Uume kulala baada ya kupiga goli kifiziologia ni kitu cha kawaida. Kitaalamu inaitwa "Refractory period", kipindi hiki kinatofautiana kati ya mtu na mtu, inaweza kuchukua dakika kadhaa au hata siku kadhaa. Umri, lishe mbovu, kukosa mazoezi, maradhi na vitu vingine vingi tu, vinaweza kuchangia huu muda kuwa mrefu.
Kifizilojia homoni ya OXYTOCIN huwa inakuwa nyingi sana pale sisi wa jinsia ya me tunapopiga goli, na uchunguzi unaonyesha ya kuwa kiwango kikubwa cha oxytocin kinaathiri hii kinzani kipindi (REFRACTORY PERIOD), oxytocin nyingi=refractory period ndefu..
Kemikali nyingine inayoathiri kinzani kipindi (refractory period) ni PROLACTIN, ambayo huwa inakandamiza uwepo wa kemikali ya DOPAMINE, kemikali ya DOPAMINE ni muhimu sana katika kuamsha ashiki na nyege. Wafamakolojia na wanabiokemia wanaangalia uwezekano wa kutumia dawa ya CARBEGOLINE (DOSTINEX, CARBESER), CARBEGOLINE inazuia uwepo wa PROLACTIN wakati goli likifungwa, hivyo kufanya DOPAMINE iwe nyingi ya kumwaga tu na matokeao yake ni kwamba hamu ya kugegeda itaendelea kuwepo na uume hautalala. Kwa bahati mbaya Carbegoline ina madhara mengi sana tu.
Wenzetu wa jinsia ya KE wengi wao hawana hii refractory period, ndio maana wanaweza kuwa na "multiple orgasms" (back to back), ila wengine huwa wanajisikia SENSITIVE sana kwenye clitoris mara tu baada ya kupata orgasm.
Cha maana wewe fanya tizi, angalia lishe yako, na usiwe na pressure, halafu kumbuka usiendekeze ngono zembe.