Ushauri: Natamani kuomba uhamisho nikafanyie kazi kijijini kwa wazazi wangu

Ushauri: Natamani kuomba uhamisho nikafanyie kazi kijijini kwa wazazi wangu

sepema

JF-Expert Member
Joined
Jun 13, 2019
Posts
591
Reaction score
1,001
Salaam wakuu,

Nimefanya kazi huku mjini kwa miaka10 saivi. Bado sina ndoa japo umri unaruhusu kufanya hivyo. Huku mjini sijafanya uwekezaji wamaana kutokani na changamoto za gharama za maisha kuwa juu.

Nahisi nalipa kodi kubwa kuliko watanzania wenzangu wakijijini kwani huku mjini kila ikianza siku lazima pesa itumike kwa mahitaji mbalimbali.

Katika siku zahivi karibuni nimejikuta nikitamani kurudi kijijini kwa wazazi wangu nikafanyie kazi huko kwani taasisi ninayoitumikia ina ofisi zake kule kijijini pia.

Kwa mtazamo wangu naona kuwa kwangu itakuwa rahisi kutoboa kimaisha kwani kijijini Kuna rasilimali nyingi muhimu ambazo naweza kuzibadilisha kuwa fedha. Kuna ardhi nzuri na maji yakutosha, vyote hivi nivya bure.

Je, kabla sijachukua uamuzi huu nijipange kwa changamoto zipi labda?

Au wazo hili litakua na faida kwangu kwa angalau asilimia 90?
 
Una point nzuri sana, ila walakini yangu inaanzia pale unaposema unarudi kijijini walipo wazazi wako (bila shaka na ndugu wengine) nauogopa sana mfumo wetu wa kijamaa hasa kwenye harakati za kuyatafuta maendeleo.
Namimi wasiwasi wangu nihuo tu mkuu
 
Namimi wasiwasi wangu nihuo tu mkuu
Nenda kijiji kingine katika wilaya hiyo hiyo. Siyo lazima urudi kijiji walipo wazazi wako, hautatoboa maisha.

Binafsi naona kijana mwajiriwa wa kijijini akituliza akili anatoboa maisha kuliko wa mjini.

Ila ukizeeka inabidi uishi mjini karibu na huduma za afya mana magonjwa nyemerezi ni mwengi!
 
Kama umepima na kuona mwenyewe hapa mjini unapiga maktime..ondoka mapema ungali una nguvu.

Ila usikae kijijini kwenu nenda wilaya ya karibu.

#MaendeleoHayanaChama
 
Una point nzuri sana, ila walakini yangu inaanzia pale unaposema unarudi kijijini walipo wazazi wako (bila shaka na ndugu wengine) nauogopa sana mfumo wetu wa kijamaa hasa kwenye harakati za kuyatafuta maendeleo.
Jamaa kakushaur vema,rudi kijijini lakini kata au tarafa tofauti na ilipo orgin yako(hutajuta)
 
utaweza kuwa bandidu sura ya mbuzi kwa ndug zako..? Maana wew ndio utakua Mkombozi na Kimbilio lao ktk raha na shida, kwahiyo pesa zitakutoka zaidi. Sisi tunao ishi mjini hatusumbuliwi na ndugu kuhusu misiba na sherehe zisizokua na kichwa wala miguu huko Kijijini
 
Back
Top Bottom