Ushauri mpya kuhusu uvaaji wa Barakoa (Masks) kujikinga na maambukizi ya Covid-19: Tujielimishe ili tuamue vema

Hahahahaha

Wote waliokuwa wanapiga vita niqaab na hijab za Kiislam, sasa watafunika nyuso zao wakipenda wasipende.

Allahu Akbar.
Kwa hio Iran walikuwa hawavai!? Mbona maambukizi yapo juu
 
.

Jr[emoji769]
 
Sasa wewe mleta mada unajichanganya, kwa nini madaktari na manesi ambao hawana Corona wavae Mask kujikinga kuambukizwa na wenye Korona halafu wakati huo utoke hapo useme eti wanasayansi wamedai kuwa hakuna msaada mkubwa wa mask kwenye kuzuia maambukizi?

Kama barakoa ni nzuri kwa madaktari na manesi basi ni nzuri pia kwa raia wa kawaida maana huko kwenye madaladala tunayopanda hatujui ni nani kasthirika. Je akipiga chafya au akakohoa si utaambukizwa kama hujavaa mask?
 

fundi25 Hiki ulichosema kuhus uuvaaji wa barakoo China umetoa wapi ndugu yangu. Nilichoongea sio fikra zangu wala habari za kupika. It is a documented fact. Unaweza kujipa muda kidogo tu ukaingia youtube kutafuta matukio ya China, Hong Kong na kwingine kabla ya Covid-19 kisha upime ukweli.
 

Umenena vema. Niliandika kwenye uzi mwingine kujadili nafasi ya watafiti/wasomi wetu kwenye janga hili. Umegusia moja ya mambo niliyoajdili: Mapambano dhidi ya Covid-19 Tanzania na kwingineko Afrika: Watafiti na wanasayansi wetu mko wapi na munasemaje? - JamiiForums
 

Uko sahihi kabisa ndugu Dystonia7 ila kama wewe ni mwanasayansi nadhani unaelewa kwamba ili ushauri utolewa kuhusu effectiveness of any practice, kunahitajika scientific evidence na sio matumizi ya "akili ya kawaida isiyohitaji kwenda medical school".

Ni kweli masks ni kinga ya magonjwa yanayoweza kuambukizwa kwa hewa au droplets. Ila kila ugonjwa una infectious characteristics zake ambazo zinaweza zisikabiliwe kirahisi kama magonjwa mengine yanayaofanana nao. Ukisoma nilichoandika, nimeuliza swali kwamba kama masks ni kinga yenye tija kama watu wengi wanavyotaka kuaminisha wengine, kwa nini South Korea, Hong Kong, Czech, China, nk wana maambukizi hadi leo wakati wanavaa muda wote nakuchukua tahadhari nyingine nyingi?

Nadhani ushauri mzuri nimeutoa namba 2. Kwa yeyeote anajisikia salama kuvaa barako kama kinga afanye hivyo ila umakini unahitajika watu wasidhani kuna uhakika wa kinga. Bado tunacheza na bahati naasibu.

MM Togolani

MM Togolani
 
Nijibu swali lako ndugu lukonge :
Nilichorekebisha ndicho sahihi. Nadhani hujasoma vizuri nilichoandika kwenye uzi wangu. Kuna maelezo ya kutosha juu ya ushauri wa kitaalamu na unaotolewa na WHO ya nani anahitajika kutumia barakoa kama kinga na kwa nini. Nimekuwekea na link.

Uko sawa kuhusu ushauri wa kuzivaa. Ila kwa sasa ushauri sahihi ni kuzitazama kama tiba ya kisaikolojia kuliko msisitizo wa kinga maana hakuna uthibitisho.

Wataalamu wanaoshauri mass masking (uvaaji wa watu wengi/wote) hawashauri kutumia medical masks. Maana ni gharama isiyo lazima. Hata ushauri wa CDC wameshauri watu kuvaa non-medical masks. Wanashauri improvisation kutumia hata vitambaa vya kawaida. Nimeona wengine wamependekeza hijabu hapa.

 
Hayo ya Hongkong angalia iyo video utajuwa kwa nini walivaa barakoa!
Nimezunguka china Sana kwenye viwanda na mashamba suala la kuvaa barakoa kwenye masuala ya safety kwa china sio kipaumbele sana!! Kama ilivyo kwa nchi za magharibi!
 

