bitekutecha
Member
- Nov 5, 2017
- 15
- 6
Nimejaribu kukiangalia kikosi cha zanzibar kwenye michuano ya kombe la chalenji inayoendelea nchini kenya ambako timu yetu ya Kilimanjaro stars imeambulia patupu, ninashauri kocha wa Stars ateue kikosi kizima cha Zanzibar kilichotinga nusu fainali kiwe ndio Taifa Stars yetu, hii ni kutokana na uwezo mkubwa iliouonyesha katika michuano hiyo hadi kufikia hatua cecafa wameamua kuwapima mkojo wachezaji wake kubaini kama wanatumia dawa za kuongeza nguvu.