bitekutecha
Member
- Nov 5, 2017
- 15
- 6
Nimejaribu kukiangalia kikosi cha zanzibar kwenye michuano ya kombe la chalenji inayoendelea nchini kenya ambako timu yetu ya Kilimanjaro stars imeambulia patupu, ninashauri kocha wa Stars ateue kikosi kizima cha Zanzibar kilichotinga nusu fainali kiwe ndio Taifa Stars yetu, hii ni kutokana na uwezo mkubwa iliouonyesha katika michuano hiyo hadi kufikia hatua cecafa wameamua kuwapima mkojo wachezaji wake kubaini kama wanatumia dawa za kuongeza nguvu.
Hahahaaa wewe hujui kwanini wazenji ni bora. Hawa wachezaji wengi wanacheza bara, hawa wana vipaji walipaswa kucheza bara kama professionals. Ni sawa na bara wangewachukuwa mf. Samatta wangefanya vizuri. Nashauri ZFA waangalie suala la michezo lisiwe la muungano ili waZNZ wawe professionals kule bara.
Kwani toke lini Michezo ilikuwa suala la Muungano?Hahahaaa wewe hujui kwanini wazenji ni bora. Hawa wachezaji wengi wanacheza bara, hawa wana vipaji walipaswa kucheza bara kama professionals. Ni sawa na bara wangewachukuwa mf. Samatta wangefanya vizuri. Nashauri ZFA waangalie suala la michezo lisiwe la muungano ili waZNZ wawe professionals kule bara.
Tutaona kama mtacheza CAF.Kwani toke lini Michezo ilikuwa suala la Muungano?
Hujajibu swali, Tokea huo Muuitao muungano uanzishwe Michezo sio suala la Muungano, lakini kwa kujidai ujanja wenu Tangnanyika ikajidai kua ndio Tanzania ikawa Hela zote za kukuza michezo kutoka FIFA munazila nyinyi tuTutaona kama mtacheza CAF.
Nani alie kwambia suala la michezo ni la muungano? taifa stars kujitia fifa na cap ni kinyume cha katiba na mkataba wa muungano, tatizo lilopo wabunge wa ccm zanzibar na cuf wameshindwa kuhoji uhalali wa taifa stars kujitia fifa.Hahahaaa wewe hujui kwanini wazenji ni bora. Hawa wachezaji wengi wanacheza bara, hawa wana vipaji walipaswa kucheza bara kama professionals. Ni sawa na bara wangewachukuwa mf. Samatta wangefanya vizuri. Nashauri ZFA waangalie suala la michezo lisiwe la muungano ili waZNZ wawe professionals kule bara.
Matusi hayo!Nimejaribu kukiangalia kikosi cha zanzibar kwenye michuano ya kombe la chalenji inayoendelea nchini kenya ambako timu yetu ya Kilimanjaro stars imeambulia patupu, ninashauri kocha wa Stars ateue kikosi kizima cha Zanzibar kilichotinga nusu fainali kiwe ndio Taifa Stars yetu, hii ni kutokana na uwezo mkubwa iliouonyesha katika michuano hiyo hadi kufikia hatua cecafa wameamua kuwapima mkojo wachezaji wake kubaini kama wanatumia dawa za kuongeza nguvu.
Kutokana na umahiri na ushujaa mkubwa pamoja na mafanikio ya timu ya taifa ya zanzibar nimewaza tufanye hivi; Timu hii na kocha wake pamoja na jopo lote la ufundi wapewe nafasi na ndio iunde timu ya taifa ya Tanzania-Taifa Stars. Nimewaza hivi kwasababu hii ni nchi moja na inapofika ushiriki wa mashindano makubwa zanzibar haihesabiwi. Ni kweli watanzania tunakiu ya mafanikio katika soka, lakini tunafanikiwaje? Hebu tuitumie timu hii kama Taifa Stars, labda hii inaweza kuwa fursa kwetu. Naamini hatuhitaji majina makubwa ili kushinda, TUNAHITAJI WACHEZAJI WANAOELEWA NA KUTAMBUA KUWA ZAIDI YA WATANZANIA MILIONI 45 WANAWATEGEMEA NA KUWAAMINI WATU 30 TU ILI KULILETEA SIFA TAIFA- HATUHITAJI WAPIGA PESA WANAOTANGUZA TAMAA BADALA YA KAZI, tunahitaji nia na malengo na kujituma. Kama majina makubwa tulisha yatumia sana lakini mafanikio ni sifuri. Nakaribisha maoni, povu, matusi vyote ruksa!
Hiyo ni kweli kabisa mi nimecheza mpira na wapemba wakati mdogo, yaani jamaa mpira uko kwenye damu kabisa na hata kichwani wapemba wapo vizuri.Kama mlikuwa hamjui ndio mnatakiwa mjue kuwa zanzibar toka zamani kiuhalisia ina vipaji vingi sana vya mpira.
Ukiwaona unaweza kuwadharau lakini wanakuaibisha mbele ya macho yako