ushauri nasaha unahitajika.

Expectation is the mother of all disappointment!

Nitaisoma zaidi hii thread, nimeishia katikakati.
 
Kaka Mbu thanks,

Sijapitia posts zote kusoma ila i think ni mutual understanding between the two .. sisi especially in african society neno mtoto ni la familia yote nasi la wanandooa peke.. its an open table discussion na kila mwanandugu ana right ya kuulizia 'whats is happening?' sasa wanandoa cant elude this business ya kuwa na mtoto .. they are haunted from all corners hata marafiki wataulizia pia coz ndo jamii yetu ilivyo. mm nasecond adoption .. coz in our african traditional society theres no way utamkataza mwanaume kuoa, kwani jamii nzima itamsuport kwa hili .. kama kaoa kanisani watamlazimisha hata afanye traditional ama secret wedding.. ilimradi tu apate mtoto ..mke wake akitaka asitake .. kwani itakua right yake.. dini pia kama ss waislamu kama mke ambaye anamatatizo ameridhia mume anaweza akaoa .. na mwanamke pia asirule out the fact kwamba mwanaume kwa kigezo hiki bila ridha yake atalazimisha tu kuoa.

adoption ambae na advocate for ni within the family .. unachukua mtoto wa ndugu yako na anakua wa kwako ... which is not bad .. rights zote zinahama kwako .. some even do it well .. kama binti yoyote hapo nyumbani amebeba mimba bila mpango na baba wa mtoto kamkimbia .. huyu mtoto anakuwa wa familia na kumpa nafasi zaidi anapewa one of the victims of such circumstances kumlea ...ama hata mwengine ambaye amefiwa na wazazi ama hata mmoja tu anajitolea kumpa mwenzie mtoto .. especially wanawake between dada's this is very possible. In my family this has happened, kuna cousin wangu mmoja has the same problem, mdogo wake akaamua na mumewe kwamba they had enough kids .. 3 ila they should try the fourth time na wakifanikisha .. that kid atakua wa sistaake .. alhamdulillah it happened so ... kila kitu cha huyo mtoto kikawa kinatoka kwa huyo mamaake mpya.. till alivyoacha kunyonya ..like mwaka mmoja mtoto akapelekwa kwa mamaake ... mpaka leo shes 18 na anatambua ukweli ila mama mwengine hamjui anamtambua mamaake huyo alomlea ..

This issue tackled kifamilia ina very excellent results .. coz we cant elude this .. all the family is concerned coz hata kama umezaa the whole family will participate kuwalea hawa watoto wako ... you cant close doors to all.


To sum it up .. si dhani kama couples should pretend kama hakuna ufa ...upo .. swala la watoto ni lazima kwa mtu yoyote .. atatamani tu kwani ni vitu ambavyo mtu anafeel vitakamilisha maisha yake .. kuavoid affairs za siri .. mtu kuja kushtukia kwamba mume wake anamke njee na watoto, i would second adoption lakini within the family bounds .. naona ina hadhi zaidi .. otherwise any other type of adoption is also good ila hapa mtoto baadae akikukua theres a possibility akaanza kudadisi ametoka wapi .. na mambo identity yake itaweza kumsumbua kisaikologia akiwa mkubwa.
 

...kwanza nakushukuru sana dada'ngu kuitikia wito huu. Pili, maoni yako yaliyojaa busara na hekima. Shukran sana kutumia muda wako mduchu ulokuwa nao angalau kuchangia katika hili.

Tukirudi kwenye mada, umezungumzia adoption...na uwezekano wa adoption within the family. Hili ni jambo la busara sana, ila adoption inakuja na ridhaa vile vile ya mleaji.

Kama unakumbuka, au mlisoma... suala la adoption niliandika is out of question sababu ni; Bi mdogo bado kabisa hajashaurika (kukubali) kwamba wamchukue mtoto 'yatima' wamlee. Hapa namaanisha, Bi mdogo huyo yeye keshafunga milango yote ya alternatives za kuwa na mtoto ila kwa IVF tu...

Awali baada ya vipimo kadhaa kuonyesha matarajio ya uzazi kwake (kwa njia za kawaida) hayapo, Mume alikuwa radhi ku adopt lakini mke hakutaka wala hataki kusikia lolote. Yeye anataka abebe mimba na azae mwanae, potelea mbali hata ikiwagharimu ndururu yao ya mwisho! The 'spooky' part ni kwamba anataka lazima azae na Bwana huyo japo mwanaume keshasema hapana.

