KERO Ushuru wa maegesho umegeuka kuwa wizi usiotumia mabavu wa serikali dhidi wananchi wake

KERO Ushuru wa maegesho umegeuka kuwa wizi usiotumia mabavu wa serikali dhidi wananchi wake

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Mzalendo Uchwara

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2020
Posts
4,437
Reaction score
13,836
Tangu utaratibu wa ushuru wa maegesho uondolewe TARURA na kupelekwa katika halmashauri umegeuka kuwa wizi wa wazi wa serikali dhidi ya wananchi wake.

Mawakala wa halmashauri wanaohusika na kukusanya ushuru huo kwa kuvitoza vyombo vya moto vilivyoegeshwa wanafanya hivyo kimyakimya bila kuacha risiti yoyote lakini pia mwenye chombo cha moto hapati hata SMS ya kumtaarifu kuwa ameandikiwa ushuru wa maegesho.

Matokeo yake huyu mwananchi anashtuka ana madeni makubwa ambayo haujui yametoka wapi, na mbaya zaidi amepigwa na faini za kiendawazimu juu yake.

Utaratibu huu wa kijambazi kabisa pia unawawezesha mawakala wa halmashauri wanaotumiwa kukusanya ushuru huo kutoza ushuru mara nyingi watakavyo, yaani anaweza kuwa amelala zake nyumbani anarudia kuzitoza namba za magari aliyoyatoza jana.

Lakini pia mmiliki wa chambo anaweza kuwa amepaki sehemu moja kwa dakika 20 kisha akakuta umeandikiwa hata mara tano, na atakuja kujua kuwa uliandikiwa ikiwa ‘too late’ maana hakuna cha risiti wala SMS yoyote kumtaarifu kuwa ameandikiwa ushuru wa maegesho.

Kero hii imekithiri sana kwenye halmashauri za jiji la Dar es Salaam, labda kutokana na pressure za kufikia malengo ya makusanyo ya mapato.

TAMISEMI liangalieni hili, halmashauri zenu na mawakala wao wa kukusanya ushuru wanaichafua serikali kwa huu ujambazi wa mchana kweupe wanaoufanya.
 
Hao watoza ushuru ni majambazi wasiodhuru.
Sehem hiyohiyo wanakataza kushusha mzigo ila mwenye hela anashusha hapohapo, bidhaa ile ile, eneo lilelile na gari yenye ukubwa uleule.
 
Hao watoza ushuru nimajambazi wasio dhuru. Unapatana nao.
Sehem hiyo hiyo wanakataza kushusha mzigo ila mwenye hela ana shusha hapohapo bidhaa ile ile,eneo lilelile na gari yenye ukubwa uleule.
Wana mambo ya hovyo kwakweli. Siku watu wakiangalia madeni yao kwenye system watakuwa shocked.
 
Juzi niko Lumumba nimetoka kufata gari ya jamaa yangu niko naweka urembo pale wakaja jamaa wa ushuru wa maegesho.

Nikawasogelea wakascan namba ya gari wakasema inadaiwa 1,300. hiyo ilikuwa tarehe 01 Novemba, gari ilisajiliwa tarehe 31 Oktoba na iliingia Tanzania mwezi Juni.

Lile deni ni la tarehe 09 Januari, 2024 kipindi ambacho hiyo gari ipo Japan na hiyo namba ya usajili haijawahi kuwepo.

Hii nchi ina maajabu sana, tulibishana na jamaa mpaka nikawatolea faili la gari nao wakabaki wanacheka
 
Tangu utaratibu wa ushuru wa maegesho uondolewe TARURA na kupelekwa katika halmashauri umegeuka kuwa wizi wa wazi wa serikali dhidi ya wananchi wake.

Mawakala wa halmashauri wanaohusika na kukusanya ushuru huo kwa kuvitoza vyombo vya moto vilivyoegeshwa wanafanya hivyo kimyakimya bila kuacha risiti yoyote lakini pia mwenye chombo cha moto hapati hata SMS ya kumtaarifu kuwa ameandikiwa ushuru wa maegesho.

Matokeo yake huyu mwananchi anashtuka ana madeni makubwa ambayo haujui yametoka wapi, na mbaya zaidi amepigwa na faini za kiendawazimu juu yake.

Utaratibu huu wa kijambazi kabisa pia unawawezesha mawakala wa halmashauri wanaotumiwa kukusanya ushuru huo kutoza ushuru mara nyingi watakavyo, yaani anaweza kuwa amelala zake nyumbani anarudia kuzitoza namba za magari aliyoyatoza jana.

Lakini pia mmiliki wa chambo anaweza kuwa amepaki sehemu moja kwa dakika 20 kisha akakuta umeandikiwa hata mara tano, na atakuja kujua kuwa uliandikiwa ikiwa ‘too late’ maana hakuna cha risiti wala SMS yoyote kumtaarifu kuwa ameandikiwa ushuru wa maegesho.

Kero hii imekithiri sana kwenye halmashauri za jiji la Dar es Salaam, labda kutokana na pressure za kufikia malengo ya makusanyo ya mapato.

TAMISEMI liangalieni hili, halmashauri zenu na mawakala wao wa kukusanya ushuru wanaichafua serikali kwa huu ujambazi wa mchana kweupe wanaoufanya.
Hii dhana kwamba kila mwenye gari ni Tajiri😅😅
 
Juzi niko Lumumba nimetoka kufata gari ya jamaa yangu niko naweka urembo pale wakaja jamaa wa ushuru wa maegesho.

Nikawasogelea wakascan namba ya gari wakasema inadaiwa 1,300. hiyo ilikuwa tarehe 01 Novemba, gari ilisajiliwa tarehe 31 Oktoba na iliingia Tanzania mwezi Juni.

Lile deni ni la tarehe 09 Januari, 2024 kipindi ambacho hiyo gari ipo Japan na hiyo namba ya usajili haijawahi kuwepo.

Hii nchi ina maajabu sana, tulibishana na jamaa mpaka nikawatolea faili la gari nao wakabaki wanacheka
Hahaha
 
Kibongo bongo, wamiliki wa magari (yawe ni kwa ajili ya matumizi binafsi, au yale ya biashara) hawana tofauti na ng'ombe wa maziwa.
 
Back
Top Bottom