Usilogwe ukaondoka nyumbani na kwenda usipopajua kwa kigezo cha kutafuta maisha

Usilogwe ukaondoka nyumbani na kwenda usipopajua kwa kigezo cha kutafuta maisha

"Usilogwe ukaondoka nyumbani na kwenda usipopajua kwa kigezo cha kutafuta maisha"
Mwanaume unatafuta maisha popote pale unapoona kuna fursa hata km hauna ndugu.
Mm mwenyewe ni mfano hai, hapa nilipo nilikuja sina ndugu wala rafiki. Nililipa chumba miezi 3 nikabakiwa na 2,000 tu mfukoni. Natandika boksi nakujifunika shati, nimeshalala na njaa mpk siku 2 lkn sasa najimudu maisha. Nalala sehemu safi na nimeoa.
Maisha popote haijalishi una ndugu au hauna huko.
Itaendelea
 
"Usilogwe ukaondoka nyumbani na kwenda usipopajua kwa kigezo cha kutafuta maisha"
Mwanaume unatafuta maisha popote pale unapoona kuna fursa hata km hauna ndugu.
Mm mwenyewe ni mfano hai, hapa nilipo nilikuja sina ndugu wala rafiki. Nililipa chumba miezi 3 nikabakiwa na 2,000 tu mfukoni. Natandika boksi nakujifunika shati, nimeshalala na njaa mpk siku 2 lkn sasa najimudu maisha. Nalala sehemu safi na nimeoa.
Maisha popote haijalishi una ndugu au hauna huko.
Sa mbona nawewe hujaleta stori yako inayohimiza watu waende sehemu wasizozijua kutafuta maisha
 
SEHEMU YA NANE

Ilipoishia,,,,,,,,,,,,,,

Asubuhi wanakuja rafiki zake pale, ni wale nlikuwa nawaona pale wanajiuza, akawa anawatambulisha kuwa mi ni shemeji yao, basi sawa, nikakaa paka mchana tukala ugali fresh, Nikaondoka zangu kurudi chuo

Endelea,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

Nikafika chuo nikalala sana siku hiyo maana hatukuwa na pindi, Nilipo kuja kushtuka nikaanza kutafakari yote yaliyotokea jana, Nikajilaumu sana maana hii yote ni sababu ya kuanza mapenzi ukubwani,

Basi ikawa ndo tabia yangu, usiku ukifika natinga kofia yangu najiachia buguruni, Nafanya yangu huko narudi room night kali nalala, Siku moja nikiwa na Jane kwenye vile vyumba vya short time mara mlango ukagongwa kwa nguvu, " Tokeni huko nyie washenzi" , Jane akaniambia hao ni polisi, Nikasema mbona hiki kisanga tena, sasa itakuwaje, itakuwaje sasa? Akasema kwa nyie hawana shida, kwa sisi ndo shida,

Basi mlango ukaendelea kugongwa, Jane akaenda kufungua, jamaa wakaingia wakatukamata na matusi kibao, tukatoka nje, kuna wengine nao wamekamatwa, Basi sisi wanaume tulikuwa kama sita, tukafungwa mashati wawili wawili, tukaswagwa na wale mademu paka kwenye gari ya polisi,

Tukazama ndani, tume kaa chini gari ikaamsha, Nikamuuliza Jane hapa tunaenda wapi? Akasema kituoni,
Basi tukazungushwa pale buguruni, mwisho tukapelekwa kituoni buguruni rozana , tukaambiwa vua mikanda,vua viatu, toa kila kitu weka mezani, tukafanya hivyo,

Haya kaa chini, tukaandikishwa majina pale, tuka kaa tunaskilizia, wale maaskari tuliokuja nao na gari wakawa wameondoka na gari, wakabaki wale tuliokuwa tumewakuta pale kituoni,

Baada kama lisaa tukiwa tumekaa pale nawaza sijui itakuwaje taarifa zilifika chuo, nikiwa bado nawaza, ndipo askari mmoja akasema oyaa, nyie semeni mna nini muondoke hapa, mkikaa hapa paka kesho tunawapeleka mahakamani, nikasema ukisikia kirangasi ndo hichi sasa,

Basi jamaa mmoja akasema mi nna elf 10 afande, Nikasikia we mwana haramu nini!! Yaan hao malaya uwape elf 10 na sisi utupe elf 10! Hanisi wewe, eeenh na nyie wengine, Mi nikasema nna elf 10 pia, Yule afande akasema nyie mna leta utani, ebu sogeeni hapa,

