Ushawahi kujifanya mjuaji ukaja kuumbuka?

Ushawahi kujifanya mjuaji ukaja kuumbuka?

BoManganese

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2017
Posts
980
Reaction score
2,679
Habari zenu wanaJF. Kama kichwa cha habari kisemavyo hapo juu, katika harakati za hapa na pale katika maisha inaweza kutokea situation fulani tuu ukajikuta unajua kitu na kukifanya mbele za watu hatimae unaumbuka hapo ndo unakuja ule msemo usemao "utajua ujui".

Mimi binafsi miaka ya nyuma kidogo nilienda water park fulani hivi kurefresh kuogelea kwenye swimming pools kufika pale nikakuta kuna swimming pools za wakubwa zenye kina kirefu na za wadogo zenye kina kifupi. Sasa sikutaka hata kujiuliza kwanini kule kwenye kina kifupi ndio kuna watu wengi kuliko ile pool nyingine yenye kina kirefu nikaona potelea pote washamba tuu. Kwakweli sikuwa nimewahi kwenda before ndo ilikuwa ni mara ya kwanza ndipo kidume nikajikuta mjuaji kwamba ndio best diver sikutaka kwenda kwenye kina kifupi nikajichanganya kwenye swimming pool yenye kina kirefu na kulikuwa na alert kabisa pale ila mimi nikajiona much know. Basi nikaingia kwenye swimming pool taratibu nikiwa nimejiegemeza pembezoni kabisa huku ukutani nikicheki watu wawili watatu mule wakicheza michezo yao.

Sasa sijui ni kitu gani kikanitekenya nikaona ngoja nisogee pale katikati nikajipush kutoka pale pembezoni yaani kama nilitumia nguvu ya ule ukuta kuswim hata pale kati sikufika vizuri nikaanza kuhisi kama navutwa ndani ya maji nikaanza kuvuta picha kwa wale wataalam wanavyo ogelea huwa kuna namna wana piga miguu ndani ya maji wanaelea basi na mimi nikaanza kufanya vile nikawa narudi juu kidogo nikiacha kupiga miguu nazama tena pale kwenye angle ya swimming napaona ila kupafikia ndio ilikuwa shughuli kwangu nilipiga sana miguu nikatumia utaalamu wote niliouona kwenye TV vile wanaogeleaga lakini wapi kupiga kelele za kuomba msaada napo nilikuwa naona aibu.

Mwisho wa siku baada ya kutapatapa sana na ukizingatia kwenye angle palikuwa sio mbali basi nikachoka nikajiachia tuu nikawa nazama ndo kama nilikuwa naiona dunia inazunguka nikiwa ndani ya maji huku nikiwa nakunywa vikombe heavy vya maji taratibu kabisa. Wakati naelekea kufumba macho kuiaga dunia kwa mbali nikaona malaika ananipa mkono na mimi nikaona nimpe mkono japo kwa kujikongoja sana huku nikijisemea moyoni Bwana ametoa Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe, nikampa mkono. Mara ghafla nikaona nimeibuliwa kwa nguvu kutoka ndani ya maji kumbe alikuwa ni jamaa tuu nahisi alikuwa ananichora tuu tangu mda ule natapatapa.

Basi akanivuta akanishikisha ile angle aisee niliing'ang'ania kwa nguvu zangu zote huku nikiwa nakohoa nikapanda hadi juu nje ya swimming pool kwa speed ya mwanga nikakaa pembeni nikiwa siamini yaliyo nitokea pale dakika chache zilizo pita huku kwa mbali nikisikia vicheko vya watu ni dhahiri kabisa mimi ndiye niliyekuwa nachekwa maana kwa wakati huo akili haikuwepo kabisa pale.
Nikanyanyuka nikatafuta nguo zangu zilipo nikavaa nikapiga msosi pale fasta nikaondoka zangu home bila hata kugeuka nyuma. Yaani hapo ndio nilijua sijui.

Vipi na nyinyi wadau ni kitu gani ulijifanya mjuaji ukaumbuka hebu tiririkeni hapo hata kama sio wewe lakini ulimshuhudia mtu mwingine,


Karibuni.
 
Kanisaniii...

Watumishi ilitokea wamepungua wawili, basi Father Akaomba yeyote anayejua Kutumikia apite mbele akavae joho, mzee mzima nikapanda madhabahuni nikaingia room nikavaa Joho..

Kwa kufupisha... Nilichanganya madesa kuanzia kwenye uvaaji, Joho nimegeuza, kola nayo imegeukia mabegani, cheteso nacho hakishikiki, full ku vibrate. Nikiangalia waumini wanaziba midomo, nikajiridhisha hii ni live nazingua sio kama najishtukia tuu.

kumcheki best yangu, ndio kainama kwenye benchi kwa kukosa nguvu za kucheka, huyu ndio akanipa go ahead kua mzee, toka sasa Utageuza altale kua futuhi, nikaone isiwe tabuu, nikarudi kinyume nyumee... Nilichomokea mlango ule wa nyuma ya Altale, nikavua joho nikasepa misa ikiwa kati...

