Ushauri: Wabunge wamchague Spika asiyetokana na chama

Ushauri: Wabunge wamchague Spika asiyetokana na chama

Kutokana na namna ambavyo imedhihirika kwamba sasa Spika hawezi kuwa na uhuru wa kuruhusu mijadala yenye afya kwa watanzania ndani ya bunge kwa hofu ya "kushughulikiwa" na chama (kwa vyama vyote) sasa ni muda muafaka kwa wabunge hasa wa CCM walio wengi bungeni kumpigia kura ya Ndiyo mgombea wa kiti cha Spika asiye na chama.

Wakiweza hili litakuwa na faida kubwa sana kwa taifa pia kwa wabunge wenyewe maana nao pia watakuwa huru kuishauri na kuisimamia serikali.

Wito wangu kwa wabunge wote wanaopigania uhuru wa mhimili huu wa bunge na wale wenye uwezo wa kuliongoza bunge ambao si wabunge njia pekee iliyobaki ni hiyo, chonde chonde tuitumie nafasi hii vizuri tutakuwa tumepiga hatua nzuri kuelekea kupata katiba mpya.
Sio kwa bunge hili Mkuu lazima wampitishe kijani mwenzao
 
Sasa si mpaka hao wenye wagombea wenye sifa wajitokeze kwanza?
 
Ndiyo Mtanzania yoyote mwenye sifa ya kuwa Mbunge (umri, uraia, elimu) anaruhusiwa kugombea Uspika bila Chama na Wabunge wote (hata wa CCM) watamchagia
Kifungu chakl 84(1) kimalizie panaposema au mwenye sifa za kuwa Mbunge
Kifungu 84(9)
Mtu yeyote ambaye sii Mbunge atakayechaguliwa kuwa Spika atatakiwa kabla ya kuanzja kutekeleza ataapisha katika Bunge kiapo Cha uaminufu (maana yangu NI kabla ya Cha Uspika
fomu zinapatikana kwa Katibu Bunge hata CCM watapewa / kununua tafsiri yangu) ninayo majina ya wagombea binafsi waliopambana na Maspika
Sasa mleta mada anamaanisha spika asie na chama ndio apigiwe kura ndo maana nikamuuliza hiyo katiba inasema hivo???spika asie na chama???rejea uzi wake hapo juu soma vizuri utamuelewa
 
Kutokana na namna ambavyo imedhihirika kwamba sasa Spika hawezi kuwa na uhuru wa kuruhusu mijadala yenye afya kwa watanzania ndani ya bunge kwa hofu ya "kushughulikiwa" na chama (kwa vyama vyote) sasa ni muda muafaka kwa wabunge hasa wa CCM walio wengi bungeni kumpigia kura ya Ndiyo mgombea wa kiti cha Spika asiye na chama.

Wakiweza hili litakuwa na faida kubwa sana kwa taifa pia kwa wabunge wenyewe maana nao pia watakuwa huru kuishauri na kuisimamia serikali.

Wito wangu kwa wabunge wote wanaopigania uhuru wa mhimili huu wa bunge na wale wenye uwezo wa kuliongoza bunge ambao si wabunge njia pekee iliyobaki ni hiyo, chonde chonde tuitumie nafasi hii vizuri tutakuwa tumepiga hatua nzuri kuelekea kupata katiba mpya.
Katiba inaruhusu?
 
Siyo lazima upendekezwe na chama. Upo utaratibu wa mtu kugombea kiti cha Spika hata kama si mwanachama wa chama chochote na wala haitahitajika kudhaminiwa na chama ili mradi tu anazo sifa za kuwa mbunge ambazo zipo katika katiba ibara ya 67(1) isipokuwa (b)

Jaribu kuwa practical mkuu. Duniani kote Siasa ziko hivyo. Chama kinajilinda. Sasa wewe utoke nje ya chama nani atakuchagua. Hao wabunge wako pale na Ni wanasiasa.
 
