Usiginwaji wa Katiba Bungeni: Watetezi wa Haki za Binadamu nchini walaani. Wawakumbushia umuhimu wa kila raia kuilinda Katiba ya Nchi

Unachokizungumza hakina ukweli moja ya chanzo cha habari ni media na Professor Assad alihukumiwa na Bunge baada ya kuonekana akiongea na chombo cha habari cha magharibi ina maana Spika aliangalia mahojiano yale akamwita.

Kama kweli Spika ana nia njema kwanini asingemwita Mwambe kwenye kamati ajieleze kwamba ni kweli amehama uanachama au kusudio lake la kutangaza ni nin? Na kwenda Lumumba kupolelewa na Polepole.

Lakin kwasababu ana macho yenye makengeza na yeye tunamfahamu anayemtuma na kwa lengo gani hatuna budi kupiga kelele.

Kwaivo ukweli lazima usemwe.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi binafsi niwapongeze hao CILAO Kwa kuweza kufuatilia kwa ukaribu na kutuelimidha juu ya haki za kiraia.

Mmewaaeleza waaandishi wavhabari kuwa pamoja na Cecil Mwambe kutangaza kupitia vyombo vya habari Ni wazi atakuwa ameshapoteza uanachama wa chama chake na kupoteza sifa ya kuwa mbunge.

Kitendo Cha Mheshimiwa Spika wa bunge kumuita kuendelea na vikao vya bunge Ni kudigina Katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Nina maswali mawili kwenu Kama ifuatavyo:

1. Je mnathibitishaje Mwambe kutangaza kwenye vyombo vya habari kuwa amehama chama ndio tayari ameshajivua kwa mujibu wa Katiba ya chadema? Katiba ya chadema inasemaje mtu kujivua uanachama na chadema kiidhinisha kwamba huyo sio mwanachama?

2. Je, CHADEMA Taarifa yao ya maandidhi waliyoipeleka kwa Spika kuhusu Cecil Mwambe kuwa sio mwanachama ilikuwa na viambatanisho vya barua hiyo km vile mkutano wowote wa chama ulioidhinisha Mwambe kujivua uanachama?

3. Je, Kuna barua yoyote iliyoambatanishwa kwenda kwa Spika iliyoandikwa na Mwambe kujivua uanachama?

Natanguliza shukrani za dhati km majibu ya maswali haya yatatolewa na CiLAO

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tanganyika Law Society nini nafasi yao katika mambo ya kusigina katiba kama haya?
 
Rejea kuitangaza kuhama cdmna kujiunga ccm kwa lengo la kuunga juhudi kwa wabunge wa majimbo ya segerea, Serengeti, siha, monduli na mengine unayoyajua!

Je, cdm ilimwandikia spika barua rasmi au wao walioandika barua kwa spika na vyama vyao? Jibu ni hapana! Isipokuwa spika alisikika taarifa zao kutoka kwenye media na yeye bila kukishirikisha chama Cha cdm alikimbilia kuandika barua nec kuhusu majimbo hayo kuwa wazi!

Na hili lipo wazi kwa mujibu wa katiba ya URT ibara ya 71 kuwa mbunge akihama chama automatically anakosa sifa ya mwanzo ya kuwa mbunge! Hakuhitajiki barua ya kuthibitisha hili!

Spika, wanasheria wa bunge pamoja na AG wote washitakiwe kwa kuvunja katiba waziwazi!
 
Kama amekiuka Katiba si mchukue hatua kuliko kulalamika tu huku mtandaoni. Jamani inakera. Mahakama si zipo.
Utakuwa umesoma aya ya kwanza ukaja kuchangia mada bila kusoma mada yote
 
Kama amekiuka Katiba si mchukue hatua kuliko kulalamika tu huku mtandaoni. Jamani inakera. Mahakama si zipo.
Wewe ndio unalalamika hapo katuhabarisha tujue kinachoendelea. Kama kakukera pita kule
 
Ni kesi muhimu sana, tatizo Je , Tuna Makakama? Kuna Makahama Kuu yenye ubavu was kukataa "amri kutoka juu"?
Concern yangu ni hiyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu naomba nikujulishe kuwa ile tu watu kwenda kufungua mashitaka tayari ni ushindi kwa wahusika maana kwa sasa dunia ni kitongoji.

Tunacho hitaji ni kuweka kumbukumbu sawa maana hii nchi tumeikuta na tutaiwacha kwa wajukuu zetu

In God we Trust
 
Kama papai limeshafika ulaya kuwa lina corona, unadhani kesi ya kufunguliwa mahakamani itashindwa kuwafikia wahusika wa haki za binadamu?
Mahakama itasema inaogopa kugonganisha mihimili.

In God we Trust
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…