Usichague kazi, soma hapa nikutie moyo

Usichague kazi, soma hapa nikutie moyo

hesalieyo

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2012
Posts
378
Reaction score
380
Naomba niwatie moyo wote wanaotafuta kazi bila mafanikio .

Wakati nimemaliza degree yangu miaka ya nyuma kidogo, nilikaa kwa muda wa miaka miwili bila kupata kazi, Kila ninapopeleka application siitwi, ila nakumbuka niliitwa katika shirika moja kubwa tu lisilo la kiserikali kwa ajili ya interview.

Nilifika kufanya usahili na tulikuwa Kama watu Saba na walikuwa wanataka Mtu mmoja katika nafasi tuliyoomba.

Nakumbuka nilijiandaa Sana katika intervew hiyo, na niliamin lazima nitaitwa kuanza kazi, kutokana na jinsi nilivyojibu maswali yangu.

Nilisubiri kuitwa kazini bila mafanikio, baada ya Kama mwezi nikarudi kuuliza vipi Kama washaita, nikapewa jibu la tayari mtu ashaanza kazi, niliumia sana mpaka niliokuwa naongea nao walinionea huruma.

Mmoja wa niliokuwa naongea nao akanambia Kama ungeweza Kuna nafasi moja ila sijui kama unaweza kuifanya ni office attendance na mshahara ni laki tatu.

Kwa jinsi nilivyokuwa na uhitaji wa kazi na kwamba nimesota nyumbani bila kazi na maisha ya kukaa nyumban yalivyo magumu nikamwambia niko tayari kuifanya mpaka wakashangaa nikaambiwa nirudi kesho yake kuanza kazi.

Wakuu nilianza kazi Kama muhudumu wa office bila aibu yoyote japo yataka moyo, lakini nilifanya tena kwa ufanisi mkubwa, nilikuwa na adabu, Kila aliyenituma wengine niliwazidi elimu, nilienda , watu walinipenda na kunisifia ufanyaji wangu kazi.

Baada ya miezi mitatu amini usiamini niliajiriwa hapo kwa nafasi inayoendana na elimu yangu, nilishukuru sana na kuamini sometimes Mungu anataka ujishushe ili akuinue.

Hivyo, nakutia moyo ndugu yangu unaetafuta kazi sometimes jishushe ile Mungu akuine.

Najua uzi ni mrefu ila kuna cha kujifunza.
 
Ukiona mtu unashindwa kufanya jambo lenye manufaa kwako, unaona aibu ujue wewe ni zwazwa.

Kazi yoyote hata kama ya kutapisha vyoo ndio rafiki yako - itakulipia bills, itakununulia chakula, itakupeleka hospitali au hata kusaidia wanao.

Siyo Hao WANAOKUCHEKA na KUKUPIGA MAJUNGU !
 
Shida siku hizi hata kuwapata hao watu wa kukuambia kuna kazi ya usafi hawapo.

Yaani kwa hali ilipofikia sina na sitowahi kuchagua au kubagua kazi yoyote ile ya halali
 
Ukiona mtu unashindwa kufanya jambo lenye manufaa kwako, unaona aibu ujue wewe ni zwazwa.

Kazi yoyote hata kama ya kutapisha vyoo ndio rafiki yako - itakulipia bills, itakununulia chakula, itakupeleka hospitali au hata kusaidia wanao.

Siyo Hao WANAOKUCHEKA na KUKUPIGA MAJUNGU !
Nakumbuka nilishawahi kwenda kwenye interview moja ya kazi ya kuzibua vyoo. Walitaka mtu mmoja na tukaomba watu 138 walitaka uwe umemaliza form four tu lakini mpaka watu wa degree walikuwepo.

Maskini ya mungu na hii pia sikupata!
 
Nakumbuka nilishawahi kwenda kwenye interview moja ya kazi ya kuzibua vyoo. Walitaka mtu mmoja na tukaomba watu 138 walitaka uwe umemaliza form four tu lakini mpaka watu wa degree walikuwepo.

Maskini ya mungu na hii pia sikupata!
Mimi Nilienda Kutafuta Kazi CarWash baada tu ya kuhitimu. SIKUPATA.

Hapo ndio unajifunza kuheshimu kazi za watu na ndio utaujua maana ya ule msemo wa:

What do you Do for a living?

Ukifika muda wa lunch, ukitakiwa unga huwezi kupika "Karatasi Lako La Degree ya GPA 4.4"
 
Yaani si ajabu kusikia mtu anatafuta kijana wa kumsaidia kazi zake wakati ndio hivi tunalia tu hata mtaji wa kuweza kujiajiri hakuna.
Mimi Nilienda Kutafuta Kazi CarWash baada tu ya kuhitimu. SIKUPATA.