Ndiyo Mtanzania yoyote mwenye sifa ya kuwa Mbunge (umri, uraia, elimu) anaruhusiwa kugombea Uspika bila Chama na Wabunge wote (hata wa CCM) watamchagia
Kifungu chakl 84(1) kimalizie panaposema au mwenye sifa za kuwa Mbunge
Kifungu 84(9)
Mtu yeyote ambaye sii Mbunge atakayechaguliwa kuwa Spika atatakiwa kabla ya kuanzja kutekeleza ataapisha katika Bunge kiapo Cha uaminufu (maana yangu NI kabla ya Cha Uspika
fomu zinapatikana kwa Katibu Bunge hata CCM watapewa / kununua tafsiri yangu) ninayo majina ya wagombea binafsi waliopambana na Maspika
Lakini hiyo katiba haijawahi fuatwa tangu tupate uhuru

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lakini hiyo katiba haijawahi fuatwa tangu tupate uhuru

Sent using Jamii Forums mobile app
Screenshot_20220109-180241.pngScreenshot_20220109-180219.pngKatiba yetu ya 1977 kifungu 84(9) kimetaja mgombea huyo binafsi kuwa ataapishwa kuwa Mbunge ndipo kiapo Cha Uspika
cc Mshana Jr
 
CCM itaweka mapandikizi tupu kama ilivyo mahakamani, tume ya uchaguzi na polisi
CCM kwa sasa ni laana kwa nchi. Ipo zaidi kwaajili ya uharibifu kuliko mema.

CCM ndiyo kikwazo kikubwa kwa mifumo bora uongozi nchini. Bila ya CCM kuondoka madarakani, kamwe nchi hii hatutakuja kuwa na mifumo bora ya kiutawala. Hakuna mahali CCM inafanya kwa dhamira njema zaidi ya kuhakijisha inabakia madarakani kwa njia zozote zile hata kama ni za kishetani.

Inaangilia mifumo ya kimahakama, bungeni, jeshini, polisi, TISS, ofisi ya CCG, DPP - kila mahali inachafua.
 
Kutokana na namna ambavyo imedhihirika kwamba sasa Spika hawezi kuwa na uhuru wa kuruhusu mijadala yenye afya kwa watanzania ndani ya bunge kwa hofu ya "kushughulikiwa" na chama (kwa vyama vyote) sasa ni muda muafaka kwa wabunge hasa wa CCM walio wengi bungeni kumpigia kura ya Ndiyo mgombea wa kiti cha Spika asiye na chama.

Wakiweza hili litakuwa na faida kubwa sana kwa taifa pia kwa wabunge wenyewe maana nao pia watakuwa huru kuishauri na kuisimamia serikali.

Wito wangu kwa wabunge wote wanaopigania uhuru wa mhimili huu wa bunge na wale wenye uwezo wa kuliongoza bunge ambao si wabunge njia pekee iliyobaki ni hiyo, chonde chonde tuitumie nafasi hii vizuri tutakuwa tumepiga hatua nzuri kuelekea kupata katiba mpya.
Kumbukeni Bunge letu limejaa wabunge wa hovyo wasiojali maslahi ya nchi, wao ni CCM tu
 
SPIKA LAZIMA ADHAMINIWE NA CHAMA CHA SIASA ILA ANAWEZA ASIWEZE MBUNGE. HAKUNA MGOMBEA BINAFS KWENYE USPIKA TUSIPINDISHE SHERIA.
 
Kutokana na namna ambavyo imedhihirika kwamba sasa Spika hawezi kuwa na uhuru wa kuruhusu mijadala yenye afya kwa watanzania ndani ya bunge kwa hofu ya "kushughulikiwa" na chama (kwa vyama vyote) sasa ni muda muafaka kwa wabunge hasa wa CCM walio wengi bungeni kumpigia kura ya Ndiyo mgombea wa kiti cha Spika asiye na chama.

Wakiweza hili litakuwa na faida kubwa sana kwa taifa pia kwa wabunge wenyewe maana nao pia watakuwa huru kuishauri na kuisimamia serikali.

