Mimi naomba nitoe ushauri ambao ninaamini utaondoa utata wa matumizi ya kura ya siri au ya wazi kwenye bunge la katiba, kwani naona hili swala linaleta mvutano mkubwa kwa wajumbe wa bunge. Kwanza nitaangalia kwa kifupi mitizamo hii miwili halafu nitashauri njia muafaka ya kufuata :
Kura ya wazi
Kura hii ina faida ya kuweka record na kuwawezesha wananchi kujua exactly kila mjumbe alivyoshiriki katika kufikia maamuzi kuhusiana na katiba, na hii taarifa inaweza ikawa muhimu huko mbeleni, ikiwa ni pamoja na kutusaidia katika michakato ya kuchagua viongozi wetu katika nafasi mbali mbali za uongozi ndani ya nchi yetu. Nchi zilizoendelea na hasa Marekani wamekuwa wakitumia njia hii kwenye mabunge yao.
Kwa mfano, maamzuzi (ya kura) ya masenata wa Marekani katika mambo mbali mbali yanayohusu nchi yao, huwa sio siri. Mfano wakati Bush anataka kwenda kuivamia Iraq, Mama Clinton alipiga kura kukubaliana na Bush na Obama alipiga kura na hapana. Obama aliutumia uamuzi huo kama sehemu muhimu ya campaign hasa ukizingatia mwaka 2008 wamerekani walikuwa wamechoshwa sana na vita vya Iraq.
Vile vile mwaka 2007, rais wa Marekani, George W. Bush aliamua kuongeza idadi ya majeshi ya marekani kwa kiwango fulani nchini Iraq (Iraq war troop surge) ili wajaribu kuleta amani iraq halafu baadaye ndio waondoke. Hii ilipingwa na
Obama pamoja na waziri wa sasa wa ulinzi (Chuck Hagel) ambaye anatoka chama kimoja na Bush. Huu uamuzi wa troop surge ulikuja kuonekana baadaye kwamba ulikuwa uamuzi sahihi kwani ulikuwa na mafaniko makubwa. Wakati huyu
waziri wa ulinzi anahojiwa na masenata wenzake kabla hajawa confirmed kuwa waziri wa Obama katika kipindi chake cha pili, (kura yake) maamuzi ya Hagel kuhusiana na surge yalikuwa kati ya vitu ambavyo vilikuwa mwiba kwake, katika kuthibitishwa kwake kuwa waziri wa ulinzi. Kwa watu waliofuatilia ile hearing watakuwa wanakumbuka jinsi Mccain alivyombana huyu Bwana.
Pamoja na faida zinazoweka kupatikana kutokana na kura ya wazi, nadhani kwa nchi zetu hizi inabidi tufikiri kidogo kabla ya kuamua kufanya kama wanavyofanya wenzetu. Ninaamini wengi tutakuwa tunakubaliana kwamba nchi zetu nyingi za kiafrika, ubabe na ulipizaji wa kisasi kutoka kwa watawala wetu bado ni kitu ambacho bado kimeshamiri, hivyo ukisema watu wapige kura za wazi, wanaweza wakafanya maamuzi kinyume na utashi wao especially kama maamuzi yao wanaona yanakwenda kinyume na maamuzi ya viongozi wao. Matokeo yake hatutapata maamuzi sahihi ya wajumbe na nadhani hii itaondoa dhana nzima ya maamuzi sahihi, kwani maamuzi yatakuwa ni ya watu wachache tu ambao wengine watakuwa wametumika kama rubber stamp tu...
Kura ya siri
Kura ya siri ina uzuri kwamba mtu anakuwa na uhakika kwamba maamuzi yake ni siri yake mwenyewe. Hii itampa mtu confidence ya kuamua kile anachokiamini ni sahihi kwani ana uhakika kwamba maamuzi yake hayatatumika na yeyote kumfanyia hujuma huko mbeleni. Pamoja na kwamba kwa kutumia njia hii, records za wajumbe pamoja na maamuzi yao hazitakuwepo, lakini tutakuwa na uhakika wa maamuzi sahihi ambayo ndio yenye umuhimu zaidi ya hizo records. Mimi ninaamini hii njia ni nzuri kwa jamii kama yetu, ambapo mambo ya intimidation na matisho kutoka kwa watawala bado yapo kwa wingi.
