OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 53,868
- 121,001
Sio kweliUnaenda mahakamani na ivyo viambata Kisha utapewa fomu mbili moja ya kuomba kuteuliwa kuwa msimamizi wa mirathi na nyingine ya wadhamini utazijaza, iyo ya kuomba kuteuliwa kuwa msimamizi utairudisha ikiwa imeambatanishwa na passport size za wanufaika, nikiimaanisha watoto wa marehemu, mume/mke. Kisha taratibu nyingine utapewa uko uko
Unatakiwa kuwa na;Vikiwepo hivyo naanzia wapi
Yeah uko sahihi Kaka, na kingine Kama hakuna vitu vingi wanaweza maliza kwa utaratibu nzuri Kama waki elewana.Unatakiwa kuwa na;
1. Kibali cha mazishi
2. Muhutasari wa familia kumteua msimamizi wa mirathi, orodha ya mali za marehemu na majina ya wategemezi wa marehemu. Muhutasari uwe na muhuri wa mtendaji wa kijiji/mtaa
3. Kama msimamizi ni mwanandoa uwe na cheti cha ndoa
4. Uwe na details za marehemu na msimamizi
Vyote hivyo unapeleka RITA. Utajaza kwenye mfumo taarifa zote za marehemu pamoja na msimamizi hapo RITA. Utalipia elfu 7. Ndani ya mwezi watakupa cheti cha kifo (death certificate).
Baada ya hapo peleka mahakama ya mwanzo hicho cheti cha kifo, cheti cha ndoa, kibali cha mazishi na muhutasari wa familia. Usiende mahakamani bila barua ya utambulisho wa wewe na wadhamini wawili kutoka kwa mtendaji. Pale mahakamani kuna form utajaza na kuonana na hakimu pamoja na wadhamini wako.
Atakupa tangazo la wito wa kusomwa shauri la mirathi ukapandike eneo la makazi ya marehemu. Kwenye hiyo tarehe mtahudhuria wewe na ndugu hasa wanufaika wa mirathi. Kama hakuna gogoro msimamizi atagawa mali na kutoa taarifa mahakamani
Yeah, kama hana mali zitakazohitaji documents za mahakama. Mfano pensheni, viwanja vyenye hati, fedha benk, TRA kubadili kadi nk. Tofauti na hapo hataweza kupata. Ukienda ardhi kubadili hati, NSSF, benk watakwambia lete docs za mahakama.Yeah uko sahihi Kaka, na kingine Kama hakuna vitu vingi wanaweza maliza kwa utaratibu nzuri Kama waki elewana.
Yap, Sema mahakamani Wana mizunguko, mfano awe na pension, dah inaeza chukua hata miezi 6Yeah, kama hana mali zitakazohitaji documents za mahakama. Mfano pensheni, viwanja vyenye hati, fedha benk nk. Tofauti na hapo hataweza kupata. Ukienda ardhi kubadili hati, NSSF, benk watakwambia lete docs za mahakama.
Nenda mahakama ya mwanzo ya karibu yako watakuelekeza yote.Vikiwepo hivyo naanzia wapi
Mkuu, mzigo huu hapaMkuu unaweza kushare link
Kazanazo Uzi huu wenye majibu ya kina.Mkuu, mzigo huu hapa
Kwa nini mtoane Roho kwa mali alizoacha baba? Ijue Sheria ya MIRATHI, WOSIA na Usimamizi wa mali zitokanazo na Mirathi
Binadamu wote ni lazima tupitie kifo ikiwa ndio mwisho wa maisha yetu hapa duniani. Wakati wa uhai mtu unaweza kumiliki mali zinazohamishika na zisizohamishika mahali tofauti tofauti ndani au nje ya nchi ya Tanzania. Kuondoka kwako duniani kwa njia ya kifo hakufanyi mali zako zipotee kwa...www.jamiiforums.com
Kufupisha muda ni mpaka umuone pembeni muheshimiwa hakimu, umtoe kidogo. Watu hawana huruma, umefiwa lakini wanakupigaYap, Sema mahakamani Wana mizunguko, mfano awe na pension, dah inaeza chukua hata miezi 6
Ehh, maana kama Yuko wilayani kazi IPO, ata ambiwa mweja hazina wa mahakama kasafiriKufupisha muda ni mpaka umuone pembeni muheshimiwa hakimu, umtoe kidogo. Watu hawana huruma, umefiwa lakini wanakupiga
🧐Mirathi yenyewe kiwanja cha lak3 tu mkuu nipe tu muongozo unisaidie na uwasaidie wengine
Ahsante sana mkuuUnatakiwa kuwa na;
1. Kibali cha mazishi
2. Muhutasari wa familia.Minute iwe na uteuzi waa msimamizi wa mirathi, orodha ya mali za marehemu na majina ya wategemezi wa marehemu. Usiandike mgao wa mali humo. Muhutasari uwe na muhuri wa mtendaji wa kijiji/mtaa
3. Kama msimamizi ni mwanandoa uwe na cheti cha ndoa. Kama mtoto uwe na cheti cha kuzaliwa.
4. Uwe na details za marehemu na msimamizi
Vyote hivyo unapeleka RITA. Utajaza kwenye mfumo taarifa zote za marehemu pamoja na msimamizi hapo RITA. Utalipia elfu 7. Ndani ya mwezi watakupa cheti cha kifo (death certificate).
Baada ya hapo peleka mahakama ya mwanzo hicho cheti cha kifo, cheti cha ndoa, kibali cha mazishi na muhutasari wa familia. Usiende mahakamani bila barua ya utambulisho wa wewe na wadhamini wawili kutoka kwa mtendaji. Pale mahakamani kuna form utajaza na kuonana na hakimu pamoja na wadhamini wako.
Atakupa tangazo la wito wa kusomwa shauri la mirathi ukapandike eneo la makazi ya marehemu. Kwenye hiyo tarehe mtahudhuria wewe na ndugu hasa wanufaika wa mirathi. Kama hakuna gogoro msimamizi atagawa mali na kutoa taarifa mahakamani
Mkuu kama kuna kiwanja tu, hapo mna eza kubaliana kwa maandishi kuwa mmiliki ni Huyu na huyu.Samahan mkuu utaratibu mzuri kivipi tunaelewana tu ni kuwa tunataka kutambulika kisheria ila hatuuzi urithi
Ahsante mkuu nimepata kuelewa baadhi ya maswali niliokuwa nayoMkuu, mzigo huu hapa
Kwa nini mtoane Roho kwa mali alizoacha baba? Ijue Sheria ya MIRATHI, WOSIA na Usimamizi wa mali zitokanazo na Mirathi
Binadamu wote ni lazima tupitie kifo ikiwa ndio mwisho wa maisha yetu hapa duniani. Wakati wa uhai mtu unaweza kumiliki mali zinazohamishika na zisizohamishika mahali tofauti tofauti ndani au nje ya nchi ya Tanzania. Kuondoka kwako duniani kwa njia ya kifo hakufanyi mali zako zipotee kwa...www.jamiiforums.com
Ni kweli mzee haukuacha vitu vingi sana ni just mashamba na nyumbaMkuu kama kuna kiwanja tu, hapo mna eza kubaliana kwa maandishi kuwa mmiliki ni Huyu na huyu.
Maana Kuna mirathi ya kisheria na Ile ya zamani..
Kama Kuna pension, nyumba, mna fata utaratibu tu