Ndugu Missile of the Nation nahofia sijajichanganya ila ni wewe hujasoma kwa utulivu. Ila ngoja nijichanganue. Ukisoma vizuri nimeleza ushauri wa kitaalamu unasema ni watu gani wanashauriwa kuvaa na kwa nini (waathirika na wanaohudumia waathirika). Nimekuwekea na link kabisa.

Vinginevyo nilichotoa ni uchambuzi wa hoja zote mbili: kuvaa na kutokuvaa kama kinga kwa mtu ambaye hajaathirika. There is a lot of publications on this subject ningezirejea hapa uzi ungekua mrefu. Ila conclusion ni moja hadi sasa: kwamba hakuna ushahidi wa kisayansi kwamba mass masking (uvaaji wa kila mtu hata ambaye hajaathirika) una tija katika kuzuia maambukizi.

MM Togolani
 

Nashukuru kwa sumaary hii. Ila tunapozungumzia uvaaji wa masks lazima tujue ni variable moja kati ya nyingi sana za equation ya Covid-19. Bado kuna unknown nyingi juu ya kazi ya maambukizi ya ugonjwa huu. Ndio mana uvaaji masks umekua ni mjadala na mvutano mkubwa miongoni mwa wanasayansi iwapo kweli zina msaada kukabiliana na maambukizi ya huyu shetani wa familia ya Corona
 
Watu wavae tu barakoa kama alivyoshauri Paskari sababu huwezi jua Nani kaambukizwa so kuavoid more spreading ya ugonjwa huo barakoa is unenevitable

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sisi Waafrica ni kama bendera tu, kokote upepo utapovuma ndio tunapoelekea,
Naamini kabisa likitokea jopo la madaktari wazungu wakatuthibitishia kua bange ni kinga dhidi ya Corona, Nina uhakika Mashehe na Mapdri wetu huku lazima nao watasokota tu.
Tena nmekumbuka hivi Jamaica [emoji1135] maambukizi yamefika huko?
 

Kama mask inamkinga daktari basi inaweza kumkinga raia pia.

Ni commonsense tu huhitaji publication kwenye scientific journal kuliona hilo.

Kama mimi ni asymptomatic lakini nina virusi vya Korona bila kujijua tukakutana na wewe kwenye daladala tukakaa karibu karibu kisha nikapiga chafya, kama umevaa mask utanusurika, kama hujavaa mask utaupata

Ni logic simple tu, wala huhitaji research kujua kuwa leo ni jumamosi, it is just a fact!

Reason kubwa kwa nini Asia imeweza kucontain hii kitu haraka na damage kuwa minimal ni kwa sababu ya combination ya measures huku Kuvaa mask kwa kila mtu kukiplay major role
 

Hawa WHO nao ni complicit kwenye kuiletea dunia hii janga, hawaminiki kwa sasa.
Hawa walitoa ushauri mbovu kuwa huu ugonjwa siyo human to human transmissible, kwa ushauri wao huu potofu wamemislead nchi na watu wengi sana, no wonder tupo hapa tulipofikia.

Sasa ukisema tuwafate hawa WHO kuhusu kupinga mask ni misleading nyingine kutoka kwa hawa jamaa
 
Ndugu yangu Missile of the Nation, hakuna mtu anachagua baba bila kujali ni mlevi, kasoma au ni mjinga lazima umsikilize kwenye majukumu yake ya kibaba. Nafasi ya WHO ni kubwa sana kwenye afya ya jamii hasa katika nchi zetu na huwezi kuipuuza. Hata hivyo simaanishi kila wanalosema ni sahihi 100% maana hata wao wako wanaowaburuza

Ila kwa hili la masks, huu sio ushauri "from the blue" bali umetokana na systematic review from scientific studies.

Kwenye kupotosha kuhusu Covid-19 (sijauona), hivi wa kuwalaumu ni wao au ni wachina amboa walikua hawasemi ukweli wa kinachoendelea? China ndio waliingiza dunia chaka na wakakata hata wataalamu wa nchi nyingine wasiende kusaidia kujua tatizo. Hadi leo wanaumiwa pia kwa kupotosha kuhusu idadi kamili ya wagonjwa na vifo.
 

MM Togilani,
Nadhani wakati unafanya masahihisho haukufuatilia vizuri paragraph alitoichukua Pascal. Nenda fanya reference ta marekebisho yako uone kama yanaendana na hali halisi.

Kama unasema practice ya N95 ni effective je hiyo ni gharama sana unalinganisha na nini? Kusubiru maambukizi utibie wagonjwa na wengine wafe au u-sabsidize tool na watu wapate kwa gharama ya chini au bure ili kuilinda jamii/protection?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…