1. Blueberry
Blueberry ni matunda yanayosaidia sana
kuongeza nguvu za kiume, wengi hupendelea
kuyaita viagra asilia kutokana na kazi
inayoifanya mwilini. Blueberries ina
virutubishi vinavyoimarisha mishipa ya damu
na kusaidia mzunguko mzuri wa damu
mwilini. Damu ndio kila kitu katika nguvu za
kiume. Vilevile, blueberries zina nyuzinyuzi
( fiber ) ambazo husaidia kuondoa kolesteroli
(Cholestrol) mwilini kabla hazijanganda
kwenye mishipa ya damu. Kuwa na mzunguko
mzuri wa damu husaidia mwanaume aweze
kuhimiri mapenzi wa muda mrefu zaidi.
2. Mtini (Figs)
Mtini (figs) ni matunda yenye kiwango
kikubwa cha amino asidi, ambayo ni kiungo
kikubwa katika kuzalisha homoni mwilini.
Homoni ndio kishawishi cha nguvu za kiume
mwilini. Kukosa amino asidi huweza
kusababisha kukosa hamu ya mapenzi au
kupungukiwa na nguvu za kiume.
3. Chaza/Kombe wabichi (Raw Oysters)
Chaza wana kiwango kikubwa cha madini ya
zinc. Madini za zinc hutumika katika
utengenezaji wa homoni ya testosterone,
shahawa na mbegu za kiume . Uwingi wa
uzalishwaji wa testosterone mwilini huathiri
pia hamu ya mapenzi na nguvu za kiume
ikiwa kidogo huondoa hamu, ikiwa nyingi
hupelekea hamu na nguvu zaidi.
Kupungukiwa kwa madini ya zinc
husababisha kupungua kwa nguvu za kiume,
udhaifu (uhanithi), na kushuka kwa kiwango
cha uwezo wa kufanya mapenzi.
4. Karanga
Karanga ni chanzo kikubwa cha kujenga
protini mwilini. Karanga huwa na kiwango
kikubwa cha amino asidi ambayo husaidia
kuweka vizuri mfumo wa damu, hivyo
kusababisha kuongezeka kwa kiwango cha
ufanyaji mapenzi.
5. Vitunguu saumu
Kitunguu saumu kina allicin, kiambato
kinachosaidia mzunguko mzuri wa damu
kwenye viungo vya uzazi. Kuwa na mzunguko
mzuri wa damu kwenye uume ni sababu
kubwa ya kuongeza stamina ya kufanya
mapenz
6. Ndizi
Kuwa na stamina ni muhimu katika ufanyaji
mapenzi. Ndizi ni chanzo kikubwa cha
vitamin B ambayo husaidia sana katika
kuongeza stamina na nguvu mwilini hasa
wakati wa kufanya kazi nzito. Ndizi ina
kimengenyo cha Bromelain ambacho
huongeza nguvu za kiume, ashki ya mapenzi
( libido).
7. Chocolate
Chocolate inasaidia kuongeza stamina
kwenye kufanya mapenzi kwasababu ina
viambato vya phenylethylamine na alkaloid .
Phenylethylamine ni kiambato
kinachopelekea kujisikia vizuri, hasa wakati
wa kufanya mapenzi na alkaloid huongeza
stamina na nguvu wakati wa mapenzi.