Usia unapokinzana na uhalisia kwenye mirathi

Usia unapokinzana na uhalisia kwenye mirathi

moghaka

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2011
Posts
252
Reaction score
143
Nawasalimieni wana Jf katika jukwaa hili, naomba kuuliza kama kichwa cha habari kilivyo ! !
Mfano; Marehemu alikuwa na wake wawili kwa muda mrefu wakati wa uhai wake, yeye na familia yake kwa ujumla wanazo mali kikubwa zidi ni nyumba tano, na katika kuchangia kwenye utafutaji wake wote walichangia sawa kwa sawa na wazijenga sawa kwa sawa,
Katika kuolea ndani ya ndoa mke mkubwa ana miaka 42 na mke mdogo 35 ya ndoa hadi mme wao kufariki.
Baada ya kufa usia aliouacha ni kama ufuatavyo:
Mke mkubwa apewe nyumba mbili tu na mke mdogo apewe nyumba tatu, n huo usia umekamilika kwani una ushahidi wa kutosha na maandishi mbele ya wakili.

TATIZO: Mke mkubwa anadai hakutendewa haki …. …. …. …. NI NINI MAAMUZI SAHIHI ?
TUFUATE USIA WA MAREHEMU AU KUUPUUZA NA KUWAGAWIA SAWA KWA SAWA ?..
 
hapo mahakama ya kadhi ni muhimu...

ila km ni sheria za mahakama za kawaida wote watapata 50/50 isipokuwa km mahakama itazingatia uwiano wa ukubwa wa familia hususani idadi ya watoto...

pia km suala hilo litatatuliwa kifamilia namaanisha hakimu akiwa mwenyekiti wa ukoo au familia basi wosi wa marehemu utazingatiwa mkuu...

ni hayo km una maswali karibu
 
hapo mahakama ya kadhi ni muhimu...

ila km ni sheria za mahakama za kawaida wote watapata 50/50 isipokuwa km mahakama itazingatia uwiano wa ukubwa wa familia hususani idadi ya watoto...

pia km suala hilo litatatuliwa kifamilia namaanisha hakimu akiwa mwenyekiti wa ukoo au familia basi wosi wa marehemu utazingatiwa mkuu...

ni hayo km una maswali karibu

umejuaje kama mahakama ya kadhi ni muhimu hapo, embu nifafanulie, maana hakuna sehemu inayoonesha kuwa marehemu ni muislam hata kama alikuwa na mke zaidi ya mmoja, huenda ikawa ni ndoa za kimila je?
 
1. wosia kama umefuata taratibu zote basi NI LAZIMA UHESHIMIWE,
2. je, marehemu hakuacha watoto?
3. kama aliacha, je kila mjane aliachwa na watoto wangapi (taja na jinsia zao)
4. Je, marehemu na wajane walikuwa wamefunga ndoa za aina gani?.


naomba ujibu hayo maswali hapo juu kwanza, ndo tujue nafasi ya huo wosia.
 
1. wosia kama umefuata taratibu zote basi NI LAZIMA UHESHIMIWE,
2. je, marehemu hakuacha watoto?
3. kama aliacha, je kila mjane aliachwa na watoto wangapi (taja na jinsia zao)
4. Je, marehemu na wajane walikuwa wamefunga ndoa za aina gani?.


naomba ujibu hayo maswali hapo juu kwanza, ndo tujue nafasi ya huo wosia.
mke mkubwa watoto 4 me 2 na ke 2......mke mdg watoto 5 me 2 ke 3,,,,
Ndoa za kimila tu,,,,

NAOMBA JIBU
 
mke mkubwa watoto 4 me 2 na ke 2......mke mdg watoto 5 me 2 ke 3,,,,
Ndoa za kimila tu,,,,

NAOMBA JIBU

fateni wosia mtu anapopandika wosia ameamua mali zake zigawanywe kama wosia unavyosema
 
Wosia wa marehemu ukifuata taratibu zote, mahakama haitakiwi kwenda nje ya kilichoelezwa kwenye wosia. hivyo basi, kwa kuwa wosia ni valid, malalamiko ya mke mkubwa hayaonekani katka jicho la sheria.
the will shall prevail
 
Back
Top Bottom