Tipstipstor
JF-Expert Member
- Nov 29, 2021
- 1,528
- 3,352
Ahlan wa Sahlan
Katika kuzunguka kwangu katika mataifa ya ulaya nimekutana na mfumo huu wa ligi za reserve wengine hupenda kuuita professional development leagues.Ni mfumo wa ligi unaohusisha wachezaji vijana kutoka academies za timu zinazoshiriki ligi kuu za nchi husika,hujumuisha vijana wa academies wasiozidi umri wa miaka 21 pamoja na wachezaji wachache ambao hawapati nafasi /muda wa kucheza katika timu A. Yaani katika reserve team wale wachezaji ambao hawapati game time katika team A au wake ambao wamerejea kutoka katika majeraha, au ambao wamepewa adhabu za kinidhamu na timu husika wanapewa nafasi ya kuja kucheza katika reserve league pamoja na vijana wa academies wasiozidi umri wa miaka 21 na wakiwa katika form nzuri basi kocha wa team A anaweza kuwarejesha kuanza katika team A, au vilevile kocha anaweza kuchagua hawa U21 players kuja kujiunga na timu ya wakubwa.
Ni mfumo mzuri sana ambao hutumiwa na mataifa yaliyoendelea kisoka, sasa hv tunaona wachezaji mfano wa chama langu Simba mfano Akpan,Dejan,Okwa na kapama hawapo ktk machaguzi ya mwalimu Matola ( Mgunda ), sasa badala ya kukaa benchi tu mwezi mzima bila ya kupata game time ni bora wangekuwa wanacheza dakika 90 kwenye hizo reserve league ili kujiweka fiti.
Pia dhumuni kubwa wa hizi reserve /development leagues ni kuibua vipaji vya wachezaji u21 .
Katika kuzunguka kwangu katika mataifa ya ulaya nimekutana na mfumo huu wa ligi za reserve wengine hupenda kuuita professional development leagues.Ni mfumo wa ligi unaohusisha wachezaji vijana kutoka academies za timu zinazoshiriki ligi kuu za nchi husika,hujumuisha vijana wa academies wasiozidi umri wa miaka 21 pamoja na wachezaji wachache ambao hawapati nafasi /muda wa kucheza katika timu A. Yaani katika reserve team wale wachezaji ambao hawapati game time katika team A au wake ambao wamerejea kutoka katika majeraha, au ambao wamepewa adhabu za kinidhamu na timu husika wanapewa nafasi ya kuja kucheza katika reserve league pamoja na vijana wa academies wasiozidi umri wa miaka 21 na wakiwa katika form nzuri basi kocha wa team A anaweza kuwarejesha kuanza katika team A, au vilevile kocha anaweza kuchagua hawa U21 players kuja kujiunga na timu ya wakubwa.
Ni mfumo mzuri sana ambao hutumiwa na mataifa yaliyoendelea kisoka, sasa hv tunaona wachezaji mfano wa chama langu Simba mfano Akpan,Dejan,Okwa na kapama hawapo ktk machaguzi ya mwalimu Matola ( Mgunda ), sasa badala ya kukaa benchi tu mwezi mzima bila ya kupata game time ni bora wangekuwa wanacheza dakika 90 kwenye hizo reserve league ili kujiweka fiti.
Pia dhumuni kubwa wa hizi reserve /development leagues ni kuibua vipaji vya wachezaji u21 .