Ushindi wa Mayweather utata

Mgulwa umeongea sana tu ,ila kumbuka may hakwenda kufanya show game, na anamjua mpinzani wake sio wa kumpiga ko kirahisi, hivyo hata ile kumbatia yake ilikuwa mbinu ya kumuuzi tu pac. Na tukumbuke pac alijuwa anarusha ngumi nyingi sana, ila zinaishia kwenye gloves tu, may anarusha chache zinaingia kichwani kabisa, na pale kuna mitambo maalum ya kuhesabu points, hivyo hakuna upendeleo wowote. Kumbuka kuna kipindi pac alionyesha kuchoka kabisa, na alipotangazwa may kashinda, pac hakushangaa.
 
Anglia Hui mchanganuo.
 

Attachments

  • 1430654665391.jpg
    41.1 KB · Views: 362

Statistics hizi zitsaidia kuamua ni nani alistahili.
 
View attachment 248893
 
Mkuu kama Ndondi ni kujilinda,kumkimbia adui na kumkukumbatia alafu unashinda,hata mimi naweza kuwa bondia mzuri.
 
Yashaisha watu wameingiza mpunga wao.
Tugange yajayo. Kesho tuone dollar ni shi ngapi maana hawachelewi kusema hela zilienda kwa May baada ya ushindi

Asante Mkuu Kwa Muongozo
 
Nimemsikia Man Pac BBC amedai hajaridhika na matokeo, anaamini amepunch zaidi na nyingi zilikuwa on target, pia ataproduce DVD watu wajionee wenyewe.. mgulwa tusubiri arelease hiyo dvd yake afu tuwajie juu mateam may
 
Last edited by a moderator:
Ngumi za mitaani ni tofauti na za mashindano. Tupate uchambuzi wa pambano wa wanaojua ngumi kama Abdallah Yasin. Nadhan leo atahojiwa na Clouds .
 
Nimemsikia Man Pac BBC amedai hajaridhika na matokeo, anaamini amepunch zaidi na nyingi zilikuwa on target, pia ataproduce DVD watu wajionee wenyewe.. mgulwa tusubiri arelease hiyo dvd yake afu tuwajie juu mateam may

Yaani iko hivyo tu,

Kilichofanyika ulingoni na matokeo! ni tofauti!

Ila na wasi wasi wacheza kamari/watu wakubet wanaweza kua wamehusika ktk upangaji wa matokeo!
Nawaza mengi aseee!

Najaribu kumtetea may weather akilini ila bado nakosa sababu!

Wamemuonea sana PAC
Pac kafanya kazi kubwa..
Katupa nyingi..
Kamkong'ota nyingi!

Sioni hakika sioni ni wapi m.weather alimzidi Pac!

Ila wachambuzi wa mambo walisema!
Kwa thamani ya pambano lile,ushindi kwa pac ni kwa ko tu!

Kweli lisemwalo lipo!

Nimeshtushwa sana na takwimu za majaji!

Kama hawakuja nazo zile takwimu,
Basi wamechanganya
Points za m.weather kapewa PAC.
Points za PAC kapewa may.afu akaongezewa!

Wamemuonea sana! Hawana hata aibu!

Atoe iyo CD/DVD. Bt hata asipotoa,kila jicho lilioona pambano litakiri kweli PAC kadhurumiwa matokeo.

Mungu atajamlipa hata mbinguni!

da!:thumbdown:
 
Last edited by a moderator:
Anglia Hui mchanganuo.

Hizi takwimu,kama hawakuja Nazo toka walikotoka..

Basi za may kapewa pac na za pac kapewa may afu na nyongeza!

Kiukweli/kiuungwana/kihaki bila takwimu hizi si za pambano lile,hata kama mchezo huujui sana,bado utauona udanganyifu mkubwa hapo kulinganisha na mchezo.

Ila sio mbaya matokeo hayatabadilika,ila ukweli utabaki palepale!
Kwamba mgeni/mnyonge/mshindi kadhurumiwa!
 

Haya mambo na Mbingu yanahusika vipi? Acheni kuchanganya mafaili.
 
Haya mambo na Mbingu yanahusika vipi? Acheni kuchanganya mafaili.

Sasa unadhani haki ataipata wapi?

Maana tunaongea tu ila hata tujaze dunia kwa maneno matokeo hayatabadilika!

Tunachofanya waungwana ni kumuachia mungu!
 
Mambo ya ki freemason tu..maywether yupo kwenye kingdom hakutakiwa aangushwe this tyme ila muda ukifika man pac akikubali kuwa raia wa us naye atapewa hiyo kingdom..secret behind the scene and mission was planned
 
Sasa unadhani haki ataipata wapi?

Maana tunaongea tu ila hata tujaze dunia kwa maneno matokeo hayatabadilika!

Tunachofanya waungwana ni kumuachia mungu!

Ya kaisari mwachie kaisari.
 
Utake usitake TMT kapiga ngumi za akiri kuliko PAC alikua anajipigia paspo malengo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…