Usidhani shetani ni mdogo kama unavyofikiri

Shetani ni roho hakuna asichojua kuhusu mambo ya rohoni,
 
Mi nashangaaga sana watu wanaomtukana shetani, wakimsema na kumchora vibaya. Shetani anapaswa kuheshimiwa.
 
Bakora bado zinatembea na mitume wanachapika sawa sawa mpaka Papa Benedicto wa XVI akaamua kujiuzulu
 
Hizo nguvu unazosema alikuwa nazo zilikuwa wakati ule wa agano lile.... YESU aliposurubiwa msalabani alikufa akaenda kuzimu akamnyang'anya shetani nguvu zile unazosema na ufunguo huku akiichukua hati ya mashitaka na kumfunga huko kuzimu na minyororo.

Kwa hiyo sasa hivi shetani hana huo uwezo unaosema ni maajenti wake ndio wanaotesa wanadamu unapotumia silaha za imani likiwamo jina la YESU KRISTO.... Wanakaa mbali nawe. Kwa hiyo silaha kibwa ya shetani kipindi hiki ni Uongo ama udanganyifu kama vile alivyofanya kwa adamu kuudanganya ulimwengu kuingia dhambini na hapo ndipo anapopata nafasi ya kukushughulikia maana dhambi ni uasi na yoyote afanyae uasi ni adui wa MUNGU.

SIKU INAKUJA YESU ATALICHUKUA KANISA LAKE NA YULE SHETANI ATAFUNGULIWA WALE WALIOBAKI PAMOJA NAE WATAKIONA CHA MOTO.
 
Mitume wangapi wanafumwa wakiwa na makahaba ama niwataje kwamajina?, walevi, wezi, wauwaji? Nguvu walizo nazo ziko wapi?
 
Shetani baba Lao binadamu kamwe humuwezi yupo enzi tangu na tangu naam amewashinda wengi mapadre wanazini masheikh wanabaka viongozi wa serikali wanaiba kura waumini wanauwana binadamu hawana wema kuna wachawi wazinifu wauwaji wala utu je nani atapona mungu ametengeneza kitu ambacho kinawafuasi wengi kushinda yeye watu wanafata dini kwakuwa wamezaliwa nazo tu lakini hawana hata moja wanalofata katika kama hakuna duniani asiye na dhambi basi shetani baba lao
 
Mtume akijifanya yeye mcha Mungu basi mshedede unamsimama mpaka anakula kondoo, vipo visa vingi sana vya kuhusu viongozi wa dini kufanya mambo ya ajabu sana, iwe kwa siri au faragha, wanaojulikana ni wachache sana wengi wao wanafanya kwa siri
 
Story hizo za kutunga zimekuja au zimewaingia wakristo wengi baada ya kukosa uhakika na dini yao...

Shetani/iblisi ni kiumbe aliyetezwa nguvu na Muumba wake na siku ya kiyama moto wa jahanamu unamsubiri.. kwa mantiki yako hiyo kana kwamba unataka kusema kuwa shetani au ku declare kabisa ushetani wako.
Hakika vitimbi vya shetani ni dhaifu ikiwa utataka hifadhi kwa Mola mbingu na nchi.

Nikikuletea ushahidi mambo mengi aliyowahi kushindwa shetani utayasadiki? Kupitia manabii na mitume na watu waliojikurubisha kwa muumba wao?
 
Shetani hashindwi, hizo ni habari za binadamu wanaojiaminisha na wanaojaribu kukimbia ukweli wa Shetani.

Mara nyingi watu wanashindwa kutofautisha kati ya Shetani na mapepo, mapepo ni vitoto vidogo ambavyo ndivyo watu wana deal navyo kila siku lakini Shetani mwenyewe akishuka katika ardhi ya Tanzania basi hii nchi itageuka kichwa chini miguu juu, mimi naongea kwa reference

Yesu pamoja na nguvu zote alichapwa vibaya sana je wewe binadamu utachapikaje utakapojaribu kuingia nae katika vita?
 
Ni kweli kabisa na kwa kuijua nguvu ya Yesu kiroho alianza kulia na kusononeka pale alipofikia hatua ya kumwomba Yesu kwa kupiga magoti na kusema "Bwana, usituangamize bali tuamuru twende kwenye lile kundi la nguruwe." Marko 5:1-14
Wale ni vijakazi wake, hakuwa shetani mwenyewe.
 
Wewe hujiulizi ana nguvu kiasi gani mpaka amtandike yesu na amwambie kama wewe ni mtoto wa Mungu basi jishushe msalabani?
Usidhani ni kitu kidogo hiki, kama yesu alichapwa kiasi kile basi binadamu utamumunywa kama pipi
Hakuna maandiko kwenye Biblia yanayosema 'kama wewe ni mwana wa Mungu jishushe msalabani".
 
Yesu alishinda kijana. Thats why alifufuka after 3 dys
 
Yesu Kristo ndiye aliyeumba vyote akiwepo shetani leo hii atakuwaje na nguvu kuliko Yesu?
Yesu kaumbaje vitu wakati Yesu kabla hajazaliwa na bikira Maria kulikua na maisha sasa inamaana aliumba vitu vyote then akafa halafu akazaliwa tena au kwa kwa urahisi tu inamaana Adam aliumbwa na Yesu wakina Ibrahim ahaaa dini zinachanganya halafu hao waliotuletea hawana habari
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…