USHAURI WA KIZALENDO KWA SIMBA S.C

USHAURI WA KIZALENDO KWA SIMBA S.C

Mhimili uliojichimbia

Senior Member
Joined
Jul 2, 2017
Posts
172
Reaction score
191
Kutokana na taarifa ya kuondoka kwa mshambuliaji wa kimataifa wa club ya Simba, Emmanuel Arnold Okwi nikiwa mtanzania mzalendo na mwenye kuitakia mafanikio timu pekee inayowakilisha Jumuiya ya Afrika Mashariki kwenye kombe la mabingwa barani Afrika, naishauri kamati ya ufundi ya timu ya simba kuanza mkakati wa kumnasa mshambuliaji mahiri wa timu ya Nkana F.C Walter Bwalya kwenye dirisha dogo la usajili la CAF, hii itasaidia kuziba pengo hilo.
Bwalya ni mchezaji mwenye uwezo mzuri na uzoefu wa kutosha kuitumiakia Simba inayokabiliana na mechi ngumu za CAF.
 
Kutokana na taarifa ya kuondoka kwa mshambuliaji wa kimataifa wa club ya Simba, Emmanuel Arnold Okwi nikiwa mtanzania mzalendo na mwenye kuitakia mafanikio timu pekee inayowakilisha Jumuiya ya Afrika Mashariki kwenye kombe la mabingwa barani Afrika, naishauri kamati ya ufundi ya timu ya simba kuanza mkakati wa kumnasa mshambuliaji mahiri wa timu ya Nkana F.C Walter Bwalya kwenye dirisha dogo la usajili la CAF, hii itasaidia kuziba pengo hilo.
Bwalya ni mchezaji mwenye uwezo mzuri na uzoefu wa kutosha kuitumiakia Simba inayokabiliana na mechi ngumu za CAF.
Habari za kuondoka Okwi ni habari ambazo sio rasmi.
Lakini cha msingi ni kwamba utafanyika usajili wa kuimarisha timu pamoja na kurudi kwa Kapombe ambaye ataanza mazoezi mepesi hivi karibuni.
 
Mtoa habari katoa habari kwa kukurupuka bila kuzingatia nidhamu ya utoaji habari yenyewe. Swala la okwi sio kwamba ameondoka au anatarakia kuondoka hapana!! Ila ni kwamba timu ya Kaiser chiefs wanahitaji huduma yake na mazungumzo kati ya timu mbili yaendelea.
 
Mtoa habari katoa habari kwa kukurupuka bila kuzingatia nidhamu ya utoaji habari yenyewe. Swala la okwi sio kwamba ameondoka au anatarakia kuondoka hapana!! Ila ni kwamba timu ya Kaiser chiefs wanahitaji huduma yake na mazungumzo kati ya timu mbili yaendelea.
Hivi kaiser chiefs bado wanamtaka tu? Walimtaka 2011 tena 2014 na 2018 tena? Nilifikiri wanahitaji vijana zaidi maana sasa hivi wameachwa kabisa na mamelod sundown ma orlando pirates! Kama uwekezaji ni wa wachezaji waliowataka toka 2011 basi wana haki ya kuburuzwa.
 
Kutokana na taarifa ya kuondoka kwa mshambuliaji wa kimataifa wa club ya Simba, Emmanuel Arnold Okwi nikiwa mtanzania mzalendo na mwenye kuitakia mafanikio timu pekee inayowakilisha Jumuiya ya Afrika Mashariki kwenye kombe la mabingwa barani Afrika, naishauri kamati ya ufundi ya timu ya simba kuanza mkakati wa kumnasa mshambuliaji mahiri wa timu ya Nkana F.C Walter Bwalya kwenye dirisha dogo la usajili la CAF, hii itasaidia kuziba pengo hilo.
Bwalya ni mchezaji mwenye uwezo mzuri na uzoefu wa kutosha kuitumiakia Simba inayokabiliana na mechi ngumu za CAF.
mkuu sheria zitamruhusu acheze kweli....lkn m naona ni wakati wa kumpa mechi za ligi za kutosha yule rashid juma na salamba (ili wawe fiti zaidi)....maana naona kama mh. bocco pumzi imekata...
 
