Uchaguzi 2020 Ushauri Tume ya Taifa ya Uchaguzi

Mbogo nyeusi

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2019
Posts
233
Reaction score
541
Lipo tatizo linalo ichafua Tume kwa kuwaengua baadhi ya wagombea na wengine kunyanganywa fomu zao wakati wa urejeshwaji,

Hayo ni madhila waliyo kutana nayo wagombea wa upinzani pekee,na hili halijatokea kwa bahati mbaya ni makusudi na mipango ilisukwa kwa ustadhi mkubwa toka watendaji wa kata walipoitwa sebuleni na kauli iliyo tolewa ya kwamba"nikuchague Mimi,nikulipe mshahara Mimi umtangaze mpinzani""ooyoooooyooo

Natambua kuwa hao waliokatwa ni kwa matakwa ya Sheria na kwa kuwa imeonekana Kama ni uonevu na unyanyasaji kwa wagombea kunyimwa haki ya kugombea nahisi Tume ya Taifa kuvaa utu na busara kuruhusu yeyote aliyechukua fomu na kuirudisha na wale walio tekwa na kuzuiwa kuchukua fomu, kama hana kosa la jinai wote wasamehewe na wapewe nafasi ya kugombea na Uchaguzi mwingine vyama vitakuwa vimejifunza japo hata Chama tawala nao walikatiwa rufaa kwa kujaza fomu kimakosa lakini hayupo hata mmoja aliyeenguliwa

Busara zilizotumika kwa wagombea wa CCM kwa mfano Gwajima (Gwaji Boy) zitumuke pia kwa vyama vingine, Uchaguzi mwingine watakuwa wamejifunza.

CCM iondoe shaka ushindi ni wao wasiogope kushindana wanatunyima uhondo wa minyukano majukwaani na pia ushindi wa mezani siyo mtamu haukupi ladha ya kujua mapenzi yako kwa wananchi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…