Usiginwaji wa Katiba Bungeni: Watetezi wa Haki za Binadamu nchini walaani. Wawakumbushia umuhimu wa kila raia kuilinda Katiba ya Nchi

Usiginwaji wa Katiba Bungeni: Watetezi wa Haki za Binadamu nchini walaani. Wawakumbushia umuhimu wa kila raia kuilinda Katiba ya Nchi

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
TAMKO KUHUSU UKIUKWAJI WA KATIBA YA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ULIOFANYWA NA SPIKA WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Ndugu Waandishi wa Habari,
Awali ya yote niwashukuru na kuwapongeza kwa kazi kubwa mnayoifanya hasa wakati huu ambapo dunia inaendelea kupambana na janga la virusi vya Corona (COVID 19). Sisi watetezi wa haki za binadamu tunapenda kuwatia moyo muendelee na kazi ya kutuhabarisha lakini bila kusahau kuchukua tahadhari za kutosha kujikinga na ugonjwa huu.

Ndugu Waandishi wa Habari,
Shirika la Elimu ya Uraia na Msaada wa Sheria (CILAO) limesikitishwa na kitendo cha Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kufanya maamuzi yanayokiuka misingi ya Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Itakumbukwa kwamba Bunge la Jamuhuri ya muungano wa Tanzania na Vyama vya siasa vinaongozwa kwa mujibu wa Katiba na sharia zingine za nchi. Ibara ya 71 ya Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania inaeleza wazi kuhusu ukomo wa mtu kuwa Mbunge. Kwa mujibu wa Ibara ya 71(1)(e) ya Katiba ni wazi kuwa Mbunge atapoteza nafasi yake ya ubunge ikiwa atapoteza uanachama wa chama chake kilichompatia ubunge wakati wa uchaguzi.

Mnamo tarehe 6 Mei 2020, Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu Job Ndugai, aliruhusu, aliyekua mbunge wa Ndanda, Bwana Cecil Mwambe ambaye aliishajiuzulu nafasi yake ya ubunge aendelee na kazi hiyo. Bwana Mwambe aliishaonekana katika vyombo vya habari akitangaza kujivua uanachama wa CHADEMA na kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM).

Kwa kuwa Cecil Mwambe alitangaza kijiondoa CHADEMA basi tunaamini pasipo shaka kwamba alipoteza tayari sifa ya kuendelea kuwa Mbunge wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ndugu Waandishi wa Habari,
Kitendo cha Spika kumruhusu kuendelea kuwa Mbunge ni ukiukwaji wa Katiba ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania na kwa kuwa Katiba inatamka wazi katika Ibara ya 26(1) kuwa kila RAIA ana wajibu wa kusimamia na kutetea Katiba na Sheria, sisi kama Taasisi kwa kushirikiana na wadau wengine tunakusudia haraka iwezekanavyo kufungua kesi Mahakama Kuu kuomba ufafanuzi wa Mahakama kuhusu kitendo hiki cha Spika.

Imetolewa leo tarehe 9 Mei 2020,

Na,

Odero Odero,
Mkurugenzi,
Civic and Legal Aid Organisation (CILAO)
CiLAO.png
 
Inawezekana Spika hana katiba katika desk lake maana kabla ya uamuzi wake huu angeweza kuisoma ibara hii ya katiba kwanza.

Ama kama sivyo, kuna uwezekana idara ya sheria na katiba ya taasisi ya Bunge ina vilaza watupu wa sheria.

Yeye katumia kigezo gani kumrejeshea ubunge mtu aliyeingia bungeni kwa udhamini wa chama cha siasa ambacho kishajivua uanachama wake?

Inawezekana yeye hakuona tamko la mbunge huyo kujivua uanachama wala chama chake hakijaliandikia bunge barua kulijulisha kuwa fulani siyo mwanachama wao tena.
 
Na ndio maana wakienda mahakamani wanashindwa, hiyo yote ni kuonyesha wasomi wetu wengi hajui wanachosimamia, utamkuta huyo mwanasheria wa haki za binadam hajui katiba na miongozo ya bunge inasemaje.

Wao wanakimbilia humu JF kisha wanaona hoja yao inashabikiwa vipi kisha wanavimba vichwa, wakienda huko wanashindwa wanaanza kusema haki haikutendeka.
 
Wabunge wamekula pesa za wananchi na kusepa hao Haki za Binadani wameziba masikio, mbunge kurudishwa bungeni kwa mapungufu ya sheria za vyama na kukosa umakini, wanachomoka na mbwembwe ooh tutaenda mahakamani.

Watuonyeshe ni kifungu gani cha Katiba ya nchi, au kanuni za bunge zimekiukwa na spika, kisha tuanzie hapo,
Vinginevyo waseme tu kuwa kuna vyama vikiguswa nao wanaguswa tujue,
 
Wabunge wamekula pesa za wananchi na kusepa hao Haki za Binadani wameziba masikio, mbunge kurudishwa bungeni kwa mapungufu ya sheria za vyama na kukosa umakini, wanachomoka na mbwembwe hoo tutaenda mahakamani,
Watuonyeshe ni kifungu gani cha katiba ya nchi, au kanuni za bunge zimekiukwa na spika, kisha tuanzie hapo,
Vinginevyo waseme tu kuwa kuna vyama vikiguswa nao wanaguswa tujue,
Ibara ya 71(1)(e) ya Katiba ya JMT--Mbunge atapoteza nafasi yake ya ubunge ikiwa atapoteza uanachama wa chama kilicho mdhamini wakati wa uchaguzi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna kosa kubwa kama kuvunja katiba.nchi zingine unanyongwa mazima.Kitendo kilichofanywa Na spika Ni cha kulaaniwa bila kuangalia itakadi zetu.Tanzania Ni yetu sote.
 
Back
Top Bottom