Daaah
Sikutegemea kuona comment ya hivi, tena ya mwanamke :shock:
Sasa hapo ilitakiwa itumike tu busara ya walokuwapo hapo, mbona simu waliitoa ili waqaailiane na jamaa zake?hongera kwa moyo huo lakini hata angekuwa na kanga asingeweza kujisetiri mwenyewe
Ni ushauri tu kwa akina dada:
Leo nikiwa njiani kuelekea kwenye deiwaka kulitokea jambo ambalo kidogo ni la kusikitisha.
Akiwa kwenye daladala ambayo ilijaza kupita kiasi dada mmoja alianguka ghafla ndani ya gari hiyo. Wakati huo daladala hiyo ilikuwa imesimama kwenye foleni. Basi konda pamoja na abiria wengine waliokuwemo humo wakamsaidia kumtoa dada huyo na kumlaza pembezoni mwa barabara.
Kimavazi, dada yule alikuwa amevaa kitopu kifupi kinachobana sana pamoja na kimini.
Kutokana na tukio lenyewe lilivyotokea wakati wa kumbeba kwa kweli ilikuwa kama vile yuko mtupu (try to imagine). Basi watu waliokuwa karibu ilibidi kila mtu aanze kusema lake (hasa kuhusiana na mavazi). Wengi walilaumu kuwa akina dada wa siku hizi wanavaa nguo zinazowashika mwili lakini kwa nini wanashindwa kuweka japo kaupande kamoja ka kanga ili kiwasetiri pindi watakapopata emergence. Walikuwepo pia akina mama ambao nao walishiriki katika lawama hizo dhidi ya "mabinti" zao.
Wakati huo mimi pia nilikuwa karibu na tukio. Dada yule ilikuwa kama vile hapumui. Basi nikajaribu kuwashauri wale watu ambao walikuwa wamejikita zaidi katika kulaumu kwamba kwa wakati huo lawama haikuwa kitu cha muhimu. Badala yake tujikite katika kuhakikisha kuwa tunaokoa maisha ya binti yule huku tukihakikisha kuwa tunamsetiri utu wake. Kitu cha kwanza nilimuomba mama mmoja ambaye alikuwa amejifunga kanga atuazime kanga moja tumsetiri. Mama alikubali.
Wakati huo dada mmoja alikuwa akimpepea kwa kitambaa chepesi. Mimi niligundua kuwa hiyo isingesaidia kitu kama nitakavyoeleza hapa chini.
Kwa kuwa dada yule ali-faint katika gari ambayo ilikuwa imejaa pomoni ni dhahiri kuwa alikosa oxygen ya kutosha hivyo moyo wake kushindwa kufanya kazi sawasawa na kupelekea ubongo kukosa oxygen ya kutosha. Kitabibu, inasadikika kuwa ubongo ukikosa oxygen ya kutosha mtu anaweza akapoteza maisha ndani ya dakika 5.
Kwa kuwa mimi nina idea ya huduma ya kwanza nikaona si vibaya nikampatia yule dada huduma ya kwanza kwa kadri ninavyoweza. Kitu cha kwanza nilijitambulisha kwa watu ambao sasa walikuwa wamejaa kumzunguka yule dada bila msaada wowote na kuwaeleza kuwa ninayo mafunzo ya huduma ya kwanza.
Baada ya hapo nikamfanyia kitu kinaitwa Cardio-Pulmonary Rescusitation (CPR) kwa ajili ya kuustua moyo wake na kumwongezea oxygen. Wakati huo nilimuomba jamaa mmoja aende kutoa taarifa kwa Traffic Police ambao walikuwa upande wa pili wa barabara wakiangalia usalama wa magari. Nilimpatia jamaa mwingine achukue simu ya yule dada na ajaribu ku-search namba za jamaa zake wa karibu na kuwataarifu juu ya mkasa huo.
Mimi niliendelea na CPR hadi nilipohakikisha kuwa yule dada amepata nafuu nikamweka kwenye "Recovery Position" halafu nikamkabidhisha kwa akina mama wawili ambao walikuwepo eneo la tukio na walikuwa wakitoa msaada wa hapa na pale then na mimi nikawahi kwenye "kijiwe changu cha kuponda kokoto".
Nikiwa njiani nilijaribu kutafakari mambo mengi sana kichwani lakini kikubwa ambacho niliona si vibaya nikawashauri akina dada:
Jamani, pamoja na kupiga mapigo makali ya viwalo si vibaya kwenye hayo mapochi yenu mkaweka japo kaupande ka kanga. Huwezi jua njiani!
