Ushauri:Nijenge au clearing and forwarding

bullion

JF-Expert Member
Joined
Aug 23, 2014
Posts
309
Reaction score
112
Wakuu habari za majukumu,

Nina kiasi cha milioni mbili na nusu, naomba ushauri wenu kati ya haya mawili
-Nina eneo kujenga chumba self kimoja cha standard ni milioni mbili na nusu, umeme, maji vyote vipo, kodi kwa mwezi elfu 50
-Niwe patner kwenye kampuni ya clearing and forwarding ambayo ndio kwanza inaanza

Naomba ushauri wenu
 
Usiwe Muoga wa maisha mkuu.

Wekeza kwanza kwa hela hiyo ukiingia kwenye C&F company kama mtaweza kuisimamia vizuri na mkaweza kufanya na strategy za market nzuri mbona ndanu ya miezi miwili tu unapiga mara nne ya hiyo hela.

Sijawahi kujutia kuwa kwenye hii industry ya Freight forwarders ingawa sasa hivi wateja tunagombea ila ukipata connection za wateja wa nje unapata profit
 
Kumbuka kampuni ndio inaanza, na wateja saivi wamepungua, je huoni kwamba itakula kwangu
 
Kumbuka kampuni ndio inaanza, na wateja saivi wamepungua, je huoni kwamba itakula kwangu

Hii connection ya C/F nami naihitaji niwekeze tatizo sina ujuzi, kama una uzoefu niambie hata kuwa partner
 
Mkuu unaweza kujenga lakini nikwambie kitu kimoja, moja ya kitu ninachokijutia ni kutumia pesa kujenga nyumba katika hatua za mwanzo za maisha yangu, ningeambiwa nirudie maamuzi kwa kiwango cha pesa nilizotumia ningenunua kiwanja nikakiwekea alama alafu pesa nyingine nikanunue mashine mbali mbali, return ya nyumba ni ndogo sana ukilinganisha na pesa ya ujenzi. Alafu ukijenga kwa kutumia mafundi wasio wasomi hawawezi kukadiria gharama, ukianza kujenga ndio utasikia mara hiki mara kile.Utakuta mtu anapata kodi ya laki nne au tano kwa mwezi nyumba kaijenga kwa millioni sabini mpaka mia.Yaani hapo pesa itarudi baada ya miaka kumi na tano. Million sabini mpe muhindi au mchina uone baada ya miaka mitatu atakua wapi?Ninamshukuru mtu mmoja nilipotaka kununua aina fulani ya gari yangu ya kwanza alinishauri kutokana na pesa zenyewe za manati ninunue gari ndogo pesa nyingine ninunue mashine au kitu cha kuniingizia pesa zaidi. In real world some assets are not real assets are liabilities.
 
Nyumba ya kuishi siku zote ni liability. Hata hvyo kuwa makini zaidi utakapowekeza kwenye kitu usichokuwa na utaalamu nacho hata kidogo. Hali ya soko pia kwa upande wa clearing sio nzuri ila sikwambii usiwekeze. Jitafakari then uamue. The choice is yours
 

Nadhan umemaliza kila kitu
 
Partner ="kamikaze tz, post: 23992218, member: 430886"]Huo uzi unaitwaje mkuu[/QUOTE]
Patner for commission basis
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…