USHAURI: Ukomo wa Utumishi wa Umma uwe miaka 10

USHAURI: Ukomo wa Utumishi wa Umma uwe miaka 10

Smartgeneration

New Member
Joined
Jul 18, 2022
Posts
2
Reaction score
5
Utumishi wa uwe mwisho miaka 10

Habari za majukumu wana jamii forum, andiko langu la leo ni juu ya ukomo wa utumishi wa umma, kwa mtazamo wangu ni bora zaidi ukomo wa kutumikia serikali upunguzwe hadi kifikia miaka 10, kwa maana ya kwamba serikali itengeneze utaratibu wa wahitimu wa vyuo kuajiliwa mapema pale tu wanapo hitimu masomo yao ya ngazi za juu, hivyo basi mifumo rafiki ya utambuzi wa hitimu iwe ni ya kusajiliwa kwenye mfumo mmoja pale tu wanapohitimu hii ni kwa kuzingatia mwaka wa kuhitimi, hii itasaidia watu kuingia mapema katika ajira za serikali wakiwa na umri mdogo matharani nikiajiliwa na miaka 21 nitastaafu nikiwa na miaka 31, hapa nitakua na nguvu za kutosha za kuweza kumudu mambo mengine kama kuweza kusoma fani zingine, kujiajili kwa kupitia marupurupu yangu ya serikalini.

Lengo kuu la kuweza kufanya hivi ni kiruhusu nafasi ya watu wengi kupata nafasi ya kuajiliwa serikalini ivyo kupunguza hadha ya ukosefu wa ajira kwa muda mrefu, pia kuweza kuongeza ufanisi katika utendaji wa kazi, vile vile itakuza uchumi wa mtu mmoja mmoja katika jamii.

Vile vile hii italeta mtazamo chanya kwa wastaafu kwa kuwa hivi ilivyo sasa watu wamekua wakistaafu wwkiwa na umri mkubwa na kupata kiasi kikubwa cha fedha na kuwa mzigo kwa familia na mstaafu, kwasababu mstaafu anakua amechoka kiakili hivyo anakuwa na mzigo mkubwa wa kumiliki fedha nyingi bila ya kujua namna ya kuzizalisha katika shughuli mbalimbali, hii ni tofauti na mtu akistaafu na umri mdogo, ukistaafu na umri mdogo unakua chachu ya maendereo katika jamii kwasababu unakua umevuna mari kwa muda mfupi na akili ya kuweza kuziongoza fedha za kustaafu inakua kubwa.

Vile vile mtu akistaafu akiwa na umri mdogo anaweza kujiendereza kimasomo katika nyanja nyingine kama ufundi, siasa, biashara na kadharika, na hapa pia ndipo CV ya mtu itakua na mashiko mapana, kwamba CV itaonesha nilishaajiliwa Serikalini katika nyanja fulani na hivyo itaongeza thamani katika sekta binafsi za nje na ndani pia.

Asanteni

Nawasilisha
 
hujui serikali inavyoendeshwa! unafkiri JKT ya kujitolea hiyo kila mkija mnalima mahindi na kumwagilia mboga
 
Kabisa kama Wabunge upewa 1500,000,000/ mapema unasepa kwa amani.
 
10 hapana Kaka at least ungenambia 20 kweli ningeweza kuafiki maana mafao yanaweza kufika hata M.30 japo Bado ndogo Sana biashara inafanya.
 
Kwahiyo hakuta kuwa na seniors wote watakua juniors kwenye kazi..hujui muda wa kustaafu madaktari na maprofesa ni miaka 70..na bado huongezewa mikataba ya kazi.

#MaendeleoHayanaChama
 
Pole, endelea kujituma kwa kujiajili utatoboa tu. Ajira rami inataka watu watakaofanyakazi kwa muda mrefu il kupata tija ya uzoefu wao kiutumishi. Ndio maana hata mwajiliwa mgonjwa wa muda aondolewi kirahisi kazini mpaka ikathibitishwa na Jopo la madaktari wabobevu kuwa hawezi kabisa kuendelea na kazi. Hizo ni sharia za ILO ambapo nyinyi ni wanachama
 
Unajua maana ya mtu kustaafu kazi au unabwabwaja tu, ukistaafu kazi na umri mdogo miaka hiyo mingine kabla hujafikia uzee utakuwa unafanya nini.......
 
Bora hata ungesena umri wa kustaafu upunguzwe kutoka miaka 60, mpaka miaka 55 kwa lazima! Na miaka kutoka miaka 55 kwa hiyari, mpaka miaka 50!

Hilo wazo lako la kustaafu baada ya miaka 10, kiukweli halitekelezeki. Na kama ndiyo uko mtaani unasubiria ajira, ni bora ukabadili tu mtazamo wako kwa kujiajiri.
 
Hii mimi nakuunga mkono,hata kama sio kumi basi 15,
Watumishi wa uma wanajisahau sana
Nimewahi kufanya shirika moja kwa miaka kama minne na kuna watu niliwakuta wana zaid ya miaka 20 lakini output yao ni sifuri(aingie kazini ama asiingia hana matokeo yoyoye)
 
Unajua maana ya mtu kustaafu kazi au unabwabwaja tu, ukistaafu kazi na umri mdogo miaka hiyo mingine kabla hujafikia uzee utakuwa unafanya nini.......

Kajipambanie,hukuzaliwa ili uajiriwe tu.
Kama ni muajiriwa fikiria pia na njia nyingine ya kupata kipato ila usimjibu mleta mada kwa jazba kiasi hicho
 
Kajipambanie,hukuzaliwa ili uajiriwe tu.
Kama ni muajiriwa fikiria pia na njia nyingine ya kupata kipato ila usimjibu mleta mada kwa jazba kiasi hicho
Kwa hiyo ukifanya kazi nyingine unakuwa umestaafu au bado unakuwa kazini...........unajua maana ya kustaafu?
 
Ni wazo zuri sana umetoa. Naomba serikali walifanyie kazi. Wazo mbadala na hilo kwa Sasa watoe japo redundancy ili wengine tuliochoka/wadhaifu na kazi tupungue na wenye nguvu waajiriwe. Watulipe mpaka happy tulipofikia ila bila kikokotoo. Ewe serikali pendwa sikia ombi letu
 
Back
Top Bottom