Wito wangu kwa wabunge wote wanaopigania uhuru wa mhimili huu wa bunge na wale wenye uwezo wa kuliongoza bunge ambao si wabunge njia pekee iliyobaki ni hiyo, chonde chonde tuitumie nafasi hii vizuri tutakuwa tumepiga hatua nzuri kuelekea kupata katiba mpya.
Wampe Wilbroad Slaa
 
Kutokana na namna ambavyo imedhihirika kwamba sasa Spika hawezi kuwa na uhuru wa kuruhusu mijadala yenye afya kwa watanzania ndani ya bunge kwa hofu ya "kushughulikiwa" na chama (kwa vyama vyote) sasa ni muda muafaka kwa wabunge hasa wa CCM walio wengi bungeni kumpigia kura ya Ndiyo mgombea wa kiti cha Spika asiye na chama.

Wakiweza hili litakuwa na faida kubwa sana kwa taifa pia kwa wabunge wenyewe maana nao pia watakuwa huru kuishauri na kuisimamia serikali.

Wito wangu kwa wabunge wote wanaopigania uhuru wa mhimili huu wa bunge na wale wenye uwezo wa kuliongoza bunge ambao si wabunge njia pekee iliyobaki ni hiyo, chonde chonde tuitumie nafasi hii vizuri tutakuwa tumepiga hatua nzuri kuelekea kupata katiba mpya.
Ni vigumu kumpata spika asiyetokana na chama! hii ni kwa sababu mgombea nafasi ya u-spika ni lazima awe na sifa za kumwezesha kuwamgombea ubunge! ambapo mojawapo ya sifa hizo ni lazima atokane na chama cha siasa, ila kwa kutofuata katiba wala mifumo rasmi hiyo itawezekana!! Nakumbuka kuwahi kuwepo nafasi ya Naibu Waziri Mkuu kama sijakosea!!!Ni ile nafasi ya mzee wa TLP
 
Siyo lazima upendekezwe na chama. Upo utaratibu wa mtu kugombea kiti cha Spika hata kama si mwanachama wa chama chochote na wala haitahitajika kudhaminiwa na chama ili mradi tu anazo sifa za kuwa mbunge ambazo zipo katika katiba ibara ya 67(1) isipokuwa (b)
Hiyo (b) ina maana haipewi umuhimu? Binafsi bado nasimamia lazima atokane na chama cha siasa, rejea pia katiba pendekezwa 125(1)c
 
Katiba inasema hivyo ndugu.
Ibara ya 84 (1)
Kutakuwa na Spika wa bunge ambaye atachaguliwa na wabunge kutoka miongoni mwa watu ambao ni wabunge au mwenye sifa za kuwa mbunge; atakuwa ndiye kiongozi wa bunge na atawakilisha bunge katika vyombo na vikao vingine vyote nje ya bunge.
Sifa mojawapo ya Spika ni kuwa na sifa za kuwa mbunge. Sifa za kuwa mbunge ni kuwa mwanachama wa chama cha siasa na ni mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa kama Katiba ilivyoainishwa hapa chini:

67.-(1) Bila ya kuathiri masharti yaliyomo katika ibara hii, mtu yeyote atakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge endapo- (a) ni raia wa Jamhuri ya Muungano aliyetimiza umri wa miaka ishirini na moja, na ambaye anajua kusoma na kuandika katika Kiswahili au Kiingereza; (b) ni mwanachama na ni mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa; (c) katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya Uchaguzi hakuwahi kutiwa hatiani katika mahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepa kulipa kodi yoyote ya Serikali.

Kwa sababu hiyo, hauwezi kugombea uspika bila kuwa mwanachama wa chama cha siasa na kupendekezwa na chama cha siasa. Hamna cha mgombea huru kwenye hili.

Amandla...
 
CCM kwa sasa ni laana kwa nchi. Ipo zaidi kwaajili ya uharibifu kuliko mema.

CCM ndiyo kikwazo kikubwa kwa mifumo bora uongozi nchini. Bila ya CCM kuondoka madarakani, kamwe nchi hii hatutakuja kuwa na mifumo bora ya kiutawala. Hakuna mahali CCM inafanya kwa dhamira njema zaidi ya kuhakijisha inabakia madarakani kwa njia zozote zile hata kama ni za kishetani.

Inaangilia mifumo ya kimahakama, bungeni, jeshini, polisi, TISS, ofisi ya CCG, DPP - kila mahali inachafua.
Jamaa ni waharibifu sn
 
Back
Top Bottom