USHAURI : Ukiacha kilimo, naweza kuwekeza kwenye nini kwa hii 2 Mil ?

Hivi punde

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2017
Posts
2,554
Reaction score
8,587
Habarini wakuu.

Nimepambana nimepata mahali 2 mil. Nataka niwekeze walau niwe napata chochote. Naishi Moshi Mjini.

Kuhusu kilimo hapana!

Naombeni ushauri mapema wakuu maana hela haikai na matatizo nayo ni mengi sana.

Wasalaam!
 
Mkuu sasa hivi hakuna sehemu nyepesi kila kona pamekaza.

Mimi naamini biashara ngumu ndio yenye faida
 
Labda biashara ya kukopesha laki 1 au 2 kwa wafanyakazi tu. Inaweza kukulipa
 
Nipe mm hiyo hela niwekeze kwenye forex kila mwisho wa mwezi ntakuwa nakupa laki 5 kama faida
 
Wekeza kwenye kubet naona raia wanatoka sana kwa kubet. Na frankly speaking, kizazi hiki kinabet mpaka jinsi (sex) zao.
Ni mwendo wa tatu mzuka tu Biko biiiko biiikooooo hadi Mitihani ya nekta la 7 na LA 4 ni kubet tu
Nawe bet tu mkuu!!!!
 
Kama una mtu anaendaga China ( Unayemuamini nasisitiza anayeaminika ) mpe milioni akufuatie Smart Watch zile za watoto zile zenye GPS pics 50 tu komaa umalize zote alafu utanipunguzia TIGO Pesa.

Hiyo milioni nyingine izuie kwanza 🤣 Usitie hela yako yote uliyonayo kwenye biashara inayoanza.
 
Kiukweli hyo hela kwa sasa biashara labda ndog ndog tu ambazo utapata hela ya kula huku ukikomaa sura mtaani.....maana ukichukua frem tu kuna utitiri wa kodi ni hatarii....ni bora utafte data fresh ujilipue scandnavian countries naskia panalipa kinoma ukifanya kazi hata za kubeba maboksi..ndan ya mwaka mmoja kama una malengo unanake around 100 mil za kbongo hapo ndo unarud bongo kuwekeza sasa.....lakn kwa sasa hyo hela bora ukalime kilimo cha mpunga itakutoa mkuu....
 
Nipe mm hiyo hela niwekeze kwenye forex kila mwisho wa mwezi ntakuwa nakupa laki 5 kama faida
wazee wa kubet forex... mna maneno sanaaaaaaa na kutonyeshaga balance fake...

cha ajabu anayekuonesha balance inasoma GBP 3800 kesho anakupiga kizinga hadi unajiuliza ww sijana umenionyesha balance yako ya forex inasoma GBP 3800
 
Iyo hela labda wakopeshe wajasiliamali tatizo we unaionea huruma
 
wazee wa kubet forex... mna maneno sanaaaaaaa na kutonyeshaga balance fake...

cha ajabu anayekuonesha balance inasoma GBP 3800 kesho anakupiga kizinga hadi unajiuliza ww sijana umenionyesha balance yako ya forex inasoma GBP 3800
Kama hujui kitu, ni bora kukaa kimya tu
 
Habarini wakuu.

Nimepambana nimepata mahali 2 mil. Nataka niwekeze walau niwe napata chochote. Naishi Moshi Mjini.

Kuhusu kilimo hapana!

Naombeni ushauri mapema wakuu maana hela haikai na matatizo nayo ni mengi sana.

Wasalaam!
BIKO..kule mshiko nje nje
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…