Ushauri: Nataka ku INVEST 750,000- Forever Living

Ushauri: Nataka ku INVEST 750,000- Forever Living

Nimefuatilia maoni ya waliotangulia nimechoka mwenyewe. Kwa kweli wengi wape, hiyo siyo biashara ya kufanya.
Ni ukweli mtupu sasa hivi kumconvince mtu kununua hizo products ni vigumu kwa sababu watu walishazistukia, sasa ndiyo itakuwa kuwambia wajiunge kabisa! Bahati mbaya zaidi wanaojaribu kuwaconvice watu waingie kwenye hiyo biashara wenyewe waanakuwa wamechoka, hawana mafanikio yeyote.
Anyway...mwisho wa siku chagua ni lako, kusuka au kunyoa.
 
Huu ni uchuuzi, au tuseme hakuna tofauti na umachinga. Hizo bidhaa zenyewe zinapewa umaarufu tu lakini are no better than common ones. fikiria tu business nyingine, hii tupa kule, utasaga lami hadi uchoke. Bidhaa za 750 k sudhani kama unazihitaji ili uzitumie. tumia bongo mkuu

ulishawah kutumia hta moja?au unaongea tu na we uonekane,kinachowashinda watu ni bei bt kaz zinafanya na zko different,me nahic ambao hawana uwezo wa kuzinunua wanabak kuponda tu,simply coz hawana uwezo wa kuzitumia,watanzania weng wakishndwa ku afford kitu wanaponda,ha ha..jipange mkuu
 
Biashara ya network marketing ni nzuri sana sivyo watu wengi wanavyodhani,ile ni kama kuwekeza tofauti kuna ukweli unafichwa ambao watu hawajui.
Nimefanya utafiti ili uanze kupata faida inachukua art least miaka miwili,kujifunza product,jinsi ya kufanya biashara,kufanya semina nk.
Pamoja na yote unashauriwa kwa muda huu usiitegemee hiyo biashara ndo maana unashauriwa kutumia masaa mawili tu kwa siku.
Mbali na yote ukipiga gharama za semina,mawasiliano, mpaka unafika hatua ya kuwa meneja (ambayo ndio mwanzo wa mafanikio) utakuwa umetumia si chini ya mil 3.5 na muda usiopungua miaka 2
ndio maana wanaongelea sana wa ziada si fulltime.
Nimeona nikupe black and white japo kidogo sana.
 
Nafikiri mafanikio yako katika biashara hii yanategemea zaidi watu wanaokuzunguka kama wana uwezo na uhitaji wa bidhaa hizi.

Bidhaa hizi ni ghali sana na kuzitumia continously unahitaji kuwa na mpunga wa kutosha.

Pili bidhaa hizi zinahusiana na mambo ya afya. Wengi wanaotumia ni wale ambao wanajali saana afya zao au ambao afya zao ni mgogoro.

Hiyo wateja wako watakuwa watu wenye mpunga na mahitaji kama nilivyoeleza ambao ni seti ndogo sana ya watanzania. Wengi wanahitaji lakini hawana uwezo wa kununua.

Wanaofanikiwa ni wale ambao wao wenyewe ni watumiaji wazuri na huwashawishi jamaa wanaowazunguka na kuwafanya pia kuwa watumiaji wazuri ambao pia hushawishi wenzao wengine na kuendelea
 
Habari Wanajamvi,

Nimeelezwa Network Marketing ya Forever Living Products inalipa. Natakiwa ku deposit Tshs 750,000. Mwenye ukweli kuhusu hii business.

Nimejaribu ku search kwenye mitandao, maelezo mengi yanaanza kwa ku clash upotoshaji wa hii biashara. Nimepatwa na mashaka, naombeni ushauri.

Ilianza GNLD watu wakaingia kwa mbwembwe kisha wengi ikala kwao. Hata kwenye deci wapo walio nufaika lakini wengi ikala kwao. Si lazima kila mtu awe mjasiria mali, je kwa sasa unafanya shunghuli gani?
 
Ilianza GNLD watu wakaingia kwa mbwembwe kisha wengi ikala kwao. Hata kwenye deci wapo walio nufaika lakini wengi ikala kwao. Si lazima kila mtu awe mjasiria mali, je kwa sasa unafanya shunghuli gani?

Employed!
 
Achana hiyo biashara kabisa. Akili, muda na nguvu utakayoitumia ni mara kumi ukajifungulia genge la mahitaji ya nyumbani utafanikiwa kwa haraka. Huko Forever utatafuta pressure.
 
Hamjaisoma fresh hii biashara, nitafteni niwape njia ya kufikia manager just for one month u don't have to sell products wala kumconvice mtu aingie chini yako what your suppose to do just kumuinvite mtu kweny presentations tu, just for one week nimekuwa supervisor ninaelekea kuwa assistant manager na ndani ya mwezi nakuwa manager huu sio uongo tar 15 nmeingiziwa lak 4 kwenye my account next month nna more than 1m, amkeni watanzania, na kuna mambo meeengiiii yakukuongezea kipato mfano kununua shares only members wanatakiwa kununua tena kwa bei rahiiisi
 
Nimeshatumia Sana. Mfano ni SHIELD deodorant ya FOREVER. Ni nzuri lakini pia ni ghali. Kwa uhakika wateja wake siyo wengi hivyo unaweza kukaa na bidhaa kwa muda mrefu. Hapa cha msingi ni kuwa hii biashara haina tofauti na umachinga kwa sababu kwanza lazima umshawishi mteja aamini unachomwambia ni sahihi lakini pia lazima ufanye recruitment ya watu zaidi ndio uanzepata faida. For me' this is a lazy man's empire.
 
Hamjaisoma fresh hii biashara, nitafteni niwape njia ya kufikia manager just for one month u don't have to sell products wala kumconvice mtu aingie chini yako what your suppose to do just kumuinvite mtu kweny presentations tu, just for one week nimekuwa supervisor ninaelekea kuwa assistant manager na ndani ya mwezi nakuwa manager huu sio uongo tar 15 nmeingiziwa lak 4 kwenye my account next month nna more than 1m, amkeni watanzania, na kuna mambo meeengiiii yakukuongezea kipato mfano kununua shares only members wanatakiwa kununua tena kwa bei rahiiisi
Binafsi sijakuelewa unachotaka kuzungumzia...toa facts zinazoeleweka mkuu!
 
Back
Top Bottom