Basi tukaenda pale mezani, Akasema toeni hizo hela, Basi mi nikaomba walet yangu ilikuwa pale mezani, nikatoa buku ten, nikachukua vitu vyangu nikasepa, na wale wengine nao wakatoka tukawaacha wale mademu kule maana walikuwa chumba kingine, Basi nikatoka pale nikadandia gari nirudi zangu chuo, moyoni najiapiza sirudii tena yaan leo ndo mwisho, nikarudi room nikalala,

Ikapita kama wiki hivi sjatia maguu tena buguruni, Ila badae uzalendo ukanishinda, nikaona usintanie nikajiachia huyooo kama kawa, Nikakutana na Jane nikamuuliza siku ile ilikuwaje, akasema walilala paka asubuhi pale kituoni, kesho yake wakadeki mule ndani na kufagia nje alafu wakaachiwa,

Basi ikawa ndo tabia yangu, siku nyingine simtafuti Jane nabadilisha ladha, Nikaotea chimbo lingine mwanzoni huku kabla hujafika sheli kunasehemu wanauza mbao, basi pale ni chap kwa haraka, nyuma ya zile mbao tu mmna malizana unampa buku tatu yake unasepa,

Basi siku moja nipo room Happy akanipigia akaanza kuongea analia, analalamika siku hizi nimemtupa hata simpigii, Nikajitetea pale kwamba shule imekaba ndo maana, Alafu akaniambia kwamba ana miezi kadhaa haoni siku zake, Ukisha ambiwa hivyo unajua tu ni nini kinafata,

Basi akasema anahisi ana mimba maana dalili zote zimeshajionesha hadi home wameshamtilia mashaka, Basi nikampooza pale kuwa ntamtumia hela aende hospital akapime, Basi tukaongea mengi, nikaahidi bado nna mpenda na hata kama ana mimba mimi kwangu ni furaha kuitwa baba,

Basi siku zikaenda, test zikaja, UE hii hapa, tukapiga pale shule ikaisha watu wakasepa zao kwenye mafield huko, Mimi field yangu nikafanyia hapa hapa Dar, Happy nikamtumia hela akaenda kupimwa akakutwa na mimba ya miez mi nne, Kidume ukiskia mziki ndo huo, Basi home kwao walipogundua dingi yake akamfukuza aende kwa mwanaume alie mpa mimba, Basi akaenda kuishi kwa Anti yake kijiji cha jirani,

Itaendelea

Huyu mjinga ni wakula ban haiwezekani hadi sasa unaendelea kuleta hadithi za uongo uongo ili uonekana shujaa
 
SEHEMU YA TISA

Ilipoishia,,,,,,,,,,,,

Basi home kwao walipogundua dingi yake akamfukuza aende kwa mwanaume alie mpa mimba, Basi akaenda kuishi kwa Anti yake kijiji cha jirani,

Endelea,,,,,,,,,

Field ikaenda poa, mchakato wa kurudi chuo ukaanza tena, mwaka wa tatu huo tunaingia, ila saivi nikasema skai tena campas, na mimi nataka saivi niende mtaani, Nikamcheki jamaangu Kidosho yeye alikuwa anakaa msewe, Nikamweleza na mimi nataka nipange mtaani , Akasema si bora uje tukae wote hapa tushirikiane kulipa kodi, Mi nikaona ni wazo zuri, tena ukizingatia wote tunasoma kozi moja itakuwa rahisi kufanya discusion,

Basi bumu lilivyotoka tukanunua kitanda kikubwa, jiko la gasi plate 2, meza nzuri ya kusomea, sabufa, basi geto likapendeza, shule ilienda vizuri sana, Getoni wakawa wanakuja wenzetu tunapiga discusion la maana pale,

Kifupi shule haikuwa ngumu sana kulinganisha na mwaka wa pili, Basi semista ikakata, mi sikwenda kijijini nikabaki pale geto tu maana wiki mbili si nyingi, Nyumbani Happy akajifungua mtoto wa kike, wakanitumia picha katoto keupe kama mama yake basi nikakapa jina Joyce kama bibi yake,

Tukafungua shule, semista ikaanza tukaikimbiza nayo ikakata, tukaenda field tena, Mimi kama kawa field yangu ni hapa hapa Dar, Basi tukamaliza field, tukaanza tena mwaka wa nne, tukawa tunaenda chuo kama kipindi ni asubuhi na kingine mchana basi tunakaa kwenye vimbweta tunajisomea paka kile cha mchana kifike tukitoka ndo twende nyumbani, kuliko nenda rudi,

Siku moja nimetulia zangu kwenye vimbweta vya NMB pale Coet nakula msuli taratibu, mara naona kimbweta cha mbele kakaa mdada mmoja bonge hivi alafu kavaa kimini, mbaya zaidi kageukia huku mimi nilipo, Basi kama kawaida yangu mzee chabo nikaanza kufanya yangu huku nazuga nasoma, Kumbe yule sista kanishtukia nna mla chabo, basi akawa anatanua mapaja alafu ana bana, anatanua anabana, ndani kavaa taiti nyeupe, kumcheki usoni naona ananiangalia alafu anatabasamu,

