lunatoc
JF-Expert Member
- Aug 16, 2017
- 2,911
- 5,479
Moja ya shauri za hovyo tangu mwaka huu uanzeMkuu,kama umestaafu,huna majukumu ya kimaisha kama vile kusomesha etc na unavitega uchumi vya kukuwezesha kuishi basi nakushauri ufanye yafuatayo.
Gawa Pesa yako katika makundi manne:
Kundi la kwanza liwe urithi-
Kundi la Pili liwe sadaka
Kundi la tatu liwe akiba
Kundi la nne liwe uwekezaji
Kwenye Hela ya Urithi weka kwenye T-Bonds au kwenye Fixed deposit ya muda mrefu kutegemea na kiasi cha riba.
Hela ya sadaka tumia kuwekeza katika kutatua changampoto ya kijamii katika eneo lako.Hasa inayohusu elimu au afya.Unaweza kuanzisha NGO yako ukajenga legacy yako nzuri tua kama philantropist.Kuna mahitaji mengi sana katika jamii ambayo yanaitaji watu wenye moyo wa kutoa.Na pia unapojenga NGO yako unaweza pia kupata michango ya wafadhili ili uweze kupiga hatua kubwa zaidi na kusaidia wengi.
Kwenye hela yako ya akiba weka benki tu ili ipate faida taratibu na huku ukiitumia kwa mambo yako madogo madgo kama kununua luku n.k.
Kwenye hela yako uwekezaji hio unaweza ukatumia muda kutafiti aina ya biashara ya kufanya ambayo ina faida nzuri na usiwe na haraka nayo.
Jambo unapaswa kuwa na haraka nalo na la hela ya SADAKA.hilo anza nalo mapema sana na litakusaidia kupata BARAKA nyingi kwa kusaidia wahitaji na kuacha LEGACY katika eneo unaloishi
Nakutakia kila la heri na karibu sana iwapo unahitaji msaada na ushauri zaidi.
Sent using Jamii Forums mobile app