Ushauri wa biashara ya kava za simu

Panua soko makava ambayo yanapitwa kimuonekano huwa yanasambazwa sehem za mbali asikudanganye mtu kava iliyo pitwa fashion Dar kule Maswa bado ni sukari
Swala ni kuwa na mtandao tu una mpushia mtu kwa jumla
Nimeanza from scratch mkuu kamtaji ka maandazi
 
Panua soko makava ambayo yanapitwa kimuonekano huwa yanasambazwa sehem za mbali asikudanganye mtu kava iliyo pitwa fashion Dar kule Maswa bado ni sukari
Swala ni kuwa na mtandao tu una mpushia mtu kwa jumla
Hili linaweza kuwa ni suluhisho.
Dawa ni kutafuta connection na kuyasukuma kwa bei ya hasara tu.
Heri nusu shari.
 
Wanunuzi wa kava kwenda mikoani huwa wanafata kava hapa Dar wao pia huchukulia mzigo unapochilukulia wewe jaribu kutumia akili yako ya kibiashara kuwashawishi
 
Dah una changamoto maana kuna kina mimi tusioweza kutumia simu ikiwa na kava ila chaji earpods lazima tuwe nazo kwahyo soma ramani vizuri

Yangu haina cover wala screen protector toka nmenunua na ni 2 yrs now[emoji91][emoji91][emoji91][emoji119]
 
Hivi duka la simu midrange linaweza hitaji mtaji kiasi gani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…