Gabachori wa mikia ameshindwa kumshawishi maana Chiefs wanaenda kumpa mshahara $15,000 kwa mwezi..
 
Habari za kuondoka kwa Okwi ni za kuuzia magazeti tu. Na suala la kumsajili Bwalya halitakuwa na tija maana jina lake liko CAF na ameshatumika kwenye michuano husika. Lete chai nyingine!
 
Hata kama Okwi bado tunahitaji striker hatari,kama Bwalya anachukulika basi anaswe
 
Hivi kaiser chiefs bado wanamtaka tu? Walimtaka 2011 tena 2014 na 2018 tena? Nilifikiri wanahitaji vijana zaidi maana sasa hivi wameachwa kabisa na mamelod sundown ma orlando pirates! Kama uwekezaji ni wa wachezaji waliowataka toka 2011 basi wana haki ya kuburuzwa.
Mkuu,unakumbuka Haruna Moshi 'Boban' mlianza kumtaka tangu lini?
 
mkuu sheria zitamruhusu acheze kweli....lkn m naona ni wakati wa kumpa mechi za ligi za kutosha yule rashid juma na salamba (ili wawe fiti zaidi)....maana naona kama mh. bocco pumzi imekata...
Simba ilifanya jambo sahihi sana kumsajili Adam Salamba, pia Rashid Juma kama akizingatia maelekezo ya makocha na akiendelea Kuwa na nidhamu atakuja kuwa mchezaji tishio kabisa hapa nchini, ana uwezo mkubwa katika umri wake mdogo.
 
  • Thanks
Reactions: Tui
mkuu sheria zitamruhusu acheze kweli....lkn m naona ni wakati wa kumpa mechi za ligi za kutosha yule rashid juma na salamba (ili wawe fiti zaidi)....maana naona kama mh. bocco pumzi imekata...
Bwalya hawezi kucheza tena kwenye CAF Champions League ya mwaka huu akiwa Simba, maana kashacheza kupitia Nkana
 
Bwalya hawezi kucheza tena kwenye CAF Champions League ya mwaka huu akiwa Simba, maana kashacheza kupitia Nkana
Labda sheria zibadilke lakini inawezekana,maana mwaka 2011 tunamtoa TP Mazembe ,Mazembe walikua wamemsajiri Mbwana Ally Samatta wakijua wameitoa Simba na acheze kwa ajili ya hatua za mbele za Ligi ya mabingwa,lakini Haki ilivyotendeka kwakua walichezesha mchezaji mamluki na kufanikiwa kuwatoa tuliwaomba Samatta atusaidie kwakua wao tushawatoa walitukatalia kipindi kile.sheria za CAF sio sawa na UEFA ndomana mkiingia makundi Kuna nafasi ya kusajiri mchezaji yeyote ila kama tuu timu yenu ilipeleka idadi ya wachezaji chini ya 30...na room ya kusajiri kwa Simba ipo kwani walikua wamepeleka idadi ya wachezaji 26 tuu.
 
Labda sheria zibadilke lakini inawezekana,maana mwaka 2011 tunamtoa TP Mazembe ,Mazembe walikua wamemsajiri Mbwana Ally Samatta wakijua wameitoa Simba na acheze kwa ajili ya hatua za mbele za Ligi ya mabingwa,lakini Haki ilivyotendeka kwakua walichezesha mchezaji mamluki na kufanikiwa kuwatoa tuliwaomba Samatta atusaidie kwakua wao tushawatoa walitukatalia kipindi kile.sheria za CAF sio sawa na UEFA ndomana mkiingia makundi Kuna nafasi ya kusajiri mchezaji yeyote ila kama tuu timu yenu ilipeleka idadi ya wachezaji chini ya 30...na room ya kusajiri kwa Simba ipo kwani walikua wamepeleka idadi ya wachezaji 26 tuu.
Ohooo sawa mkuu ngoja nitaendelea kufuatilia zaidi na nitaleta mresho
 
Back
Top Bottom