Uchaguzi 2020 Ushauri wa bure kwa John Mnyika kuhusu mzabuni wa NEC

Uchaguzi 2020 Ushauri wa bure kwa John Mnyika kuhusu mzabuni wa NEC

Singo Batan

JF-Expert Member
Joined
Apr 24, 2020
Posts
295
Reaction score
198
Nimefuatilia Press ya Katibu Mkuu wa CHADEMA Bw. John John Mnyika, akiitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuhusisha vyama vya siasa juu ya manunuzi ya vifaa vyote vya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.

Mnyika anakiri kwamba Tume imeitisha zabuni ya manunuzi ya vifaa vya Uchaguzi zikiwemo Karatasi za kupiga Kura. Kwa Taarifa hiyo inathibitisha NEC imefuata taratibu za manunuzi ya Umma kisheria, Na kwa maana nyingine Mzabuni aliye shinda tenda ndiye aliyepewa kazi. Lakini Mnyika ameonesha wasiwasi juu ya Mzabuni wa Manunuzi ya karatasi tu za kupigia Kura (ballot papers) kuwa "kwa vyanzo vyao CHADEMA" Kampuni inayochapisha Karatasi iko Dar es salaam.

Kwa maoni yangu naona Bw. Mnyika anasahau kwamba kabla hajaifanyia uchunguzi NEC kupitia "vyanzo vyao" , yeye kama Kiongozi na mtendaji Mkuu wa Chama alitakiwa kufika NEC na apate Taarifa kuhusu manunuzi ya Vifaa mbali mbali yalivyofanywa kama kuna haja hiyo na (kwa basis ile ile) kwamba ni Manunuzi ya UMMA na kwa namna yoyote Taarifa zake zipo NEC sio kwenye "Vyanzo vyao"

Ikiwa Kampuni imeshinda zabuni na kupewa tenda ubaya uko wapi kiasi cha kutiliwa shaka na Mtu Mkubwa kama yeye?, Karatasi za kura zina maajabu gani yanayoweza kutiliwa shaka?, Ni nini umaalum wa kuona Afrika kusini wanaweza kuwa na sifa za ziada kuliko Jamana (Kama kweli Jamana ndio wametengeneza hizo ballot papers?)

Kama Chadema ambayo ni Taasisi, haijawahi kuingiliwa katika maamuzi ya manunuzi ya Vifaa vyake vya kazi na Taasisi nyingine yoyote, Je, Ni sawa kuishurutisha NEC kufuata matakwa ya CHADEMA?

Bw. Mnyika haoni kwamba kufanya hivyo ni kuingilia Uhuru wa Tume kama ambavyo anaaminisha Umma kwamba Tume hii haipo huru?, Unasisitizaje mabadiliko kama wewe hutaki kuwa Mfano?

USHAURI
Katika kutafuta Mafanikio kisiasa na hata kushika Dola ni vyema CHADEMA kikajikita zaidi kuonesha ubora wa sera zake kwa wananchi hasa katika siku hizi zilizobaki kuliko kila wakati kutafuta Migogoro na Migongano isiyo ya lazima na kuweka kila "kinachohisiwa hakipo sawa" mitandaoni au kwenye vyombo vya habari bila ya kufuata utaratibu wa kisheria ili kujiridhisha na jambo fulani na ikibidi kama haliko sawa kulizuia.
 
Yaani unataka NEC ifanye utopolo halafu tunyamaze? Eti Mnyika aende ofisi za tume.

Kwanini wao hawakwenda wao ofisi za CHADEMA kuwaambia kuwa wamebadilisha mzabuni?

Mwaka huu CHADEMA imewashika pabaya. Huku Robert Amsterdam, huku Lissu. Kule Mnyika huku Kigogo2014. Mtanyooka mwaka huu.
 
Mkuu, umeanzisha Uzi kumshauri nani? Chama kinajua kila kitu, hujui ktk chama hicho kuna nguli was sheria na diplomasia? Basi vumilia kidogo majibu yao, usipokuwa makini utahama jf!
Nguli wa sheria anasema uongo na kufungiwa kampeni?
Huyo ni boya tu,

Hebu leteni mafuriko ya leo tuone ukame wa watu waliokuwa na hamu na mgombea
Nimeingia youtube mida yote sioni kitu nini shida?

Au warusha pivha nao bado wako jela ya NEC?

Tunataka picha hatutaki uinga ujinga, mbona za kanza ya ziwa mlikuwa mnawahisha?

Za huko nyumbani kwake, kwa nini mnachelewa kutoa?
 
Nguli wa sheria anasema uongo na kufungiwa kampeni?
Huyo ni boya tu,
Hebu leteni mafuriko ya leo tuone ukame wa watu waliokuwa na hamu na mgombea
Nimeingia youtube mida yote sioni kitu nini shida?
Au warusha pivha nao bado wako jela ya NEC?
Tunataka picha hatutaki uinga ujinga, mbona za kanza ya ziwa mlikuwa mnawahisha?
Za huko nyumbani kwake, kwa nini mnachelewa kutoa?
We ndo unaamka sa hizi watu washaona picha za Dodoma na ikungi ni balaa tupu,mpaka yehodaya akasema hakuna kijiji chenye watu wengi namna hiyo.

Au ndo unatoka kazini kwa wahindi sa hizi.
 
We ndo unaamka sa hizi watu washaona picha za Dodoma na ikungi ni balaa tupu,mpaka yehodaya akasema hakuna kijiji chenye watu wengi namna hiyo.

Au ndo unatoka kazini kwa wahindi sa hizi.
Dodoma nimeona ila ni kidogo tu ila ikungi mnaficha au huko hakuna hata maandamano,
Mbona kanda ya ziwa tuliona kwa haraka na media zenu mnazofunga sehemu ya comment bado zina kigugumizi?
 
CHADEMA nawaweka kwenye kundi either la wajinga au matapeli.

Kwanza wanakiri zabuni ilitangazwa halafu wanaenda kulalamika kwenye vyombo vya habari, kama kuna shida ina maana hawajui pa kupeleka malalamiko yao au hizo ndio strategies waliopewa na Amstadam 😂😂😂
 
CHADEMA nawaweka kwenye kundi either la wajinga au matapeli.

Kwanza wanakiri zabuni ilitangazwa halafu wanaenda kulalamika kwenye vyombo vya habari, kama kuna shida ina maana hawajui pa kupeleka malalamiko yao au hizo ndio strategies waliopewa na Amstadam 😂😂😂
CCM mama foleni chakula.jpg

Asante mama D, nakuona unasubiri kubugia ubwabwa...​
 
Wagombea wa CCM huwa wanatuambia tuache Kutegemea kuajiriwa na serikali, tujitegemee na tujiajiri wenyewe!! Wakati wao wanatuomba kura Ili tuwape ajira waajiriwe na wananchi.

TUSAIDIANE MAWAZO HAPA VIJANA WENZANGU, HAWA WATU ZIMO KWELI VICHWANI MWAO ?
 
Makini sana kiongozi, hawa CHADEMA kiufupi wamepwaya sana. Ni hopeless kabisa, samahani kwa hii lughasina namna. Wanadandia hoja hovyo.

Kifo cha nyani miti yote huteleza
 
Lissu hatajenga barabara, shule wala zahanati maana hayo ni maendeleo ya vitu
Atakachokifanya ni kuwafukuza wamachinga barabarani maana hayo ndiyo maendeleo ya watu
 
Back
Top Bottom