Usiegemeze maisha yako kwenye Chama cha siasa

Usiegemeze maisha yako kwenye Chama cha siasa

Manyanza

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2010
Posts
16,464
Reaction score
35,629
Wadau!
Kama kichwa cha huu uzi kinavyosomeka hapo juu.

Swali la kujiuliza 🤔

Kwa nini binadamu aliyeifanyia makubwa Chadema, aliyejenga wasifu wa kipekee na uliotukuka kwenye siasa za upinzani na kupigania demokrasia Tanzania, Freeman Aikaeli Mbowe, jana alfajiri aliangushwa aliyekuwa msaidizi wake, Tundu Antipas Lissu?

Majibu ya swali hilo yanajibiwa na hoja mbili hizi hapa chini

1. Chama cha siasa kina mapenzi ya majira.
Leo kitakupenda sana, kesho kitakupuuza, keshokutwa kitakuchukia. Chama cha siasa kinaweza kukupamba kama shujaa asubuhi, jioni kikatangaza kuwa adui, usiku kikakufukuza.

2. Wanasiasa hukosea kuegemeza maisha yao kwenye vyama vyao.

Chama cha siasa hakina utu, kinaweza kukung'ang'ania mfe wote kisiasa, kama Prof Ibrahim Lipumba na Cuf, au kikakuua kwanza, kisha chenyewe kikaenda kufa sehemu nyingine, mithili ya James Mbatia na NCCR-Mageuzi.

Fanya siasa kwa akili. Wanachama na viongozi wenzako kwenye chama, siyo familia yako.
 
Mama Tanzania amekuwa under utilized (Hajatumika vya kutosha)

Potential yake ni Kama imeelekezwa sehemu ambayo sio sahihi kabisa.

Mtaalamu na Mbobezi wa maswala ya Elimu.
 
KIgangwaaaa.......laaaahaaa🤣

1000331782.jpg
 
Mama Tanzania amekuwa under utilized (Hajatumika vya kutosha)

Potential yake ni Kama imeelekezwa sehemu ambayo sio sahihi kabisa.

Mtaalamu na Mbobezi wa maswala ya Elimu.
Mkuu Unamaanisha Mama Tanzania anataka kuegemeza maisha yake kwenye Chama cha Siasa?
 
1.Alishindwa tu kusoma alama za nyakati na akasahau kuwa mcheza muziki mzuri ni yule anayeondoka kabla muziki haujaisha na watu bado wana hamu ya kumuona aki dance.

2.Aliishi kwa mazoea akiamini atashinda tu kama anavyoshindaga siku zote.

3.Kupoteza mvuto na kutokung'amua kuwa kapoteza mvuto.

Hakuna marefu yasiyokuwa na ncha.

Hakika kila lenye mwanzo lina mwisho.
 
Wadau!
Kama kichwa cha huu uzi kinavyosomeka hapo juu.

Swali la kujiuliza 🤔

Kwa nini binadamu aliyeifanyia makubwa Chadema, aliyejenga wasifu wa kipekee na uliotukuka kwenye siasa za upinzani na kupigania demokrasia Tanzania, Freeman Aikaeli Mbowe, jana alfajiri aliangushwa aliyekuwa msaidizi wake, Tundu Antipas Lissu?

Majibu ya swali hilo yanajibiwa na hoja mbili hizi hapa chini

1. Chama cha siasa kina mapenzi ya majira.
Leo kitakupenda sana, kesho kitakupuuza, keshokutwa kitakuchukia. Chama cha siasa kinaweza kukupamba kama shujaa asubuhi, jioni kikatangaza kuwa adui, usiku kikakufukuza.

2. Wanasiasa hukosea kuegemeza maisha yao kwenye vyama vyao.

Chama cha siasa hakina utu, kinaweza kukung'ang'ania mfe wote kisiasa, kama Prof Ibrahim Lipumba na Cuf, au kikakuua kwanza, kisha chenyewe kikaenda kufa sehemu nyingine, mithili ya James Mbatia na NCCR-Mageuzi.

Fanya siasa kwa akili. Wanachama na viongozi wenzako kwenye chama, siyo familia yako.
Wale punguani wenginawadanganya Hadi wanakufa unadhani watakuelewa? 😂😁
 
Wale punguani wenginawadanganya Hadi wanakufa unadhani watakuelewa? 😂😁
CHAMA CHA SIASA
LEO
kitakupenda sana,
KESHO kitakupuuza,
KESHO KUTWA kitakuchukia.
Kumbe Wajumbe Wanaonewa tu.
 
Back
Top Bottom