kuota kutu kama ikiform zinc oxide au Aluminium Oxide.
Matumizi ya Gauge ktk nyumba.
Kama mleta mada alivyouliza nini tofauti ya matumizi ya bati G28 dhidi ya G30.
1. Hutegemea na mahitaji ya mjengaji, mfano serikali inayojenga majengo makubwa kama kiwanda, godauni, shule au hospitali hutumia bati zenye thickness kubwa kutokana na umuhimu wa jengo lenyewe tofauti na mtu binafsi anayejenga nyumba ya vyumba vitatu.
2. Uimara wa nyumba, msingi na teknolojia ya ujenzi. Hapa tunaona kuwa nyumba kubwa inahitaji mabati mengi zaidi. Lakini pia kama nyumba imejengwa na Fundi Maico yatarajiwa viwango vyake vya uimara( strength) ya msingi na ukuta vitakuwa si mujarabu hivyo kuezeka nyumba hii kwa G28 inaweza kupeleka uzito mkubwa unaoweza kuhatarisha maisha ya nyumba yako. Vile vile kama hali ya hewa ya udongo, maji kutwama, mmomonyoko n.k vyaweza kupelekea nyumba kutitia.
Hii ni muhimu kwa sababu Bando la bati 16 , G28 lina karibu uzito wa kilo 92 wakati bando la bati 16 G30 lina uzito wa takribani kilo 50. Kwahiyo nyumba kubwa kama shule, godauni, kanisa au hospitali utajenga kwa bando ngapi na huo msingi na ardhi vitahimili hizo tani za uzito wa paa??
3. Teknolojia ya uezekaji. Hii inaenda sambamba na ukubwa wa jengo. Nyumba zetu hizi kenchi hadi kenchi ni mita moja tu au chini ya hapo. Shule na kanisa au msikiti vipimo ni vikubwa zaidi so yafaa G28.
Kuhusu Bei za Mabati kutofautiana.
Katika uchunguzi wangu nilifikia hitimisho kuwa hakuna tofauti kubwa ktk bei na utofauti wa bei haumanishi yenye bei kubwa ni imara na bora zaidi. Fuatana nami:
Wauzaji wengi watakueleza kuhusu Gauge ya bati, rangi, na urefu na bei kamwe hawakwambii upana wa bati.
Mfano. Kiwanda cha tabata bati la G30. Migongo mipana( msauzi) urefu futi 10 linauzwa elfu 30. Bati hilo hilo Kiwanda cha Bati Bomba wanauza elfu 28,500. Lakini ni hivi upana kwa Tabata ni 750mm wakati BatiBomba ni 90mm. Vivyo hivyo Sunshare bati zao upana ni 870mm na wanauza elfu 34,500 kwa bati hilo hilo la urefu futi 10, G30 na rangi ile ile.
Kwa G28 Batibomba wanauza futi 10 migongo mipana kwa 34500 wakati ALAF wanauza takriban 55,500. Unaweza kudhani Alaf wanauza bei kubwa sana lakini ALAF bati zao upana ni 1220mm wakati Batibomba ni 900mm. Hapa utaona kuna tofauti kubwa sana. Uki converge hizi factors kwa pamoja utakuta wote bei karibu sawa.
Mfano huo huo unaenda kwa Sunshare na Tabata.
So utahitaji kununua mabati machache ALAF a utahitaji mabati mengi Sunshare.
Jambo lingine linaloweza kuchangia utofauti wa Bei( usihusishwe na ubora au uimara) ni miundo mbinu ya uzalishaji mali pamoja na rasilimali watu.
Mfano. ALAF wana majengo mazuri ya kisasa ya kibiashara full kiyoyozi na ukifika pale kama uko nyumbani au ofisi ya CAG Kichere. Wakati ukifika Tabata na Batibomba joto na vumbi mwendo mdundo wanazalisha kwenye magodown hapo hapo ndio wateja wanachukulia mizigo yao. Hawa watu hawawezi kuchaji bei sawa. Lazima bei za pango na mandhari mazuri uyalipie. Hivyo hivyo kwa Makampuni mengine.
Ushindani wa kibiashara: makampuni mengine nje ya ALAF ni mapya na mageni. Hivyo wanaunafuu kidogo kutokana na mahitaji ya kujitangaza na kujitanua. ALAF tayari ni mkongwe wajenzi wa viwanda na serikali inachukua mizigo mikubwa kwake. Hana shida na hizo milioni zako 2,3, 4, 5...
Kuhusu Malighafi
Wote wananunua kwa supplier wanaofanana. Aidha South afrika au China na india. Na wote mali zao huingizwa zikiwa tayari zimeshachanganywa materials na Rangi. Kazi yao hapa Dar ni kukata na kukunja muundo unaotaka IT4, IT5, Versatile, Romantile....etc.
NB: mimi sio Injinia wa ujenzi wala sina any formal profession kwenye industry hii. Hii ni kutokana na elimu ya hapa na pale niliyodanya mimi mwenyewe kwa kuona, kuuliza, kushika na kusikia viwandani.
Penye makosa/ mapungufu wataalam karubuni kurekebisha.