To sum it up .. si dhani kama couples should pretend kama hakuna ufa ...upo .. swala la watoto ni lazima kwa mtu yoyote .. atatamani tu kwani ni vitu ambavyo mtu anafeel vitakamilisha maisha yake

...Katika uliloandika hapo, nadhani uwingi au upungufu wa Imani utachangia. Kwa imani yangu mimi naridhia kwamba mtu anapata ajaliwalo, na anaepushiwa lisilo na heri naye...

Kushawishika wanandoa juu ya mambo haya kunahitaji nguvu ya imani kwa kweli, kama inavyosimuliwa kisa cha Nabii Ibrahim, Mkewe Sarah na kijakazi wao Hagar.
 
Kaka Mbu, kwani uhusiana kati ya bi mdogo na bi mkubwa upo vipi ? maana mara nyingi huwa kuna mvutano wivu vinyongo na ushindani mkubwa kati ya Mke aliyetangulia na Bi mdogo, hasa kama Bi mdogo kwa namna moja au nyingine alikuwa kwenye picha kabla ya bi mkubwa kutalikiwa (situation ambayo hutokea mara nyingi), mshauri bwana mkubwa asi underestimate hilo, kama kuna tatizo liwekwe wazi lijadiliwe, inaweza ikasaidia kujua mzizi wa tatizo zima

Wengi ambao shida pekee ni kukosa mtoto, baada ya kujaribu njia mbalimbali bila mafanikio wanaweza kupokea ushauri na kufarijika kwa kulea watoto wa wenzao, kuadopt, kulea yatima etc, hali ambayo haiwezi kumfariji anayeshindana na mwenzie kwa sababu hata akiadopt bado atakuwa “inferior” kwa mwenzie kwa sababu hajazaa mwenyewe, ndio maana wengine huwa wanakataa kabisa adoptions au kulea watoto wa wenzao kwa sababu wanajua hiyo haiwezi kuwa sulution ya matatizo yao

Kuna mambo yanayo leta hisia kwamba inawezekana machungu yake bi mdogo yanasababishwa na ushindani kati yake na bi mkubwa kama vile
 bi mdogo kusema ananyanyasika kwa vile hazai
 watoto wa bi mkubwa aliowalea toka utotoni kuhamia kwa mama yao na bi mdogo kutokuelewana na watoto hao baada ya wao kuhamia kwa mama yao
 bi mdogo anataka kupata mtoto wa kuzaa mwenyewe na si vinginevyo
 bi mdogo kutafuta mtoto kwa waganga wa kienyeji _ inawezekana kuna mganga aliye mpoint bi mkubwa kama ndio mbaya wake maana tunasikia waganga wengi ndivyo walivyo
 

Safi sana Triplets umelenga kwenye kiini hasa, bado kidogo umalize kulikamua jipu...

...uhusiano wao mbaya sana. Bi mkubwa anaona kama si bi mdogo, huenda huyo bwana mkubwa angerudiana nae. Na bi mdogo anaona asipozaa mtoto, huenda Bw'mkubwa akarudiana na mama watoto wake. Wakati huo huo, huyo mheshimiwa keshaapa heri aoe mke mwingine kuliko kurudiana na huyo ex-wife wake, kwa jinsi alivyomtenda...

 
Mh Mbu,
Kwa heshima zote naomba nami niweke neno kwenye hii mada nyeti.
Mwanzo wa mapenzi na hata ndoa ni raha tupu na focus huwa ni kwa wawili wapendanao.Kipindi hiki ni vigumu kuuona ukweli na hata kama wawili hao wangeambiana watathmini katika ndoa yao itakuwaje kama hakuna watoto, bila shaka kila mmoja kwa wepesi sana angesema kuwa hiyo haitakuwa hoja.Mapenzi yangekuwa yamewapofusha wasiweze kuuona ukweli, hivyo basi naomba nitofuatiane kidogo na Mwana F1 hapa chini:

Mtoto ni majaaliwa ya ndoa/matunda ya ndoa, hivyo inawezekana mkapata au mkakosa.
.
Hili ni neno ndugu yangu Pretty... kweli kabisa wanandoa hiki ni kitu wanapaswa kujua ila wengi wanakuwa wakiweka mbele tegemeo la watoto wakisahau kuwa Muumba wetu anakuwa na mpango na kila kiumbe wake.Kuna watu wameumbwa bila uzazi kwa sababu huenda kazi yao ni nyingine kabisa...huenda wao wameumbwa waje kusaidia wengine wenye mahitaji mfano kutunza mayatima au kwenda kutoa huduma nyingine zenye kuhitaji mtu mwenye muda wa kutosha.Lakini hili linahitaji mtu mwenye imani ... na bahati mbaya hatuwezi kujua kiwango cha imani cha Bi Mdogo huyu.Ukizingatia pia kama aliwahi kuharibu mimba huko nyuma basi itakuwa ngumu kwake kukubali ushauri kama huu.


Ushauri kwenye hili ndugu yangu nitasema hivi:
Wanawake wengi wanaamini kuwa bila kuzaa basi hawajamilisha uanawake wao...ndio utawakuta mara waende kwa waganga mara watumie hata hila za kujaribu kupata mimba kutoka kwa wanaume wengine alimuradi basi wathibitishe wako kamili;
Kuna swala la security siku za usoni kama livyosema Kweli hapa chini.Watu wengi hili hawalioni na hasa kama bado ni vijana.Angalia hata kwa wazazi wetu wanavyojisikia fahari kutambulisha wajukuu zao ndio tutaelewa kwanini bi Mdogo anang'ang;ania kuzaa.Uzeeni kuna upweke sana.Focus ya wazee mara nyingi ni kuangalia watoto wa watoto wao.Sasa Bi mdogo hili linampa shida sana.Ila anaweza kushauriwa kuwa hata kama hataki kuasili ( adoption) bado kuna watoto wa ndugu wa upande wake hata kama wale watoto wa bi Mkubwa maelewano yametetereka.Cha muhimu ni yeye kujenga ukaribu hasa na watoto wa nduguzake ili waje wawe nguvu yake huko mbeleni.Hii nimeiona hata kwa baadhi ya ndugu zangu mimi mwenyewe na inafanya kazi vizuri tu.

Nionavyo mimi huyu bibie anasumbuliwa zaidi na mawazo (sio ya kukosa kizazi) bali ya maisha yake ya baadae pindi huyu bwana akifa?
!

Wakati mwingine watoto wa kufikia hujakubadilika hata kama unawalea vema kama Mbu ulivyoonyesha hapa chini.Cha msingi ni huyu Bi Mdogo ashauriwe kuwa pamoja na yote, ajiepushe kujibishana nao na aendelee kuwaonyesha upendo tu maana huenda hawa watakuja kumfaa huko mbeleni.Kuendelea kujenga chuki ni kwa hasara yake mwenyewe maana Bw Mkubwa akiondoka duniani, basi ajue hatakuwa na mtetezi.



Huyo bwana naye inabidi aonyeshe msimamo wake katika suala hili... ama ampe uhuru aende kuolewa kwengine ama mwanamke akubali matokeo atulie.Isitoshe huyo bi Mdogo hatujaelezwa kama yuko katika nafasi gani kuja kulea watoto wadogo wakati mume umri ushaenda.Ashauriwe aangalie hilo nalo maana kuzaa kunaendena na majukumu.Je atakuwa tayari kuja kulea "wajukuu" na "babu yao" pia?Kulea watoto wadogo ni shughuli achilia mbali kumlea mume anayezeeka.


Kwa vyovyote ushindani wa wanawake hawa utaendelea kuwepo na hata kama bi mdogo atazaa asifikirie ndio mwisho wa matatizo.Hivyo Bi Mdogo ashauriwe ajitahidi kutokuongeza chumvi kwenye kidonda.Amheshimu Bi Mkubwa kwa vile alimtangulia na pia ajifikirie hali yake na matatizo aliyo nayo.Huenda hata haya matatizo ya kutaka kuzaa yanaongeza stress kwa bw. Mkubwa kiasi akajaona bora kujipumzisha kwa Bi Mkubwa kuepuka presha za bi mdogo.
Mbu naona umekuwa mstaarabu ukaacha kutuhabarisha jinsi bw. Mkubwa anavyowekwa kwenye wakati mgumu wa kuhakikisha mtoto anapatikana kwa bi Mdogo maana sidhani kama bwana huyo ana raha na hata anaweza kuhimili mikikimiki ya mradi huo wa kumzalisha bi mdogo.
 
Last edited:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…