Usilolijua: Mafundi ujenzi waongo ndio wamesaidia maskini kujenga nyumba zao kwa sababu hizi

Usilolijua: Mafundi ujenzi waongo ndio wamesaidia maskini kujenga nyumba zao kwa sababu hizi

Wana JF,

Duniani hakuna fundi ujenzi ambao sio waongo, tumekuwa na ugomvi kubwa mpaka kimataifa tukishitakiana na makampuni mbalimbali hadi haya kushindwa kesi au kushinda kesi. Kitaifa mpaka sasa tunamwona Jafo, Mbalawa na Kamwele wanavyokimbizana na mafundi wasiomaliza kazi.

Tuje MTU na MTU, sisi kwa sisi, fundi ujenzi atakuja kwako atakupa mahesabu mpaka nyumbani inaisha, hapo si nawe unachomoa tu million 30 eti nyumba itaisha thubutu. Pesa nyumba itapanda mpaka linta baada ya hapo Pesa inakata, kama ulikuwa na wazo la kumkimbia mama mwenye nyumba na ushaanza ubishoo hapo patamu, hapo hata hela yabkunua msumari hauna kabisa, ndipo fundi uingia hatua mpya ya kukufanya umalize nyumba, atakushauli uzibe madrisha machache uwezeke uoande nmoja amia, kufuatana uwezo hauna utamsikiliza na kuondokana kero za mama mwenye nyumba kwani ashataka uondoke apandishe kodi kwani wewe hawezi kukupandishia, vijemba vya hamia kwako haviishi.

Ndipo hasira hukutuma kuhamia hivyo hivyo kama hakuna mvua unanunua tundubali la muda unaanza ndogo ndogo. Ukisikia kuanza maisha ndio huku. Utaanza kukusanya mabati Mbao huku ukikimbizana na majira ya mvua. Bia moja utakuwa unahiesabia tofali, bia mpaka upewe ofa. Choo pipa la kutumbukiza. Mlango kipande cha blamketi.

Fundi haachi kuja kwa kuwa anajua ashakutia akili na ashakutia kimeo, ndipo uanza kukupa mawazo ya kuwezeka upande, wewe unakuwa na hasira unaezeka yote, hapo mawazo yanakuwa angalau afadhali inaanza kuitwa nyumba baada ya kuezeka wanaacha kuliita pagale, na kulambia madem vinuka mkojo au kupafanya choo ya majirani.

Hasira na mahesabu feki ndiyo umsaidia maskini ajenge kwani akipewa sahihi nyumba ya tsha mil 40 hawezi jenga
Nakukumbusha pia fundi huyo huyo naweza kukupeleka sehemu inakopeshwa materials lakini ajbi yeye hakopeshi labour charge zake.yeye anapita na cash yake kama ilivyo hakopeshi hata mia[emoji85][emoji85][emoji85][emoji85]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jenga Msingi wa Nyumba nzima kama ilivyo kwenye Ramani yako. Kisha pandisha master bedroom na chumba kinachopakana fanya kila kitu, Lipu, Rangi, Wiringi, Umeme, Maji safi, shimo la maji taka N.K kisha hamia kwingine utamalizia ukiwa hapo hapo ndani kwako.
The best approach, nimeishuhudia kwa wengi wakifanya hivyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakukumbusha pia fundi huyo huyo naweza kukupeleka sehemu inakopeshwa materials lakini ajbi yeye hakopeshi labour charge zake.yeye anapita na cash yake kama ilivyo hakopeshi hata mia[emoji85][emoji85][emoji85][emoji85]

Sent using Jamii Forums mobile app
ukitaka kumpata akukopese subiri kipindi cha mvua wengi hawana kazi, kazi kama za lipu, kupiga blandaling, rangi kazi yote ya ndani kama kuweka tylies anakufanyia tu, lakini wakati wa jua kali bei huwa juu kishenzi maana hata mchanga wanaupata kirahisi
 
UJENZI UWA HAUISHI..
Mteja anakuja dukani anakwambia ndugu yangu asubuhi nilikuja na milioni 3 lakini mpaka sasa zimebaki laki 5..
Na hapo nyumba ipo kwenye foundation tu.
"MTU akijenga muheshimu hata kama ni chumba kimoja"


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom