Ushauri wangu kwa serikali na Tume ya Taifa ya Uchaguzi - Kabla ya kurejesha kura ya Maoni

Ushauri wangu kwa serikali na Tume ya Taifa ya Uchaguzi - Kabla ya kurejesha kura ya Maoni

Mapambano Yetu

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2012
Posts
1,130
Reaction score
2,102
Katiba ni mali ya watanzania wote bila kujali dini, kabila, umri, na elimu ya mtu. Hivyo ni vema serikali ikahakikisha maridhiano kabla ya kuirejesha kwa wananchi ili ipigiwe kura. Haitakuwa vyema kura ya maoni iliyohairishwa ikarejeshwa na kupata kura nyingi za "HAPANA". Ili kuepuka hayo, binafsi naishauri serikali kufanya yafuatayo:

1. Makundi yanayopingana yapatanishwe kwanza ili kuweka mambo sawa. Hapa namaanisha serikali ifanye UPATANISHO WA KWELI baina ya waislam na wakristu. Yale aliyokuwa akiyafanya Pinda ni vichekesho vitupu. Huwezi kukutanisha viongozi wa dini ambao unajua dhahiri kuwa ni wafuasi wako kisiasa na ni wanaccm watiifu ukasema kuwa umefanya upatanisho. Inabidi kukutanisha viongozi wa Waislam wenye msimamo mkali, Viongozi kutoka jukwaa la Wakristu na makundi mengine ya dini bila kujali itikadi zao kisiasa ili kufanya upatanisho wa kweli.


2. Serikali ihakikishe imefanya upatanisho wa kisiasa baina ya vyama vyetu. Pale palipo na makosa yarekebishwe kabla ya kurejea kwenye kura ya maoni. Tutafurahi kama serikali, ccm na ukawa watakaa meza moja na kufanya makubaliano yenye tija na mwelekeo wa kitaifa bila kujali itikadi za vyama vyao.


3. Tume ya Uchaguzi iepuke kutumiwa kama mtaji kwa baadhi ya vyama vya siasa (ccm). Kabla ya kutangaza tarehe ya kura maoni tume ijiridhishe kwanza kuwa kila kitu kiko sawa. Mfumo wa kuwafurahisha watawala haufai kwa dunia ya sasa. Zaidi itakuwa ni kujidhalilisha kama ilivyodhalilika this time.

NAWATAKIA UTEKELEZAJI MWEMA

"MUNGU IBARIKI TANGANYIKA, MUNGU IBARIKI ZANZIBAR"
"MUNGU IBARIKI TANZANIA"

 
Mkuu, unashauri halafu unawatakia 'utekelezaji mwema' dah.

Back to the topic, upatanisho unaopendekeza ufanyike tu baada ya kuondoa hiyo katiba ya nyoka wa makengeza na kurejesha ile yenye maoni ya wananchi. Short of that, hakuna upatanisho utakaotoa suluhu ya mkwamo tulionao.

cb
 
Mkuu, unashauri halafu unawatakia 'utekelezaji mwema' dah.

Back to the topic, upatanisho unaopendekeza ufanyike tu baada ya kuondoa hiyo katiba ya nyoka wa makengeza na kurejesha ile yenye maoni ya wananchi. Short of that, hakuna upatanisho utakaotoa suluhu ya mkwamo tulionao.

cb


Hata hilo ulilolisema ni sehemu ya suruhu. Wakirejea kwenye Maoni ya wananchi kama yalivyokuwa yameainishwa na Tume ya warioba nadhani hiyo ndo itakuwa suruhu ya kudumu kwa upande wa vyama vya siasa
 
Mkuu, unashauri halafu unawatakia 'utekelezaji mwema' dah.

Back to the topic, upatanisho unaopendekeza ufanyike tu baada ya kuondoa hiyo katiba ya nyoka wa makengeza na kurejesha ile yenye maoni ya wananchi. Short of that, hakuna upatanisho utakaotoa suluhu ya mkwamo tulionao.

cb

Huo ushauri wa upatanisho ulishatolewa kitambo tangia existence ya BMK watu wakajifanya wajanja wale jamaa wa UKAWA ambao ndio vinara wanaoombewa suluhu as if wao hawajiwezi, ushauri wako sijui kama unatekelezeka afu nani mpatanishi kwa faida ya nani?hao wanaopatanishwa ni dhidi ya nani?sheria ikoje?
 
Hata hilo ulilolisema ni sehemu ya suruhu. Wakirejea kwenye Maoni ya wananchi kama yalivyokuwa yameainishwa na Tume ya warioba nadhani hiyo ndo itakuwa suruhu ya kudumu kwa upande wa vyama vya siasa

Watu wengine bwana wanakumbuka shka kumekucha,wao si walienda kutafuta suluhu kwa umma na ndio maana wakajiita ukawa sasa leo hao wananchi waliowaendea ndio kwanza wanajiandaa kujiandikisha ili wapige kura sasa si watulie?wanahofu nini na kuanza kutafuta ahueni????
 
Mkuu, unashauri halafu unawatakia 'utekelezaji mwema' dah.

Back to the topic, upatanisho unaopendekeza ufanyike tu baada ya kuondoa hiyo katiba ya nyoka wa makengeza na kurejesha ile yenye maoni ya wananchi. Short of that, hakuna upatanisho utakaotoa suluhu ya mkwamo tulionao.

cb


Lazima awatakie utekelezaji mwema maana hajui alichokiandika kamezeshwa huyo!!!!
 
Mkuu, unashauri halafu unawatakia 'utekelezaji mwema' dah.

Back to the topic, upatanisho unaopendekeza ufanyike tu baada ya kuondoa hiyo katiba ya nyoka wa makengeza na kurejesha ile yenye maoni ya wananchi. Short of that, hakuna upatanisho utakaotoa suluhu ya mkwamo tulionao.

cb

Tuongee kama Watanzania wenye kuipenda nchi yao, Katiba Mpya ili ipatikane ililazimu ianzishwe kisheria na Sheria ya mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011. Na taratibu zake. Ni lazima kuheshimu sheria iliyotungwa na Bunge letu kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo ndiyo msingi wahoja ya Katiba nchini. Tusirudishane nyuma kama hufahamu taratibu hizo ni vizuri ukauliza usaidiwe maana hapa JF ni mwafaka pa kupata elimu
 
Swala kubwa hapa ni sisi watanzania wenzangu tutambue kuwa nchi hii ni yetu sote na haina itikadi zinazoegemea upande fulani,kwa mantiki hiyo ni vyema tukashikamana katika kuhakikisha kuwa nafasi hii iliyotolewa na tume ya taifa ya uchaguzi tunaitumia vzr na tunaepuka kuingia kwenye mtego wa makundi ya viongozi wetu wa dini kwa kuwa yatatugawa na athari zake sote tunazijua kwa hiyo hebu tubaki na msimamo wa kuisoma katiba inayopendekezwa na mwisho tuipigie kura pasipo na shinikizo toka kwa mtu yeyote kwakuwa tunao utashi wetu na hii ni haki ya msingi katika kuamua mustakabali wa nchi yetu,tuepuke makundi yenye mawazo ya kutugawa katika swala hili la kura ya maoni kuhusu katiba inayopendekezwa
 
Katiba ni mali ya watanzania wote bila kujali dini, kabila, umri, na elimu ya mtu. Hivyo ni vema serikali ikahakikisha maridhiano kabla ya kuirejesha kwa wananchi ili ipigiwe kura. Haitakuwa vyema kura ya maoni iliyohairishwa ikarejeshwa na kupata kura nyingi za "HAPANA". Ili kuepuka hayo, binafsi naishauri serikali kufanya yafuatayo:

1. Makundi yanayopingana yapatanishwe kwanza ili kuweka mambo sawa. Hapa namaanisha serikali ifanye UPATANISHO WA KWELI baina ya waislam na wakristu. Yale aliyokuwa akiyafanya Pinda ni vichekesho vitupu. Huwezi kukutanisha viongozi wa dini ambao unajua dhahiri kuwa ni wafuasi wako kisiasa na ni wanaccm watiifu ukasema kuwa umefanya upatanisho. Inabidi kukutanisha viongozi wa Waislam wenye msimamo mkali, Viongozi kutoka jukwaa la Wakristu na makundi mengine ya dini bila kujali itikadi zao kisiasa ili kufanya upatanisho wa kweli.


2. Serikali ihakikishe imefanya upatanisho wa kisiasa baina ya vyama vyetu. Pale palipo na makosa yarekebishwe kabla ya kurejea kwenye kura ya maoni. Tutafurahi kama serikali, ccm na ukawa watakaa meza moja na kufanya makubaliano yenye tija na mwelekeo wa kitaifa bila kujali itikadi za vyama vyao.


3. Tume ya Uchaguzi iepuke kutumiwa kama mtaji kwa baadhi ya vyama vya siasa (ccm). Kabla ya kutangaza tarehe ya kura maoni tume ijiridhishe kwanza kuwa kila kitu kiko sawa. Mfumo wa kuwafurahisha watawala haufai kwa dunia ya sasa. Zaidi itakuwa ni kujidhalilisha kama ilivyodhalilika this time.

NAWATAKIA UTEKELEZAJI MWEMA

"MUNGU IBARIKI TANGANYIKA, MUNGU IBARIKI ZANZIBAR"
"MUNGU IBARIKI TANZANIA"

Ndugu senior ulianza vizuri sana ila ukamalizia vibaya. Hapa hatuna Tanganyika. Sijui wakati wa Tanganyika kama ulikuwa umezaliwa. Hata tuliokuwepo tulikaa nayo kwa muda mfupi sana baadaye ikawa Tanzania. Ufunguliwe ufahamu ili ujitambue mahali unapoishi. Kesho ukiamka usije ukajiita msomali au Mnigeria.
 
Katiba ni mali ya watanzania wote bila kujali dini, kabila, umri, na elimu ya mtu. Hivyo ni vema serikali ikahakikisha maridhiano kabla ya kuirejesha kwa wananchi ili ipigiwe kura. Haitakuwa vyema kura ya maoni iliyohairishwa ikarejeshwa na kupata kura nyingi za "HAPANA". Ili kuepuka hayo, binafsi naishauri serikali kufanya yafuatayo:

1. Makundi yanayopingana yapatanishwe kwanza ili kuweka mambo sawa. Hapa namaanisha serikali ifanye UPATANISHO WA KWELI baina ya waislam na wakristu. Yale aliyokuwa akiyafanya Pinda ni vichekesho vitupu. Huwezi kukutanisha viongozi wa dini ambao unajua dhahiri kuwa ni wafuasi wako kisiasa na ni wanaccm watiifu ukasema kuwa umefanya upatanisho. Inabidi kukutanisha viongozi wa Waislam wenye msimamo mkali, Viongozi kutoka jukwaa la Wakristu na makundi mengine ya dini bila kujali itikadi zao kisiasa ili kufanya upatanisho wa kweli.


2. Serikali ihakikishe imefanya upatanisho wa kisiasa baina ya vyama vyetu. Pale palipo na makosa yarekebishwe kabla ya kurejea kwenye kura ya maoni. Tutafurahi kama serikali, ccm na ukawa watakaa meza moja na kufanya makubaliano yenye tija na mwelekeo wa kitaifa bila kujali itikadi za vyama vyao.


3. Tume ya Uchaguzi iepuke kutumiwa kama mtaji kwa baadhi ya vyama vya siasa (ccm). Kabla ya kutangaza tarehe ya kura maoni tume ijiridhishe kwanza kuwa kila kitu kiko sawa. Mfumo wa kuwafurahisha watawala haufai kwa dunia ya sasa. Zaidi itakuwa ni kujidhalilisha kama ilivyodhalilika this time.

NAWATAKIA UTEKELEZAJI MWEMA

"MUNGU IBARIKI TANGANYIKA, MUNGU IBARIKI ZANZIBAR"
"MUNGU IBARIKI TANZANIA"

Tanganyika tena? Wewe wa wapi, Tangayika ilikuwa enzi hizo wakati wa mababu zetu, sema Tanzania bhana.
 
Ndugu senior ulianza vizuri sana ila ukamalizia vibaya. Hapa hatuna Tanganyika. Sijui wakati wa Tanganyika kama ulikuwa umezaliwa. Hata tuliokuwepo tulikaa nayo kwa muda mfupi sana baadaye ikawa Tanzania. Ufunguliwe ufahamu ili ujitambue mahali unapoishi. Kesho ukiamka usije ukajiita msomali au Mnigeria.


