ushauri wa bure kwa Jide juu ya redio ya watu

ushauri wa bure kwa Jide juu ya redio ya watu

naomba kujua jamani, kwani luge na jide walishalala pamoja huko south africa?? kilitokea nini hapo?...
 
Jide angetulizana na kupambana na biashara zake!aachane na mipasho!wenzake hawamjibu sio kwamba hawawezi wanamshangaa asivyo na shukrani hasa kwa kaka yake Joseph!
 
Mnayaendeleza wengine,sidhani kama JD kajibishana tena kwenye JF,hayo ni yenu msio na dogo.
 
Let me get this clear.

JD kawa mtumwa miaka kibao chini ya Clouds FM. Wamemtumia na yeye kwa kiasi fulani kawatumia kupanda.

Kapanda chati mpaka kaweza kusimama mwenyewe.

Kaamua kusema mabaya aliyoyaona Clouds FM.

Mnamwambia asiseme kwa sababu tu "sinyee kambi"?

Kwanza huu mfano ni mbovu, kwa sababu mpaka sasa hivi JD - as much as I think she is hyped up and bloated- hayumo kwenye kambi, kashatoka.

Pili Clouds is not exactly a home, it is an exploitative business. And the fact that people who were so close it's management like JD are going against it should tell you something.

Tatu, nchi yetu ina uhuru wa kujieleza, kwa nini mnataka kumnyima JD uhuru wake wa kujieleza?
 
Huu ni ujinga wa ngazi ya shahada yani hata kama mtu alikusaidia basi akunyanyase na usiseme uendelee kunyamaza tuu kama zezeta? Huu uoga mnamfundisha nani? Clouds ina maana hawakunufaika na jyde? Wao ni nani? Kuna radio ngapi nchini mpaka muwaofie? Mnajua hao wasanii wanalipwa sh ngapi kwenye matamasha ya clods?

Ukweli lazima usemwe hata kama ni mchungu na kwa hili na msifu jyde? Ukitaka kujua clouds wana matatizo hakuna sababu za msingi alizotoa ben pol wala linah zilizo wazui kuto kuhudhuria show ya jyde!

Hivi mnajua na chid benz nae kalalamika nyimbo zake kutopigwa? Hivi kwa nini mnaihabudu hii radio@ wao wamekuwa nani kumshusha mtu?

Na wahakikishi jyde hawezi kuyumba wala kuyumbishwa na clouds!

Watanzania tunapenda kulambana miguu sana!ujinga wa ngazi ya degree!

Lady jaydee shika ulipo shika wala usiyumbishwe na mtu!
 
Lad Jay Dee, The Pumpkin of the Old Homestead MUST NOT BE UPROOTED! maana halisi ya hiyo proverb ni USINYEE KAMBI. waswahili wanasema usisahau ulikotoka na aliyekutoa..

wanadamu tuna tabia ya kujisahau sana, haswa tupatapo mafanikio katika nyanja fulani zinazotuhusu. Kujisahau ni ugonjwa mkubwa tupatao sisi wanadamu. Lakini lazima tukubali kujisahau sio kuzuri, ebu jaribu kuvuta picha, hata tu ya kufikirika, vipi asingejitokeza yule mtu katika njia ya maisha yako, je leo ungekuwa hapo? ungekuwa ulivyo?

kamwe usijisahau kiasi cha kumtusi aliyekusimamisha, aliyekutoa katika aibu, aliyekufanya leo utembee na uonekane ulivyo...

Jide, redio ya watu ndio iliyokutoa, ndio waliokutambulisha katika anga ya muziki. maisha yako wewe ni matokeo ya moja kwa moja ya redio ya watu, leo ukitusi na kukebehi kiasi hicho ni kwamba hutafuti kingine zaidi ya laana.. wewe umeonekana kwa sababu ya redio ya watu, wale ndio waliokusimamisha, usisahau ulikotoka. Mumeo, kafundishwa ujanja na redio ya watu, kipaji chake kilionyeshwa na redio ya watu, ni redio ya watu ndio ilimlea na kumkuza. Biashara yenu, yaani Nyumbani Lounge, ni redio ya watu iliyotambulisha biashara yako, kumbuka, kumbuka fresh..... Leo mbona mnajisahau sana..

ushauri wangu: The Pumpkin of the Old Homestead MUST NOT BE UPROOTED!
 
Guys,

Yaani kwavile mawingu wamemtoa JD hivyo wanakibali cha kumfanya watakavyo?
Go JD! nitakuunga mkono kwasababu moja tu,kutetea maslahi ya muziki Tanzania hatutaki ya Tanesco na umeme ktk muziki!
Go JD!
 
Back
Top Bottom