Usilolijua kwa Hamornize ni ujenzi mpya wenye mvuto. Fagio lake mtalishukuru baadae

Usilolijua kwa Hamornize ni ujenzi mpya wenye mvuto. Fagio lake mtalishukuru baadae

mgt software

JF-Expert Member
Joined
Nov 1, 2010
Posts
13,778
Reaction score
7,145
Wana JF

Watu wengi wamekalia lawama nyingi sana na kuhukumu kila kukicha nafasi ya kondeboy Harmonize katika mikakati ya kuangushwa na mpenzi wake na mtu mzima Kajala.

Pengine ufagio mpya alioutumia unaonekana kuwakera wengi tu lakini kwa jicho jipya ni kwamba kisafisha nyumba na kuweka vitu vipya si jambo geni wala si la kubeza kwani ni mikakati ya kusajiri timu yenye uwezo koupinzani.

Kwa hakika kondeboy ndiye mtu makini anayeweza kushindana na diamondi kwa karibu kwani Ali Kiba ashatupwa, kondegang ni lebo ambayo inapigiwa chapuo na watu wengi kuleta ushindani mkubwa wa kimziki.

Mwanzoni kabisa harmonise alikuwa akipiga miziki ya vijembe na majibizano na malalamishi kwa kile alichotendewa na hasmu wake.

Ni muda sana akaona anapoteza muda kwani wasanii wa WCB lebo alikotoka walikuwa bize kumlipia bosi wake ambaye hakuwahi kujibu lolote.

Wasanii wake walikosa muda mzuri kuburudisha watu kwa kipindi kile cha malalamishi. Sasa kondeboy ameona kwenye ushindani nguvu nyingi zinapelekwa kwenye kushadadia mapenzi ndiko watu hutoboa, alipojaribu ndio watu wakaanza kuona sasa anaweza. Kondeboy wasanii wake wamepooza sana.

Hivyo inabidi afanye usajiri makini utakaomlipa mapema ndio maana kaamua kupurula woote aanze upya. Kajala kwa kuwa ni jina kubwa kuna watu wanadhani anamdrive.

Kwanza walianza kwa kutengeneza follower muhimu. Kifuatacho ni kusakiri vijana wenye uwezo wa kutunga mashahiri bora na ya viwango. Msimbeze sana kazi ya kusajiri ngumu sana. Naona anaenda kutoboa huyu kijana
 
Bado Ibrah duuh Kajala ana Uroho wa Madalaka ya Kulevya, hatimae angel.....atabaki analia
 
Tatizo vi
Bado Ibrah duuh Kajala ana Uroho wa Madalaka ya Kulevya, hatimae angel.....atabaki analia
Tatizo vijana wanapewa fedha hawajitumi kabisa. Anajenga team mpya. Usajiri makini unahitajika sana
 
Wana JF

Watu wengi wamekalia lawama nyingi sana na kuhukumu kila kukicha nafasi ya kondeboy Harmonize katika mikakati ya kuangushwa na mpenzi wake na mtu mzima Kajala.

Pengine ufagio mpya alioutumia unaonekana kuwakera wengi tu lakini kwa jicho jipya ni kwamba kisafisha nyumba na kuweka vitu vipya si jambo geni wala si la kubeza kwani ni mikakati ya kusajiri timu yenye uwezo koupinzani.

Kwa hakika kondeboy ndiye mtu makini anayeweza kushindana na diamondi kwa karibu kwani Ali Kiba ashatupwa, kondegang ni lebo ambayo inapigiwa chapuo na watu wengi kuleta ushindani mkubwa wa kimziki.

Mwanzoni kabisa harmonise alikuwa akipiga miziki ya vijembe na majibizano na malalamishi kwa kile alichotendewa na hasmu wake.

Ni muda sana akaona anapoteza muda kwani wasanii wa WCB lebo alikotoka walikuwa bize kumlipia bosi wake ambaye hakuwahi kujibu lolote.

Wasanii wake walikosa muda mzuri kuburudisha watu kwa kipindi kile cha malalamishi. Sasa kondeboy ameona kwenye ushindani nguvu nyingi zinapelekwa kwenye kushadadia mapenzi ndiko watu hutoboa, alipojaribu ndio watu wakaanza kuona sasa anaweza. Kondeboy wasanii wake wamepooza sana.

Hivyo inabidi afanye usajiri makini utakaomlipa mapema ndio maana kaamua kupurula woote aanze upya. Kajala kwa kuwa ni jina kubwa kuna watu wanadhani anamdrive.

Kwanza walianza kwa kutengeneza follower muhimu. Kifuatacho ni kusakiri vijana wenye uwezo wa kutunga mashahiri bora na ya viwango. Msimbeze sana kazi ya kusajiri ngumu sana. Naona anaenda kutoboa huyu kijana
Tokea aanze kushindana na Diamond kafikia wapi?

Ogopa sana mtu anaye shindana na target zake,Mondi anatarget zake na ndio maana kila anacho kifanya tayari kisha kifanyia calculation,hata yeye mwenyewe mpaka alipofikishwa na Mondi,tayari Mondi alishapiga calculations mapema.

Huyo Konde mkurupukaji label kaanzisha kwa kukurupuka,wasanii kawa sajili kwa kukurupuka, hata nyimbo anatoa kwa kukurupuka, nyimbo nyingi ila total streaming zina karibia na Zuchu aliyetoa nyimbo chache.

Labda kama ukiniambia anashindana na wasanii wake wa Kondegang kutoa nyimbo hapo nitakubali tena anawafunika na kuhakikisha hawasikiki na ndio maana wana mkimbia.
 
mnapenda kumtaja alikiba kwenye upupu wenu hasa mkiishashiba makande.
 
Hamonaiz ameshajambiwa na yule bibi mademu zake watakua mabibi tu
 
Namkubali Harmonize, kila la kheri kwake
 
Ingekuwa vema abaki peke yake kwanza...kusimamia wasanii bado sana kwa levels zake
 
Usimtetee, kawatumia hao vijana kupata huruma ya jamii ili ajinufaishe yeye mwenyewe.

Kawapotezea muda, kawaacha kinyemela na hawana nguvu ya kujisimamia.

Kama hawa kawashindwa hao waandika mashairi makali watakuja na fedha zao za kuendesha muziki wao???

Watu wamuelewe huyu kijana, kila anachofanya anahakikisha kinamnufaisha yeye pekeake. Kama hana uwezo wa kusimamia wasanii afanye sanaa yake mwenyewe.
 
Nimemhurumia Angel aisee.

Nadhani alitegemea kondegang ndo mkombozi wa matatizo yake mwisho wa siku wana wamekula pesa wamemtema.

Ila kama wamemuachia social platforms zake sio mbays ila kama ndo ile meneja wake alivosema mpaka alipe billion 1, itakua mbaya sana aisee.
 
Tunamuombea ila kwenye lile chaka alimoingia tumuombee sana sana.. Maana historia haidanganyi
Mkuu ilibidi nicheke kwanza. Mtu ana fedha. Vitoto vizuri chuchu saa sita unaviacha unavamia vibibi upwelepwete
 
Back
Top Bottom