Ushauri please !!!

sagna

New Member
Joined
Mar 6, 2012
Posts
2
Reaction score
0
Kuna jamaa yangu leo amegunduwa kuwa mkeo huwa anatabia ya wizi pesa anazotoa za matumizi anapeleka kwao. Na gharama za nyumbani zimepanda lakini huduma na chakula ni kile kile leo katika pekua pekua zake kakuta laki moja chini ya meza na jana tu mkewe alikuwa analalamkika kuwa pesa haitoshe anayo acha aongeze kila akifika stori ni pesa pesa. Yeye ameamuwa ampe talaka arudi kwao mimi nimemshauri ampe nafasi nyingine ya kujirekebisha, jee nyie mnamshauri nini??????
 
Sasa pesa zote anapeleka wapi jamani?
Labda anashida kubwa na mume wake si muelewa?
Na huyo mume asiwe mwepesi kumtishia mkewe talaka!
 
Huu uzi unanikumbusha mbali sana, kuna ile nyimbo ilikuwa inaimbwa hivi.

Huyu niliyeoa, sina la kusema
Mshahara nikipata
Bajeti apange yeye
Anajenga nyumba kwao
Mimi kwangu midabwada

Mimi naona ampe muda wa kujirekebisha, yawezekana mume hampi hata pocket money ndio akaamua kuiba.
 
Huu uzi unanikumbusha mbali sana, kuna ile nyimbo ilikuwa inaimbwa hivi.

Huyu niliyeoa, sina la kusema
Mshahara nikipata
Bajeti apange yeye
Anajenga nyumba kwao
Mimi kwangu midabwada

Mimi naona ampe muda wa kujirekebisha.
Du! kumbe na wewe umekula age kama mimi? mmmhh!
 
He just need to judge if he has been a good husband, Kama ni mbahili sana kwa mkewe na mke Hana kipato unategemea niño? He can only be a judge by himself, ukimwambie ampe naFasi Kama lijamaa lenyewe Lina matatizo itasaidia niñi?

Halafu achana na mapenzi ya watu, hujui wamekutana wapi na kwa mistake gani!

 
anamuachia kiasi gani mpaka aseme anaiba pesa za matumizi?

mke haruhusiwi kuwa na pesa?

hana kazi wa kibiashara wala hachezi upatu au hayumo kwenye vikoba?

huyo rafiki yako kamchoka mkewe/ au ni aina ya wanaume wasiotaka wake zao wawe na kitu aka wafujaji
 
Uwazi na mawasiliano ndani y mahusiano ni kitu kizuri sana,

Huyo mwanamme inawezekana ana kipato kikubwa tu lkn ndio hivo hajampa nafasi mkewe kuwa muwazi na kujieleza shida zake especial km ni mama wa nyumban ndio maana inampelekea kufanya ivo au kutafuta njia ya kumaliza shida za kwao,

Tena anatakiwa amshukuru mkewe kwan hiyo njia nayotumia kubana hiyo hela ni nzuri kuliko angetafuta bwana wa nje wa kummalizia matatizo yake,

Na huyo mwanamke naye namlaum kwann asifunguke kwa mumewe japo akamsaidia hata kuwa na kijimradi cha kumwingizia chochote ili ajibane yeye na kumaliza shida za nyumban kwao?

Cha kufanya huyo mwanaume aache akili za kitoto hawezi acha mke anayempenda kwa kosa km hilo,hapo tatizo ni uelewa,uwazi na mawasiliano yako kuwa madogo,

Anatakiwa kumuonya mkewe kwa kumuelewesha na sio kumgombeza,na ampe mtaji ili ajishuhukishe na kupata japo kipato kidogo kwa ajili ya mambo yake binafsi na kuwasaidia ndunguze!!!
 
nadhani kuna mapugufu kwa wote wawili mume na mke wanatakiwa wakae waeleweshae hasa suala la kipato
 

Inawezekana huyu mumewe huwa hana muda mzuri wa kukaa na mkewe na kudiscuss matatizo/mahitaji ya pande zote mbili. Na pia inawezekana mkewe huyo hana ajira na hana namna yoyote ya kumuingizia kipato nje na hela ya mboga anayoachiwa. Hivyo yumkini mkewe kaamua kutumia utaratibu huo ili kusaidia wazazi na ndugu wa upande wake. Ushauri: Mwambie jamaa awe karibu na mkewe na kumhoji kwa nini anachukua pesa na kupeleka kwao bila taarifa, na kuyasolve mambo haya kwa hekima zaidi kuliko kukimbilia talaka. Nani aliyewaambia talaka ndiyo suluhisho pekee la matatizo ya ndoa??
 
Awe anamdakisha mkewe fungu lake la macarolite, mapowder na mazagazaga ili aache udokozi.
 
Ukiona mwanamme anauliza chenji ya nyanya, si mwanamme timamu.

Hivi unamwacha mkeo kila siku, unataka hadi hela ya pedi akuombe?
kama mnakula kama kawaida na anasaidia kwao kunashida gani?

Uchoyo wa aina gani huo?
Hivi unadhani unioe uniweke mama wa nyumbani sina hata genge la nyanya, nitaacha kupiga panga niwasaidie kwetu?
Hivi unadhani umenikuta mtu mzima, nimetokea shimoni?
Sina uchungu na wazazi wangu? Niwaone wanalala njaa mie najichana, nitakuw MWEHU WA KARNE.

Tatizo baadhi ya wanamme wana uchoyo wa chakula sana, hii ni aibu ya mwaka na wala si ya kuongea mabele za watu.
Kama chakula tu ni tatizo, kusomesha watoto je?

Mpe mkeo kahela ka matumizi yake binafsi kama utaona anakata panga hela ya nyumbani kwako.

Big up sana kwa huyo dada, ndo maana nasema ukizaa binti umezaa asset hatakuacha ulale njaa, wana akili ya kujiongeza. Mwanamme aah anajali kwake na mkewe tu.
 
Sasa mke wake akipeleka pesa kwa wazazi wake kosa gani.


Mimi ndo ningezidisha kumpenda mke wa namna hio, mana ana wajali wazazi wake.

Afu huyo mwanaume kama ana adabu hata kusema hi issue asinge sema, ange nyamaza tu...mana wale wazee wamempa mtoto wao yani mke, lazima uwafanyie heshima.
 

Nakubaliana na wewe, km kuna mawasiliano mazuri na mwanamke anapata mahitaji yake hawezi kuficha fedha, kubali kataa hatuwezi kuziacha hizi familia mtambuka(extended families) hivyo mnapokuwa katika ndoa ni vema kuangalia na mahitaji ya wanandugu wengine. Jadili talaka siyo suluhisho aangalie kosa liko wapi warekebishe.
 
Ukute analisha mume mwenza. . . . Kaaaazi kweli kweli.
 
Kongosho nimekupenda buuuuuuure bila senti tano,


 

mkuu hao wote wanaonekana kwanza hawaaminiani pili wote wanatamaa ya mkwanja kwa kuwa hilo limetokea basi kama wameachana watajijua wenyewe kwani wakati wanakubaliana hawakukushirikisha..

let them go praaaa.....
 
muulize huyo rafiki yako huwa anawakumbuka ukweni kwake au ndo dada huyo kashaolewa mahari keshatolewa ndo kwao basi tena kama huwa anawapa fungu hapo ndo tatizo lakini kama ndo bahili ni halali yake huyo mwanamama lol.Chezea uchungu wa mzazi:attention:
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…