Nini kifanyike ?
Kuna mjumbe mmoja wakati anachangia kwenye bunge la katiba jana alisema amepata simu kutoka kwa wananchi wake wakisema wanataka wabunge wafanye maamuzi kwa uwazi ili wafahamu wabunge wao wamefanya maamuzi gani. Hiyo ni sawa na lazima kutakuwa na wengine wengi tu wenye mawazo kama hayo. Vile vile ninaamini kuna wananchi wengine (kama mimi) ambao wanataka maamuzi yawe ya kura ya siri. Katika hili, watu mbali mbali wanaweza wakawa na misimamo tofauti.
Namna sahihi ya kuamua nini kifanyike ni kujua wengi wanataka kitu gani na hicho watakachoamua wengi ndicho kifanyike. Kama wengi wanataka kura ya siri, itakuwa wazi wengi wanaamini kwamba kura za namna hiyo ndio zitatota maamuzi sahihi na hivyo itabidi zipigwe kura za siri. Na kama wengi wanataka kura za wazi basi itabidi zipigwe kura za wazi. Sasa hakuna namna tunaweza tukapiga kura wote na kujua tunataka nini, ila tuna wabunge wa katiba ambao baadhi yao ni wawakilishi wa wananchi wa kuchaguliwa na wengine ni wa kuteuliwa (ambao nao originally walitoka kwenye makundi ya wananchi). Hawa wanaweza kupiga kura kwa niaba yetu, na watakaloamua ndilo tutakuwa wote tunalitaka na ndilo lifanyike.
Ninachoshauri ni kwamba KURA HII ya kuamua whether maamuzi ya Bunge la Katiba yawe kwa kura za wazi au za siri, yafanyike kwa KURA YA SIRI. Kama wataamua kura ziwe za wazi sawa, kama wataamua ziwe za siri sawa, ila kura hii ya kati ya haya maamuzi mawili iwe ya SIRI. Nadhani kwa wale wanaotaka kura za wazi hoja yao kubwa ni kwamba wananchi wajue wabunge wao walifanya maamuzi gani kuhusu katiba, na hii kura ninayoizungumzia hapa haihusu katiba bali inahusu tu maamuzi ya kanuni ya upigaji kura.
Kura ya wazi
Kura hii ina faida ya kuweka record na kuwawezesha wananchi kujua exactly kila mjumbe alivyoshiriki katika kufikia maamuzi kuhusiana na katiba, na hii taarifa inaweza ikawa muhimu huko mbeleni, ikiwa ni pamoja na kutusaidia katika michakato ya kuchagua viongozi wetu katika nafasi mbali mbali za uongozi ndani ya nchi yetu. Nchi zilizoendelea na hasa Marekani wamekuwa wakitumia njia hii kwenye mabunge yao.
Kwa mfano, maamzuzi (ya kura) ya masenata wa Marekani katika mambo mbali mbali yanayohusu nchi yao, huwa sio siri. Mfano wakati Bush anataka kwenda kuivamia Iraq, Mama Clinton alipiga kura kukubaliana na Bush na Obama alipiga kura na hapana. Obama aliutumia uamuzi huo kama sehemu muhimu ya campaign hasa ukizingatia mwaka 2008 wamerekani walikuwa wamechoshwa sana na vita vya Iraq.
Vile vile mwaka 2007, rais wa Marekani, George W. Bush aliamua kuongeza idadi ya majeshi ya marekani kwa kiwango fulani nchini Iraq (Iraq war troop surge) ili wajaribu kuleta amani iraq halafu baadaye ndio waondoke. Hii ilipingwa na
Obama pamoja na waziri wa sasa wa ulinzi (Chuck Hagel) ambaye anatoka chama kimoja na Bush. Huu uamuzi wa troop surge ulikuja kuonekana baadaye kwamba ulikuwa uamuzi sahihi kwani ulikuwa na mafaniko makubwa. Wakati huyu
waziri wa ulinzi anahojiwa na masenata wenzake kabla hajawa confirmed kuwa waziri wa Obama katika kipindi chake cha pili, (kura yake) maamuzi ya Hagel kuhusiana na surge yalikuwa kati ya vitu ambavyo vilikuwa mwiba kwake, katika kuthibitishwa kwake kuwa waziri wa ulinzi. Kwa watu waliofuatilia ile hearing watakuwa wanakumbuka jinsi Mccain alivyombana huyu Bwana.