Kama Tanzania sio Muungano wa nchi mbili, Tanganyika na Zanzibar basi hoja yako itakuwa ni ya msingi sana
 
Tuongee kama Watanzania wenye kuipenda nchi yao, Katiba Mpya ili ipatikane ililazimu ianzishwe kisheria na Sheria ya mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011. Na taratibu zake. Ni lazima kuheshimu sheria iliyotungwa na Bunge letu kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo ndiyo msingi wahoja ya Katiba nchini. Tusirudishane nyuma kama hufahamu taratibu hizo ni vizuri ukauliza usaidiwe maana hapa JF ni mwafaka pa kupata elimu

Hiyo sheria unayoirejea hapa iliposainiwa tu ilifanyiwa marekebisho kabla hata haijatumika. Kama wewe ni mfuatiliaji utakumbuka sababu ya marekebisho hayo ya kihistoria. Lakini itoshe kusema kwa sheria haindoi tatizo let alone upatikanaji wa sheria yenyewe! Chama chenye wabunge wengi (ikiwa ni pamoja na spika) hakijawahi kuwa na ajenda ya katiba, je unategemea watunge sheria ya kutunga katiba nzuri ilhali wenyewe wanataka iliyopo iendelee?? Wakati mwingine uwe unachanganya na za kwako.
 
Hiyo sheria unayoirejea hapa iliposainiwa tu ilifanyiwa marekebisho kabla hata haijatumika. Kama wewe ni mfuatiliaji utakumbuka sababu ya marekebisho hayo ya kihistoria. Lakini itoshe kusema kwa sheria haindoi tatizo let alone upatikanaji wa sheria yenyewe! Chama chenye wabunge wengi (ikiwa ni pamoja na spika) hakijawahi kuwa na ajenda ya katiba, je unategemea watunge sheria ya kutunga katiba nzuri ilhali wenyewe wanataka iliyopo iendelee?? Wakati mwingine uwe unachanganya na za kwako.
Acha uongo wako wewe mchumia tumbo, unayoyasena hayo nahc unajitungia tu, ukweli unaujua.
 
Acha uongo wako wewe mchumia tumbo, unayoyasena hayo nahc unajitungia tu, ukweli unaujua.

It seems you are a real Alien. Pole sana. Siku nyingine uache kuhisi utafute facts, poor you!
 
It seems you are a real Alien. Pole sana. Siku nyingine uache kuhisi utafute facts, poor you!
Jina lako hapo linatudhihirishia kuwa yote uyasemayo unabahatisha ndo maana umejiita CABHATICA yani unajibu kwa kulabdialabdia ama bla bla tu. Hahahah pole kijana
 
Jina lako hapo linatudhihirishia kuwa yote uyasemayo unabahatisha ndo maana umejiita CABHATICA yani unajibu kwa kulabdialabdia ama bla bla tu. Hahahah pole kijana

Mimi namjibu ALIEN we ebola umetoka wapi? Kutumia ID nyingi ni dalili ya kutokujiamini.

cc UFO_ALIEN
 
Last edited by a moderator:
Mkuu, unashauri halafu unawatakia 'utekelezaji mwema' dah.

Back to the topic, upatanisho unaopendekeza ufanyike tu baada ya kuondoa hiyo katiba ya nyoka wa makengeza na kurejesha ile yenye maoni ya wananchi. Short of that, hakuna upatanisho utakaotoa suluhu ya mkwamo tulionao.

cb

Huyu nae unawaza kupatanisha watu gani?sie tunawaza tarehe ya kupiga kura wewe unawaza kupatanisha watu ambao hata hawajulikani wako wapi??? acha kuzingua.
 
Huyu nae unawaza kupatanisha watu gani?sie tunawaza tarehe ya kupiga kura wewe unawaza kupatanisha watu ambao hata hawajulikani wako wapi??? acha kuzingua.

Mkuu umetoka kuamka nini?? Kama huelewi kinachojadiliwa si dhambi kupita kimyakimya. Waachie wenye uelewa, wewe endelea kuwaza kupiga kura maana hilo ndilo fungu lako.
 
Mkuu, unashauri halafu unawatakia 'utekelezaji mwema' dah.

Back to the topic, upatanisho unaopendekeza ufanyike tu baada ya kuondoa hiyo katiba ya nyoka wa makengeza na kurejesha ile yenye maoni ya wananchi. Short of that, hakuna upatanisho utakaotoa suluhu ya mkwamo tulionao.

cb


Cabhatica unawaza kuondoa Katiba inayopendekezwa then what?acha nadharia hapa huo mkwamo unaousemea umetokea wapi wenzio tunasubiri tarehe tu aaa kura kama kawa!
 
Back
Top Bottom