Gulf Streamer
Member
- Aug 7, 2014
- 90
- 40
Dhumuni la post hii ni kutaka kupata ushuhuda wa mafanikio katika biashara na vikwazo mbali mbali tunavyovipitia katika majukumu yetu ya kibiashara.
Mpo waajiriwa mnaojihusisha na biashara kama part time, wengine mliacha kazi ili mjiajiri wenyewe kama wafanyabishara, Mpo ambao maisha yenu ni biashara tu. Tungependa kusikia kutoka kwenu, mafanikio na vikwazo mlivyokumbana navyo.
Kuna mambo mengi sana jamii ingependa kuyajua kuhusu biashara unayoifanya au uliyowahi ifanya, mpo ambao mnafanya biashara nje ya Tanzania, mpo mliokumbana na dhoruba ya wafanyakazi wenu kukimbia na mitaji yenu, mpo ambao wafanyakazi wenu walianzisha biashara kama zenu baada ya kupata ujuzi toka kwenu, mpo ambao mnakutana na hali ya ushirikina katika uendeshaji wa biashara zenu, Je partners katika biashara yako walikuwa msaada au mzigo kwako? Je ulifanikiwa katika kilimo, au ulikutana na changamoto gani? Mpo mnaofuata bidhaa China na nchi nyingine duniani, toeni uzoefu wenu uwasaidie wengine? Yapo mengi, kama mfanya biashara tungependa sikia toka kwako.
Nimeamua anzisha post hii ili iwe msaada kwa watu wanaopenda kujifunza kabla ya kuingia katika biashara, usije ukajikuta unafanya makosa yale yale yaliyofanywa na watangulizi wako.
Mpo waajiriwa mnaojihusisha na biashara kama part time, wengine mliacha kazi ili mjiajiri wenyewe kama wafanyabishara, Mpo ambao maisha yenu ni biashara tu. Tungependa kusikia kutoka kwenu, mafanikio na vikwazo mlivyokumbana navyo.
Kuna mambo mengi sana jamii ingependa kuyajua kuhusu biashara unayoifanya au uliyowahi ifanya, mpo ambao mnafanya biashara nje ya Tanzania, mpo mliokumbana na dhoruba ya wafanyakazi wenu kukimbia na mitaji yenu, mpo ambao wafanyakazi wenu walianzisha biashara kama zenu baada ya kupata ujuzi toka kwenu, mpo ambao mnakutana na hali ya ushirikina katika uendeshaji wa biashara zenu, Je partners katika biashara yako walikuwa msaada au mzigo kwako? Je ulifanikiwa katika kilimo, au ulikutana na changamoto gani? Mpo mnaofuata bidhaa China na nchi nyingine duniani, toeni uzoefu wenu uwasaidie wengine? Yapo mengi, kama mfanya biashara tungependa sikia toka kwako.
Nimeamua anzisha post hii ili iwe msaada kwa watu wanaopenda kujifunza kabla ya kuingia katika biashara, usije ukajikuta unafanya makosa yale yale yaliyofanywa na watangulizi wako.