Pamoja na faida zinazoweka kupatikana kutokana na kura ya wazi, nadhani kwa nchi zetu hizi inabidi tufikiri kidogo kabla ya kuamua kufanya kama wanavyofanya wenzetu. Ninaamini wengi tutakuwa tunakubaliana kwamba nchi zetu nyingi za kiafrika, ubabe na ulipizaji wa kisasi kutoka kwa watawala wetu bado ni kitu ambacho bado kimeshamiri, hivyo ukisema watu wapige kura za wazi, wanaweza wakafanya maamuzi kinyume na utashi wao especially kama maamuzi yao wanaona yanakwenda kinyume na maamuzi ya viongozi wao. Matokeo yake hatutapata maamuzi sahihi ya wajumbe na nadhani hii itaondoa dhana nzima ya maamuzi sahihi, kwani maamuzi yatakuwa ni ya watu wachache tu ambao wengine watakuwa wametumika kama rubber stamp tu...
Kura ya siri
Kura ya siri ina uzuri kwamba mtu anakuwa na uhakika kwamba maamuzi yake ni siri yake mwenyewe. Hii itampa mtu confidence ya kuamua kile anachokiamini ni sahihi kwani ana uhakika kwamba maamuzi yake hayatatumika na yeyote kumfanyia hujuma huko mbeleni. Pamoja na kwamba kwa kutumia njia hii, records za wajumbe pamoja na maamuzi yao hazitakuwepo, lakini tutakuwa na uhakika wa maamuzi sahihi ambayo ndio yenye umuhimu zaidi ya hizo records. Mimi ninaamini hii njia ni nzuri kwa jamii kama yetu, ambapo mambo ya intimidation na matisho kutoka kwa watawala bado yapo kwa wingi.
Nini kifanyike ?
Kuna mjumbe mmoja wakati anachangia kwenye bunge la katiba jana alisema amepata simu kutoka kwa wananchi wake wakisema wanataka wabunge wafanye maamuzi kwa uwazi ili wafahamu wabunge wao wamefanya maamuzi gani. Hiyo ni sawa na lazima kutakuwa na wengine wengi tu wenye mawazo kama hayo. Vile vile ninaamini kuna wananchi wengine (kama mimi) ambao wanataka maamuzi yawe ya kura ya siri. Katika hili, watu mbali mbali wanaweza wakawa na misimamo tofauti.
Namna sahihi ya kuamua nini kifanyike ni kujua wengi wanataka kitu gani na hicho watakachoamua wengi ndicho kifanyike. Kama wengi wanataka kura ya siri, itakuwa wazi wengi wanaamini kwamba kura za namna hiyo ndio zitatota maamuzi sahihi na hivyo itabidi zipigwe kura za siri. Na kama wengi wanataka kura za wazi basi itabidi zipigwe kura za wazi. Sasa hakuna namna tunaweza tukapiga kura wote na kujua tunataka nini, ila tuna wabunge wa katiba ambao baadhi yao ni wawakilishi wa wananchi wa kuchaguliwa na wengine ni wa kuteuliwa (ambao nao originally walitoka kwenye makundi ya wananchi). Hawa wanaweza kupiga kura kwa niaba yetu, na watakaloamua ndilo tutakuwa wote tunalitaka na ndilo lifanyike.
Ninachoshauri ni kwamba KURA HII ya kuamua whether maamuzi ya Bunge la Katiba yawe kwa kura za wazi au za siri, yafanyike kwa KURA YA SIRI. Kama wataamua kura ziwe za wazi sawa, kama wataamua ziwe za siri sawa, ila kura hii ya kati ya haya maamuzi mawili iwe ya SIRI. Nadhani kwa wale wanaotaka kura za wazi hoja yao kubwa ni kwamba wananchi wajue wabunge wao walifanya maamuzi gani kuhusu katiba, na hii kura ninayoizungumzia hapa haihusu katiba bali inahusu tu maamuzi ya kanuni ya upigaji kura.