Basi mi nikajifanya nipo serious napiga msuli simwangalii, Sjakaa vizuri mara naskia "ulikuwa unachungulia nini?" Kucheki dada huyu hapa , kaja kwenye kile kimbweta changu, akaniambia soogea tukae wote, basi nikajisogeza akakaa, akaniuliza unasoma nini hapo? nikamwambia hii inaitwa engineering thermodynamics, Akasema we unasoma engineering nikamwambia ndio , akasema hongera, nikamuuliza kwanini? akasema naskia hiyo engineering ni balaa, upo mwaka wa ngap? nikamwambia wa nne, basi tukapiga stori pale, akasema yeye anaitwa Sity, yeye hasomi pale, bali pale kaja kujisomea tu, yeye anasoma chuo cha magogoni anasomea certificate of record management,

Mtoto ni mzuri huyo, choclate flani hivi, ana vidimpo vya kuibia, kajaa kidogo alafu huko nyuma sasa ni masha allah si kitoto, tukapiga stori pale ikafika mchana nikampeleka cafteria ya block A pale tukapiga menyu,

Basi mi nikamuaga maana muda wa pindi ulikuwa umefika, alafu pindi lenyewe yombo hukoo, Basi tukapeana namba pale mi nikasepa,

Basi usiku nikiwa na kidosho tunapiga stori mara mtoto akaniendea hewani, akaniuliza kama kesho naenda chuo nikamwambia sina kipindi ntakuwa geto tu, basi akasema atakuja geto tusome, nikamwambia poa,

Moyoni nikasema huyu mtoto ananitaka nini!!!, Haya bana,kesho yake mida mida hivi kweli mtoto akatimba, kanipigia suruali hiyo imebana, nikasema khaah huu mzigo nitauweza kweli? Basi kidosho akajikataa zake akaniacha geto na mtoto,

Tukaanza kusoma, yeye kaja na kadaftari chake kameandikwa mambo ya register, sijui what is register, sijui importance of register, bana atajua mwenyewe, Mi najifanya nasoma ila msuli haupandi, yaani nikimcheki mtoto nahis kuchanganyikiwa, ukichanganya na perfum yake ndo ananimaliza akili kabisa,

Basi nikajikaza kidume ila uzalendo ukanishinda baaria, nikamwomba gemu mtoto, akagoma kata kata, akasema hawez kufanya mapenzi na mtu hata hamjui vizuri, akipata virusi je? Akasema kama nataka twende kwanza tukapime, basi mzee mzima nikawa sina jinsi nikawa mpole tukaendelea kusoma,

Basi tukapanga siku twende pale zahanati ya chuo tukapime, nikasema poa maana ile zahanati ya chuo naiamini, chochote utachopima pale utaambiwa hauna, kuna siku nilienda pale nnaumwa balaa, yaan nashikiliwa nisianguke, ajabu nikapimwa maleria nikaambiwa sina, kwenda kairuki kupima nakutwa na maleria za kufa mtu, basi nikasema pale ukienda kupima hata uzito si ajabu ukaambiwa hauna

Basi siku ikafika mi na Sity hao tukatimba pale zahanati, nikiwa na imani kabisa haitaniangusha, basi tukamwambia yule nesi kuwa sisi ni wapenzi kwaiyo tumekuja kujua afya zetu, Akatupa nasaha zake pale mwisho akatutoa damu akaweka kwenye kidude chake kile akatuambia tukasubiri nje atatuita, basi tukatoka,

Tukiwa tumekaa nje kwenye benchi tunapiga stori mara tukaitwa kule ndani, Basi nesi akatuambia majibu yenu tayari, ila kwa kuwa ninyi ni wapenzi na mna aminiana basi kila mmoja atasoma majibu ya mwenzake, tukasema sawa, basi mi nikapewa ya Sity na Sity akapewa yangu, Basi sity alipofungua majibu asome mara ghafla akashtuka kwa nguvu,

Itaendelea
 
Katika hali ya kawaida unawezaje kukumbuka vitu vya miaka zaidi ya 5 au zaidi iliyopita kwa 'detail' hivyo? Naona kama ni ngumu sana....

Vyovyote vile hadithi ni nzuri iwe ya utunzi au ya kweli. Nahisi wewe ni mtunzi maana unaishia sehem zenye 'suspense' ili msomaji ifuatilie kiliendelea nini kwneye muendelezo.
 
Back
Top Bottom