Hapo ndio unajifunza kuheshimu kazi za watu na ndio utaujua maana ya ule msemo wa:

What do you Do for a living ?

Ukifika muda wa lunch, ukitakiwa unga huwezi kupika "Karatasi Lako La Degree ya GPA 4.4"
 
Nakumbuka nilishawahi kwenda kwenye interview moja ya kazi ya kuzibua vyoo. Walitaka mtu mmoja na tukaomba watu 138 walitaka uwe umemaliza form four tu lakini mpaka watu wa degree walikuwepo.

Maskini ya mungu na hii pia sikupata!
Nimecheka kama mazuri vile daah
 
Naomba niwatie moyo wote wanaotafuta kazi bila mafanikio .

Wakati nimemaliza degree yangu miaka ya nyuma kidogo, nilikaa kwa muda wa miaka miwili bila kupata kazi,Kila ninapopeleka application siitwi,ila nakumbuka niliitwa katika shirika moja kubwa tu lisilo la kiserikali kwa ajili ya interview.

Nilifika kufanya usahili na tulikuwa Kama watu Saba na walikuwa wanataka Mtu mmoja katika nafasi tuliyoomba.

Nakumbuka nilijiandaa Sana katika.intervew hiyo, na niliamin lazma nitaitwa kuanza kazi,kutokana na jinsi nilivyojibu maswali yangu.

Nilisubiri kuitwa kazini bila mafanikio, baada ya Kama mwezi nikarudi kuuliza vipi Kama washaita , nikapewa jibu la tayari mtu ashaanza kazi,niliumia Sana,mpaka niliokuwa naongea nao walinionea huruma.

Mmoja wa niliokuwa naongea nao akanambia Kama ungeweza Kuna nafasi moja ila.sijui.kama unaweza kuifanya ni office attendance na mshahara Ni laki tatu.

Kwa jinsi nilivyokuwa. Na uhitaji was kazi,na kwamba nimesota nyumbani bila kazi ,na maisha ya kukaa nyumban yalivyo magumu nikamwambia Niko tayari kuifanya mpaka wakashangaa nikaambiwa nirudi kesho yake kuanza kazi.

Wakuu nilianza kazi Kama muhudumu wa office bila aibu yoyote japo yataka moyo,lakini nilifanya Tena kwa ufanisi mkubwa,nilikuwa na adabu,Kila aliyenituma wengine niliwazidi elimu,nilienda ,watu walinipenda na kunisifia ufanyaji wangu kazi.

Baada ya miezi mitatu amini usiamini niliajiriwa hapo kwa nafasi inayoendana naelimu yangu, nilishukuru Sana na kuamini sometimes mungu anataka ujishushe ili akuinue.

Hivyoo nakutia moyo ndugu yangu unaetafuta kazi sometimes jishushe ile Mungu akuine. Najua uzimni mrefu ila.kuna Cha kujifunza.
Fact mkuu
 
Mkuu
Ukiona mtu unashindwa kufanya jambo lenye manufaa kwako, unaona aibu ujue wewe ni zwazwa.

Kazi yoyote hata kama ya kutapisha vyoo ndio rafiki yako - itakulipia bills, itakununulia chakula, itakupeleka hospitali au hata kusaidia wanao.

Siyo Hao WANAOKUCHEKA na KUKUPIG

Mkuu unajua watu wakiwa.chuoni wanajua maisha baada ya chuo Ni rahisi Sana,yaan wanajua ukimaliza degree kazi unapata popote, Mimi Nina rafiki yangu tangu tumemaliza chuo hajawahi kupata kazi sehemu yoyote ata ya kujitolea , na asingeweza kufanya kazi Kama hiyo ya uhudumu ofisini kwa jinsi alivyo sister duu, na alinishangaa Sana mm kukubal hiyo kazi.
Mpaka ninavyoongea hapa ashavunja urafiki na mm, hataki ata mawasiliano na mimi
 
Kuna watu hawaelewi umuhimu wa kujishusha

Una degree hutaki kuosha magari, utakutana vipi na kiboba akupe mchongo?

Una degree hutaki kushona/ku shine viatu, utakutana vipi na Afisa mwajiri akupe kazi?
 
Kuna watu hawaelewi umuhimu wa kujishusha

Una degree hutaki kuosha magari, utakutana vipi na kiboba akupe mchongo?

Una degree hutaki kushona/ku shine viatu, utakutana vipi na Afisa mwajiri akupe kazi?
Ni kweli mkuu ,japo yataka moyo , Mimi nilikuwa natumwa Hadi na watu niliowazidi elimu ,kiuninadamu unajiskiaje vibaya lakini ndiyo inabidi ili ufikie lengo lako
 
Back
Top Bottom