Gaijin
JF-Expert Member
- Aug 21, 2007
- 11,812
- 5,298
inawezekana wanawake wanaopigania haki za wanawake
hawajaona jinsi lugha inavyowarudisha nyuma,
misamiati ya kuolewa na kuachwa inawaathiri zaidi kuliko tunavyofikiri...
Kubadili lugha ni ngumu mno japo kuwa watu wanajaribu.Siku hizi kuna matumizi makubwa zaidi ya 'kuoana' au 'kutalikiana' lakini matumizi yake yanabaki ni panapozungumzwa kiujumla tu. Linapokuja suala la mmoja mmoja basi mwanamke hawezi kusema 'nimemuoa' kwa vile inaleta picha hasi kwa mwanamme
Utasikia "Nae yule kaoa au kaolewa?" ikimaanisha kuwa jamii imegawa majukumu ya muoaji na muiolewaji, na kabla hatujabadili hilo sidhani kama tutaweza kubadili maneno