Usidhani shetani ni mdogo kama unavyofikiri

Usidhani shetani ni mdogo kama unavyofikiri

Frumence M Kyauke

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2021
Posts
630
Reaction score
1,262
Kuna baadhi ya watu wanadhani shetani ni jambo dogo, ile ni nguvu kubwa iliyoshinda binadamu wote. Utakapojaribu kuingia kwenye ugomvi na yeye ndipo utatambua kuwa unajaribu kupigana na jambo usiloweza. Kwa reference fupi, wapo mitume waliojaribu kupambana naye wakaishia kupata adhabu kali zisizoelezeka.

Wakwanza ni Yesu, mwana wa Mungu alipojaribu kupambana nae aliishia kusulubishwa. Ayubu mcha Mungu alipata kipigo kikali sana alipomcha Mungu, Adam na Hawa pamoja na utashi wao wote walitiwa kwenye 18, mitume ikiwemo Stephano walipigwa na mawe mpaka kufa walipoingia kwenye vita na shetani.

Unaposema unataka vita na shetani labda pepo ila sio shetani aliyemsulubisha Yesu, vinginevyo utaishia kuchapwa kipigo kitakatifu.
Jiulize je, kama Yesu na nguvu zake zote alisulubishwa vibaya sana wewe atakufanyia jambo gani?
 
Kuna baadhi ya watu wanadhani Shetani ni jambo dogo, ile ni nguvu kubwa iliyoshida binadamu wote...

Kwa Yesu, shetani alidhani amemkomoa ila alitimiza maandiko. .. . ilikuwa lazma mwana wa Adamu aje aishi kama mwanadamu na asubulubiwe...afanyike laana ..aimwage damu yake isiyo na hatia kwa ajili ya utakaso wa kila mwanadamu mwenye mwili duniani.. afe azikwe na afufuke..

Msalaba una nguvu kuliko mauti.
 
Kuna baadhi ya watu wanadhani Shetani ni jambo dogo, ile ni nguvu kubwa iliyoshida binadamu wote, utakapojaribu...
Shetani hana mamlaka dhidi ya Roho (UHAI)ya mtu. Shetani anaishia kwenye kudhuru mwili tu. Na mwili ni Mavumbi (Udongo)na Mavumbini Utarudi (Kifo).

Mkuu, Wote uliowataja hapo juu, mwishoni waliibuka washindi na Shetani unayemfagilia aliaibika mno.
 
Kwa Yesu, shetani alidhani amemkomoa ila alitimiza maandiko. .. . ilikuwa lazma mwana wa Adamu aje aishi kama mwanadamu na asubulubiwe...afanyike laana ..aimwage damu yake isiyo na hatia kwa ajili ya utakaso wa kila mwanadamu mwenye mwili duniani.. afe azikwe na afufuke..

Msalaba una nguvu kuliko mauti.

Na wala hakuwa shetani ni wanadamu tu na tamaa zao za madaraka, walidhani atawakwapua madaraka.
 
Yesu Kristo ndiye aliyeumba vyote akiwepo shetani leo hii atakuwaje na nguvu kuliko Yesu?
Ni kweli mkuu shetani hawezi kuwa na nguvu kuliko Yesu, lakini iko hivi:
Yesu kimwili ni Binadamu i.e alikua, aliishi sawa kama na sisi tunavyoishi.
Lakini Kiroho, Yesu ni Mungu na ndo maana ndiye aliyeumba vyote na Shetani analifahamu hilo na kukiri hivyo.

Kwa mantiki hiyo, Shetani alipambana na Yesu lakini ilikuwa ni kimwili zaidi na aliishia kuudhuru mwili.Hakuweza na Alishindwa kabisa Kiroho. Yesu alifufuka na kuvaa mwili usioharibika tena.
 
Shetani hana mamlaka dhidi ya Roho (UHAI)ya mtu. Shetani anaishia kwenye kudhuru mwili tu. Na mwili ni Mavumbi (Udongo)na Mavumbini Utarudi (Kifo).
Mkuu, Wote uliowataja hapo juu, mwishoni waliibuka washindi na Shetani unayemfagilia aliaibika mno.
Mtu amepigwa mawe mpaka kufa alafu anasema ameshindaje?
 
Back
Top Bottom