Phillemon Mikael
Platinum Member
- Nov 5, 2006
- 10,557
- 8,673
Soma vizuri maelezo ya jamaa amesema Shirima amewauzia Wakenya 51% ya hisa za shirika.
Tupe data zilizokupelekea kusema haya, kumbuka huzi za fastjet ni jet engineNani kakudanganya? Wanaleta ndege ambazo zitakidhi mahitaji ya watanzania.
Na wako kibiashara zaidi sio magumashi kama ATCL
Kibiashara fast jet watakuwa Na uwezo wa kutoza bei Nafuu Zaidi ....Kwani wamechukua embadier Yenye engine power Na fuel consumption sawa Na Bombadier lakini Yao ina more searing space ....inabeba Abiria 105 ...kibiashara Hilo Ni Bao ...
Ina maana Katika Kila route watakayoshindana Na atc wao watakuwa Na advantage ya seats kwa asilimia 40%
Mfano kwa route zenye faida za Mbeya ,Arusha ,mwanza Kama atc wameweka nauli Kati ya 160,000 hadi 180,000 ...basi fast jet watakuwa Na Uwezo wa kupiga nauli ya 100,000 hadi 130,000 ...Na mapato watapata sawa ...SKY WARS
Bombadier za ATCL bado ni suluhisho kwa watanzania wengi kutokana na uwezo wake wa kutua hata viwanja visivyo vya lami na vyenye runway fupi.Huko Mpanda, ATCL itapata abiria wa kutosha ndugu yangu?
Tuwekeze katika safari za kimataifa angalau tunaweza kufanikiwa lakini sio kwa safari za ndani ya nchi.
Mkuu Salary Slip kumbe haya mambo ulianza zamani, ingebidi TCAA wakulipe kama expert opinion maker kuwasaidia kwenye regulations kuyazuia mashirika haya kuuwana kugombea kasungura kadogo.Bado naamini hakuna abiria wa kushindanisha kwa "afya" makampuni matatu au zaidi ya ndege hapa nchini kwa safari za ndani.
Kama waliporomoka kiuchumi wakati ATCL hai-operate, leo hii wakianza kugawana abiria hali itakuwaje?
Mtafakari sana kwanini wanasema ATCL ifike kule ambako wao hawafiki(Mpanda,Musoma n.k).
Swali hapa ni je,sababu zinazowafanya wao wasifike huko haziwezi kuwafanya ATCL nao wasifike?Nani anapenda hasara?
Je,huu si mwanzo wa kubanana katika destination chache tu?
Unafikiri ni nini kitafuata hapo?
ATCL iwekeze zaidi katika safari za kimataifa kwa mtazamo wangu kama tunataka kufanikiwa.
.
Mkuu Phillemon Mikael, thanks for this, kiukweli its sad!, ila kwenye data, ndege ni 10, na sharez za KQ ni 49% not 51% hivyo Shirima was still the majority shareholder angeweza kuuzuia uhuni wa KQ lakini aliwaamini sana na kumuachia kila kitu Kioko.air Tanzania wamenunua ndege mpya ....Hawa Precision walishawahi kumiliki hadi ndege 20 ATR na kuna wakati ilikuwa ndio shirika pekee linalotufunika uchi ....bila precision KENYA airways wangetuonea sana ..
Walikuwa wanaenda vizuri hadi pale Kenya airways walipofanya mbinu chafu ya kuinunu ....hili ilitakiwa idara ya usalama igundue ......walinunua Precision halafu wakaanza kufanya mbinu chafu za kuiuwa ..
walichofanya walinunua hisa 51% za mzee Michael Shirima ....lakini baada ya kununua hawakuweka mtaji walioahidi na wakaanza kuhujumu route za Precison ...pia wakimtumia Meneja Mkenya Michael Kioko ..wakaingiza Precision kwenye mkataba wa kununua ndege 10 mpya toka ATR huku wakijuwa mtaji walioahidi hawajaweka ......
Mzee wa watu akaja kushituka too late ...akamuondoa meneja mgeni akamuweka meneja mzawa ......tena mwanamke ambaye amejtahidi sana kufukia hasara .....na naona karibuni nao wanakuwa vizuri ....
Ilibidi mzee shirima kuangukia kwa Wakenya kupata mtaji zaidi baada ya kuwa ombi lake la kupewa mkopo nafuu na serikali kukataliwa kwa sababu za kibinafsi na chuki tu .hata alipoamua kuuza share zingine Nairobi na Dar stock exchange ...watu hao hao wabaya wenye chuki kwa mzawa waliandika barua kwenye mashirika yaliotaka kununua hisa hasa ya hifadhi kuyakataza yasifanye hivyo ....hili nilisikia mwenyewe kwa masikio Mwenyekiti mmoja wa bodi za haya mashirika akiwa VIP lounge akimuambia mkubwa mmoja kuwa walipewa maelekezo mahsusi ya kutonunua hisa za precision ili kumkomoa Mzee Shirima .... , alikuwa anastahili mkopo kwakuwa alikuwa anasaidia sana serikali upande wa kubeba watalii ....na alistahili kukopa hakutaka bure ....au hata wangemdhamini ....huyu mzee anastahili tuzo kwa kuweza kusimama tena Kenya Airways tayari walikuwa wamemmaliza.