Niliacha vicheko na taharuki kwa waumini na Wote pale mbele, na ilikua mtu zaidi ya 200..
 
Kanisaniii...
Watumishi ilitokea wapungua wawili, basi Father Akaomba yeyote anayejua Kutumikia apite mbele akavae joho, mzee mzima nikapanda madhabahuni nikaingia room nikavaa Joho..
Kwa kufupisha nilichanganya madesa kuanzia kwenye uvaaji, kushika vifaa na kila kitu...

Mambo yalivyozidi kua magumu, nikaone isiwe tabuu..
Nilichomokea mlango ule wa nyuma ya Altale, nikavua joho nikasepa misa ikiwa kati...

Niliacha vicheko na taharuki kwa waumini na Wote pale mbele, na ilikua mtu zaidi ya 200..

Pili nilitoka mjini nikaenda kijijini kusalimia, nikajitia najua ngumi tena za movie,
Nikalichokoza jamaa flani hivii...

Kilichonipata ilibidi niingie kwenye karavati, yeye alishindwa sababu ya mwili mkubwa.
[emoji23][emoji23][emoji23]noumer sana
 
Dada alipika wali home nikaukosoa vibaya mno kwa maneno mbofu mbofu tukiwa mezani nkawa nakula huku naongea tu wali m'baya m'baya,,nkawa naelekeza hiki kingefanyika hivi,kingefanyika vile Muda huo mimi tu ndio

Natawala maongezi watu wengine mezani wote kimya,nilipomaliza mama akasema kesho CONTROLA upike wali kisha wewe dada utamsaidia kupika mboga,Kimoyo moyo nikasema ngojea mtajua kuwa mimi ndio mpishi konki

Mama alivyotoa maagizo nikaitkia kisha nikasema kesho ntapika mimi,dada akaambiwa akimaliza kupika asigse kitu kingine chochote,basi kidume kesho ikafika nilichokipika Ki ukweli ilibidi nisingizie naumwa tumbo ghafla maana balaa lake nilijua lingekua kubwa

Lakini pamoja na kusingizia naumwa,janja yangu mama aliishtukia alisema niitwe kisha nikalazimishwa kula ule wali wengine wote wakanunuliwa kiepe kuku,mimi niliambiwa ule wali wangu uishe Nikiula wiki sawa,nikiula mwezi sawa

Ila ole wangu nitupe kile chakula,(bi kubwa angu n mkoloni sana) ki ukweli nilikula ule wali/uji sijui wiki nzima ile mpaka nikamaliza chakula chote,tangia Hapo sijawahi kosoa chakula chochote hata kama n kibaya vipi kapika mama ntilie

Nikiona kitu kibaya namezea kimya kimya ila sikosoi mtu na kupitia ile adhabu nilijikuta nampenda yule dada angu kiasi kwamba ikawa nikirudi mahali,nikimkuta jikoni naenda kupka nae.
 
Tulikua tunaenda Dodoma na coaster tulipofika maeneo ya Mbezi kuna dogo akamwambia konda tukifika Morogoro naomba uniambie konda kama poa tukafika Kibaha dogo akauliza Moro bado ? Konda akasema bado ,tukafika chalinze dogo akauliza tena ,konda akawa mbogo mixa maneno ya shombo dogo kausha tukifika moro nitakwambia.

Basi safari ikasonga baada ya masaa mwili dogo akauliza tena moro bado ? hapo tunaitafuta Gairo konda akasema dah! Moro tushapita dogo , kidume nikageuka mbogo na magwanda yangu ya JKT nikamwambia dereva geuza gari turudi Moro abiria wakamaindi kinoma sema wakiangalia konda kazingua wakiniangalia pia mimi ni mwanausalama halafu mwili jumba niko na wenzangu wawili nimewazid ranks kwashingo upande suka kageuza gari mpaka moro.