Note: Kisa hiki kimetokea kweli leo asubuhi kama nilivyokielezea.
mkuu mimi siwezi kujitafutia umaarufu jf ror what? Nadhani kwa commet yako hii wewe ndo unaonekana mjinga zaidiwakati mwingine unaweza kudhani watu wanatumia mbinu ya kujifanya wajinga ili kujipatia umaarufu humu, lakini ndo tunawaona wajinga kweli hivyo.
mkuu mimi siwezi kujitafutia umaarufu jf ror what? Nadhani kwa commet yako hii wewe ndo unaonekana mjinga zaidi
kama ni lazima mwanamke atembe na kanga ingekuwa imewekwa iyo sheria kwenye
huduma ya kwanza
mimi kwangu sioni kama ni muhimu wala sitokaa nione ni muhimu kamwe,kuna njia nyingi za kukabiliana na majanga mkuu.sio kila lawama mnambebesha mwanamke khaaaaaaaaaa
Mkeshaji,
Napata hisia kama ulimpa huyu dada "Mouth to Mouth" mzee :lol:
kwa mwanamke khanga si kwa ajili ya kufunikwa ukizimia tu, wanawake tuna mambo mengi na ukiwa na khanga utasitirika, nadhani mleta mada ana nia safi kabisa sioni sababu ya kuwaambia na wanaume nao wavae khanga! Wakati mwingine tuko too sensitive unnecessarily!
SL rudisha ule upande wa kanga yangu iloandikwa 'utamu wa shoki shoki nyama peke yake'....ile ingine nakuachia
ni dakika 3 tu na si 5 ubongo ukikosa oxgen..lazima ufe.....
asante kwa msaada uliotoa.....
kumbe mi ni huduma ya kwanza . . . . :lol:
Wakati mwingine unaweza kudhani watu wanatumia mbinu ya kujifanya wajinga ili kujipatia umaarufu humu, lakini ndo tunawaona wajinga kweli hivyo.
Hivi smile kuna mahali mwanamke amebebeshwa lawama hapa? Nijuavyo mimi imeletwa kama ushauri, na ushauri huwa unatolewa bure kuukubali au kuukataa ni haki yako ya msingi....ila pia sio lazima utoe lugha chafu, kama wewe huoni umuhimu wa kubeba kanga au mtandio kwenye handbag yako ni sawa na ungeweza kutufundisha na sie washamba tunaobeba mbadala wake ni nini. Jf ni mahali pa kufundishana na kujifunza hivyo mie binafsi ningefurahi kusikia mwenzetu una mbadala gani..mkuu mimi siwezi kujitafutia umaarufu jf ror what? Nadhani kwa commet yako hii wewe ndo unaonekana mjinga zaidi
kama ni lazima mwanamke atembe na kanga ingekuwa imewekwa iyo sheria kwenye huduma ya kwanza
mimi kwangu sioni kama ni muhimu wala sitokaa nione ni muhimu kamwe,kuna njia nyingi za kukabiliana na majanga mkuu.sio kila lawama mnambebesha mwanamke khaaaaaaaaaa
mkuu mimi siwezi kujitafutia umaarufu jf ror what? Nadhani kwa commet yako hii wewe ndo unaonekana mjinga zaidi
kama ni lazima mwanamke atembe na kanga ingekuwa imewekwa iyo sheria kwenye huduma ya kwanza
mimi kwangu sioni kama ni muhimu wala sitokaa nione ni muhimu kamwe,kuna njia nyingi za kukabiliana na majanga mkuu.sio kila lawama mnambebesha mwanamke khaaaaaaaaaa
Kanga ya nini?Mwingine anabeba ili na yeye aonekane mwanamke kwa vile kaaminishwa kubeba kanga ndio kutamfanya aonekane mwanamke na hasa mbele ya wanaume.
Ingekuwa kanga itakuzuia na wezi au matapeli hapa bongo kweli,vinginevyo hata mwanaume anatakiwa ajisitiri.
Hivi smile kuna mahali mwanamke amebebeshwa lawama hapa? Nijuavyo mimi imeletwa kama ushauri, na ushauri huwa unatolewa bure kuukubali au kuukataa ni haki yako ya msingi....ila pia sio lazima utoe lugha chafu, kama wewe huoni umuhimu wa kubeba kanga au mtandio kwenye handbag yako ni sawa na ungeweza kutufundisha na sie washamba tunaobeba mbadala wake ni nini. Jf ni mahali pa kufundishana na kujifunza hivyo mie binafsi ningefurahi kusikia mwenzetu una mbadala gani..