Ushauri wenu tafadhali, Ardhi huua

Ushauri wenu tafadhali, Ardhi huua

TheMnyonge

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2022
Posts
738
Reaction score
1,886
Moja kwa moja kwenye mada, itifaki imezingatiwa!

Mwaka 2018 nilinunua kiwanja maeneo ya mtaa wa mawasiliano, Mkundi -Morogoro!

Baada ya kununua na kuandikishana kupitia serikali za mitaa niliendelea na shughuli zangu hapa nchini.

Mwaka 2020 walioniuzia wakaamua kupima viwanja kwenye maeneo yao (walikuwa na maeneo makubwa)

Wakati wa upimaji, wakajumuisha na kipande changu bila kunifahamisha, na kutokana na mchoro wa kampuni iliyopima structure ya viwanja ikabadilika kabisa...

Baada ya kugundua kuwa kiwanja kimepimwa, nilifuatilia kampuni ya upimaji, wakanitoa wasi wasi kwamba kiwanja changu kitakuwa salama, nifanye utaratibu wa kulipia gharama za upimaji, tukakubaliana hivyo, lakini kwa kadri muda unavyokwenda naona dalili za walioniuzia n'a waliopima kama kuna mpango ovu nyuma ya pazia!

Nini nifanye ili kunusuru ardhi yangu hii, nilipie gharama za upimaji then nianze kudai hati?
Au nikatae zoezi la kampuni kupima kiwanja changu bila kunishirikisha?

Sent from my Infinix X652 using JamiiForums mobile app
 
Una maandishi na mashahidi. Nenda kwa waliokuuzia uwaulize suala la kiwanja walichokuuzia limekaaje. Na kwa nini walipima bila kukutaarifu? Ukipata majibu ndiyo utaanzia hapo.
 
Back
Top Bottom