Nikamwambia dogo moro ndio hapa ,dogo akasema asante bro akafungua begi lake akatoa chupa ya chai na mkate akaanza kugonga konda akamwambia shuka bas dogo akasema anaenda dom ila mama yake alimwambia akifika moro ndio anywe chai lunch atakula dom, unaambia gari zima macho yenye Jazba, hasira,husda,gubu, nongwa,dharau na uchungu yakaelekezwa kwangu hapo ndio ikabidi nizuge naenda kuchimba dawa nikakimbia nikawatext makamanda mizigo yangu nitaikuta kambini
 
Zamani kidogo tulitakiwa kwenda kusaga mashine ilikuwa mbali kidogo, nikajitia kujua nikamwambia dada tangu we fanya mambo mengine nitaenda mimi na baiskeli. Mama akasema huwezi wewe kubeba mahindi zaidi ya debe nikasema tulia uone. Ile nimetoka nyumbani nikaingia barabarani niliingia kwenye shimo nikala mweleka mkali, halafu watoto wa she ya msingi ndio walikuwa wanarudi kutoka shule na mimi kipindi hicho mimi niko form two. Walinicheka wale watoto jamani nahisi hadi leo wanakumbuka[emoji41]
 
Ulikua tunaenda Dodoma na foster tulipofika maeneo ya mbezi kuna dogo akamwambia kinda tukifika morogoro naomba uniambie kinda kama poa tukafika Kibaha dogo akauliza Moro bado ? Konda akasema bado ,tukafika chalinze dogo akauliza tena ,konda akawa mbogo mida maneno ya shombo dogo kausha tukifika moro nitakwambia
Basically safari ikasonga baada ya masaa mwili dogo akauliza tena moro bado ? hapo tunaitafuta Gairo kinda akasema dah! Moro tushapita dogo , kidume nikageuka mbogo na magwanda yangu ya JKT nikamwambia dereva geuza gari turudi Moro abiria wakamaindi kinoma sema wakiangalia konda kazingua wakiniangalia pia mimi ni mwanausalama halafu mwili jumba niko na wenzangu wawili nimewazid ranks kwashingo upande stika kageuza gari mpaka moro.
Nikamwambia dogo moro ndio hapa ,dogo akasema asante bro akafungua begi lake akatoa chupa ya chai na mkate akaanza kugonga konda akamwambia shuka bas dogo akasema anaenda dom ila mama yake alimwambia akifika moro ndio anywe chai lunch atakula dom, unaambia gari zima macho yenye Jazba, hasina,husda,gubu, nongwa,dharau na uchungu yakaelekezwa kwangu hapo ndio ikabidi nizuge naenda kuchimba dawa nikakimbia nikawatext makamanda mizigo yangu nitaikuta kambini

Daah hii kali [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hahaaaa dah...! Mkuu pole sana maana nami niliwahi kwenda kina kirefu cha ziwani aisee bahati mbaya nilikanyaga shimo la samaki nilikunywa vikombe vya kutosha walinitoa nimechoka,

Pia kisa kingine nipo na kaangu kanivusha mpaka kwenye jiwe lililokuwa kwenye kina kirefu cha maji wakati tumekaa pale ananiambia utaanguka kwenye maji mi namwambia najua kuogolea, aisee nikawa nachezea ukuku ulioota pale kwenye jiwe bahati mbaya ukanitelezesha nikaanguka kwenye maji aisee nilikunywa vikombe hapo nikaokolewa nilitoka mpole aisee...
 
Dada alipika wali home nikaukosoa vibaya mno kwa maneno mbofu mbofu tukiwa mezani nkawa nakula huku naongea tu wali m'baya m'baya,,nkawa naelekeza hiki kingefanyika hivi,kingefanyika vile Muda huo mimi tu ndio

natawala maongezi watu wengine mezani wote kimya,nilipomaliza mama akasema kesho CONTROLA upike wali kisha wewe dada utamsaidia kupika mboga,Kimoyo moyo nikasema ngojea mtajua kuwa mimi ndio mpishi konki

mama alivyotoa maagizo nikaitkia kisha nikasema kesho ntapika mimi,dada akaambiwa akimaliza kupika asigse kitu kingine chochote,basi kidume kesho ikafika nilichokipika Ki ukweli ilibidi nisingizie naumwa tumbo ghafla maana balaa lake nilijua lingekua kubwa

lakini pamoja na kusingizia naumwa,janja yangu mama aliishtukia alisema niitwe kisha nikalazimishwa kula ule wali wengine wote wakanunuliwa kiepe kuku,mimi niliambiwa ule wali wangu uishe Nikiula wiki sawa,nikiula mwezi sawa

ila ole wangu nitupe kile chakula,(bi kubwa angu n mkoloni sana) ki ukweli nilikula ule wali/uji sijui wiki nzima ile mpaka nikamaliza chakula chote,tangia Hapo sijawahi kosoa chakula chochote hata kama n kibaya vipi kapika mama ntilie

nikiona kitu kibaya namezea kimya kimya ila sikosoi mtu na kupitia ile adhabu nilijikuta nampenda yule dada angu kiasi kwamba ikawa nikirudi mahali,nikimkuta jikoni naenda kupka nae.

This is hilarious, I can't stop laughing!!
Ulikula siku ngapi huo wali?
 
Back
Top Bottom