USIKU WANGU HUU! (shairi)

USIKU WANGU HUU! (shairi)

Swahilian

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2009
Posts
591
Reaction score
69
Usiku wangu umefika' natamani pale n'geshika'
Usiku wangu huu aah! nsingetaabika'
Moyo wangu huu! usingehuzunika'
Ningefika wakati huu aah! nsingechoka'

Ndoto yangu hii! lazima ingetimilika'
Lakini mmh! hakika nataabika'
Pangu pakavu pa mwenzangu patiririka'
Wale wanapeana huku wanacheka'

Kesho hivyo hivyo hadi kumwagika'
Usiku wangu huu! sijui nami ntaota na kuokoka'
Labda weye mwenzangu usiku wako ni sawa na huu!
Au weye ndo kuukuu?
 
Back
Top Bottom